Croatian

Swahili: New Testament

Revelation

19

1Nakon toga začujem kao jak glas silnoga mnoštva na nebu: "Aleluja! Spasenje i slava i moć Bogu našemu!
1Baada ya hayo nikasikia kitu kama sauti kubwa ya umati wa watu wengi mbinguni ikisema, "Haleluya! Ukombozi, utukufu na nguvu ni mali yake Mungu wetu!
2Doista, istiniti su i pravedni sudovi njegovi jer osudi veliku Bludnicu, što pokvari zemlju bludom svojim, i osveti na njoj krv slugu svojih!"
2Maana hukumu yake ni ya kweli na ya haki. Amemhukumu yule mzinzi mkuu ambaye alikuwa ameipotosha dunia kwa uzinzi wake. Amemwadhibu kwa sababu ya kumwaga damu ya watumishi wake!"
3I ponove: "Aleluja! Dim njezin suklja u vijeke vjekova!"
3Wakasema, "Asifiwe Mungu! Moshi wa moto unaoteketeza mji huo utapanda juu milele na milele!"
4Nato starješine, njih dvadesetčetvorica, i ona četiri bića padoše ničice i p okloniše se Bogu, koji sjedi na prijestolju, govoreći: "Amen! Aleluja!"
4Na wale wazee ishirini na wanne, na vile viumbe hai vinne, wakajitupa chini, wakamwabudu Mungu aliyeketi juu ya kiti cha enzi wakisema, "Amina! Asifiwe Mungu!"
5I s prijestolja iziđe glas: "Hvalite Boga našega, sve sluge njegove, svi koji se njega bojite, i mali i veliki!"
5Kisha kukatokea sauti kwenye kiti cha enzi: "Msifuni Mungu enyi watumishi wake wote, nyote mnaomcha, wadogo kwa wakubwa."
6I začuh kao glas silna mnoštva i kao šum voda mnogih i kao prasak gromova silnih: "Aleluja! Zakraljeva Gospod, Bog naš Svevladar!
6Kisha nikasikia kitu kama sauti ya umati mkubwa wa watu na sauti ya maji mengi na ya ngurumo kubwa, ikisema, "Haleluya! Maana Bwana Mungu wetu Mwenye Uwezo ni Mfalme!
7Radujmo se i kličimo i slavu mu dajmo jer dođe svadba Jaganjčeva, opremila se Zaručnica njegova!
7Tufurahi na kushangilia; tumtukuze, kwani wakati wa arusi ya Mwanakondoo umefika, na bibi arusi yuko tayari.
8Dano joj je odjenuti se u lan tanan, blistav i čist!" A lan - pravedna su djela svetih.
8Amepewa uwezo wa kujivalia nguo ya kitani safi, iliyotakata na yenye kung'aa!" (Nguo hiyo ya kitani safi ni matendo mema ya watu wa Mungu.)
9I reče mi: "Piši! Blago onima koji su pozvani na svadbenu gozbu Jaganjčevu!" I reče mi: "Ove su riječi istinite, Božje."
9Kisha malaika akaniambia, "Andika haya: Heri wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwanakondoo!" Tena akaniambia, "Hayo ni maneno ya kweli ya Mungu."
10Padoh mu pred noge da mu se poklonim. A on će mi: "Nipošto! Sluga sam kao i ti i braća tvoja koja imaju svjedočanstvo Isusovo. Bogu se pokloni!" Jer svjedočanstvo Isusovo duh je proročki.
10Basi, mimi nikaanguka kifudifudi mbele ya miguu yake nikataka kumwabudu. Lakini yeye akaniambia, "Acha! Mimi ni mtumishi tu kama wewe na ndugu zako; sote tunauzingatia ukweli ule alioufunua Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ukweli alioufunua Yesu ndio unaowaangazia manabii."
11I vidjeh: nebo otvoreno - i gle, konj bijelac, a na nj sjeo On, zvani Vjerni i Istiniti, a sudi i vojuje po pravdi;
11Kisha nikaona mbingu zimefunguliwa; na huko alikuwako farasi mmoja mweupe, na mpanda farasi wake aliitwa "Mwaminifu" na "Kweli". Huyo huhukumu na kupigana kwa ajili ya haki.
12oči mu plamen ognjeni, na glavi mu mnoge krune; nosi napisano ime kojeg nitko ne zna doli on sam;
12Macho yake ni kama mwali wa moto, na alikuwa amevaa taji nyingi kichwani. Alikuwa ameandikwa jina ambalo hakuna mtu alijuaye isipokuwa tu yeye mwenyewe.
13ogrnut je ogrtačem krvlju natopljenim; ime mu: Riječ Božja.
13Alikuwa amevaa vazi lililokuwa limelowekwa katika damu. Na jina lake huyo ni "Neno la Mungu."
14Prate ga na bijelcima Vojske nebeske, odjevene u lan tanan, bijel i čist.
14Majeshi ya mbinguni yalimfuata yakiwa yamepanda farasi weupe na walikuwa wamevaa mavazi ya kitani, meupe na safi.
15Iz usta mu izlazi oštar mač kojim će posjeći narode. Vladat će njima palicom gvozdenom. On gazi u kaci gnjevne srdžbe Boga Svevladara.
15Upanga mkali hutoka kinywani mwake, na kwa upanga huo atawashinda mataifa. Yeye ndiye atakayetawala kwa fimbo ya chuma na kuikamua divai katika chombo cha kukamulia zabibu za ghadhabu kuu ya Mungu Mwenye Uwezo.
16Na ogrtač, o boku, napisano mu ime: "Kralj kraljeva i Gospodar gospodara."
16Juu ya vazi lake, na juu ya mguu wake, alikuwa ameandikwa jina: "Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana."
17I vidjeh jednog anđela: stajaše na suncu vičući iza glasa svim pticama što nebom lete: "Ovamo! Skupite se na veliku gozbu Božju
17Kisha nikamwona malaika mmoja amesimama katika jua. Akapaaza sauti na kuwaambia ndege wote waliokuwa wanaruka juu angani, "Njoni! Kusