1Hoću reći: sve dok je baštinik maloljetan, ništa se ne razlikuje od roba premda je gospodar svega:
1Basi, nasema hivi: mrithi, akiwa bado mtoto, hawi tofauti na mtumwa ingawaje mali yote ni yake.
2pod skrbnicima je i upraviteljima sve do dana koji je odredio otac.
2Wakati huo wote yuko chini ya walezi na wadhamini mpaka wakati ule uliowekwa na baba yake.
3Tako i mi: dok bijasmo maloljetni, robovasmo počelima svijeta.
3Hali kadhalika na sisi tulipokuwa bado watoto, tulikuwa watumwa wa pepo watawala wa ulimwengu.
4A kada dođe punina vremena, odasla Bog Sina svoga: od žene bi rođen, Zakonu podložan
4Lakini wakati ule maalumu ulipotimia, Mungu alimtuma Mwanawe aliyezaliwa na mwanamke, akaishi chini ya Sheria
5da podložnike Zakona otkupi te primimo posinstvo.
5apate kuwakomboa wale waliokuwa chini ya Sheria ili sisi tufanywe wana wa Mungu.
6A budući da ste sinovi, odasla Bog u srca vaša Duha Sina svoga koji kliče: "Abba! Oče!"
6Kwa vile sasa ninyi ni wana, Mungu amemtuma Roho wa Mwanae mioyoni mwenu, Roho ambaye hulia "Aba," yaani "Baba."
7Tako više nisi rob nego sin; ako pak sin, onda i baštinik po Bogu.
7Basi, wewe si mtumwa tena, bali mwana. Na ikiwa ni mwana, basi, wewe utapokea yote Mungu aliyowawekea watoto wake.
8Onda dok još niste poznavali Boga, služili ste bogovima koji po naravi to nisu.
8Zamani hamkumjua Mungu na hivyo mkatumikia miungu isiyo miungu kweli.
9Ali sada kad ste spoznali Boga - zapravo, kad je Bog spoznao vas - kako se sad opet vraćate k nemoćnim i bijednim počelima i opet im, ponovno, hoćete robovati?
9Lakini sasa, kwa vile mnamjua Mungu, au tuseme mnajulikana na Mungu, mnawezaje tena kurudi kwa wale pepo maskini na dhaifu hata kutaka kuwatumikia tena?
10Dane pomno opslužujete, i mjesece, i vremena, i godine!
10Bado mnaadhimisha siku, miezi na miaka!
11Sve se bojim za vas! Da se možda nisam uzalud trudio oko vas!
11Nahofu kwamba labda kazi niliyoifanya kwa ajili yenu imepotea bure!
12Postanite, braćo, molim vas, kao ja jer i ja postadoh kao vi. Ničim me niste povrijedili.
12Ndugu, nawasihi muwe kama mimi, kwa vile hata mimi nimekuwa kama ninyi. Hamkunitendea ubaya wowote.
13Znate: prvi sam vam put za bolesti navješćivao evanđelje.
13Mnajua kwamba ugonjwa wangu ndio ulionipatia fursa ya kuwahubirieni Habari Njema kwa mara ya kwanza.
14Svoju kušnju, moje tijelo, niste ni prezreli ni odbacili, nego ste me primili kao anđela Božjega, kao Krista Isusa.
14Hata hivyo, wakati ule hamkunidharau wala kunikataa kwa sababu ya udhaifu wangu ingawa mlishawishiwa kufanya hivyo; lakini mlinipokea kama malaika wa Mungu, kama vile ningekuwa Kristo Yesu mwenyewe.
15Gdje je sada ono vaše blaženstvo? Svjedočim vam doista: kad bi bilo moguće, oči biste svoje bili iskopali i dali mi ih.
15Mlikuwa wenye furaha; sasa kumetokea nini? Naapa kwamba wakati ule mngaliweza hata kuyang'oa macho yenu na kunipa mimi.
16Tako? Postadoh li vam neprijateljem propovijedajući vam istinu?
16Je, sasa nimekuwa adui yenu kwa sababu ya kuwaambieni ukweli?
17Oni revnuju za vas, ne časno, nego - odvojiti vas hoće da onda vi za njih revnujete.
17Hao watu wengine wanawahangaikia ninyi, lakini nia zao si njema. Wanataka kuwatenganisha nami ili ninyi muwahangaikie wao.
18Dobro je da se za vas revnuje u dobru uvijek, a ne samo kad sam nazočan kod vas,
18Kwa kweli ni jambo jema daima kuwahangaikia wengine katika mambo mema, na si tu wakati mimi nipo pamoja nanyi.
19dječice moja, koju ponovno u trudovima rađam dok se Krist ne oblikuje u vama.
19Watoto wangu, kama vile mama mja mzito anavyotaabika wakati wa kujifungua, mimi nataabika tena kwa ajili yenu mpaka hapo hali yake Kristo itakapoundwa ndani yenu.
20Htio bih sada biti kod vas, pa i jezik promijeniti, jer ne znam što bih s vama.
20Laiti ningekuwa pamoja nanyi sasa, maana ningalipata msimamo ufaao juu yenu! Nina wasiwasi sana nanyi!
21Recite mi vi, koji želite biti pod Zakonom, zar ne čujete Zakona?
21Niambieni, enyi mnaopenda kutawaliwa na sheria: Je, mnasikia isemavyo Sheria?
22Ta pisano je da je Abraham imao dva sina, jednoga od ropkinje i jednoga od slobodne.
22Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu kwamba Abrahamu alikuwa na watoto wawili: mmoja kwa mwanamke mtumwa, na wa pili kwa mwanamke huru.
23Ali onaj od ropkinje rođen je po tijelu, a onaj od slobodne snagom obećanja.
23Yule wa mwanamke mtumwa alizaliwa kama kawaida, lakini yule wa mwanamke huru alizaliwa kutokana na ahadi ya Mungu.
24To je slika. Doista, te žene dva su Saveza: jedan s brda Sinaja, koji rađa za ropstvo - to je Hagara.
24Mambo hayo yamekuwa mfano; mama hao wawili ni mfano wa maagano mawili; la kwanza ni lile lililofanyika mlimani Sinai, mwakilishi wake ni Hagari, na watoto wake wanazaliwa utumwani.
25Jer Hagara znači brdo Sinaj u Arabiji i odgovara sadašnjem Jeruzalemu jer robuje zajedno sa svojom djecom.
25Hagari anawakilisha mlima Sinai ulioko Arabia, na ni mfano wa Yerusalemu ya sasa, ulio mtumwa pamoja na watoto wake.
26Onaj pak Jeruzalem gore slobodan je; on je majka naša.
26Lakini Yerusalemu ya juu mbinguni ni mji ulio huru, nao ni mama yetu.
27Pisano je doista: Kliči, nerotkinjo, koja ne rađaš, podvikuj od radosti, ti što ne znaš za trudove! Jer osamljena više djece ima negoli udana.
27Maana imeandikwa: "Furahi, ewe uliye tasa usiyezaa; paaza sauti wewe usiyepata kujifungua mtoto; maana watoto wa yule aliyeachwa ni wengi zaidi kuliko wa yule aliye na mume."
28Vi ste, braćo, kao Izak, djeca obećanja.
28Sasa, basi, ndugu zangu, ninyi ni watoto wa Mungu kutokana na ahadi yake kama alivyokuwa Isaka.
29I kao što je onda onaj po tijelu rođeni progonio onoga po duhu rođenoga, tako je i sada.
29Lakini kama vile siku zile yule mtoto aliyezaliwa kwa njia ya kawaida alimdhulumu yule aliyezaliwa kwa uwezo wa Roho wa Mungu, vivyo hivyo na siku hizi.
30Nego, što veli Pismo? Otjeraj sluškinju i sina njezina jer sin sluškinje ne smije biti baštinik sa sinom slobodne.
30Lakini Maandiko Matakatifu yasemaje? Yasema: "Mfukuze mama mtumwa pamoja na mwanawe; maana mtoto wa mtumwa hatarithi pamoja na mtoto wa mama huru."
31Zato, braćo, nismo djeca ropkinje nego slobodne.
31Kwa hiyo, basi, ndugu, sisi si watoto wa mtumwa bali wa mama huru.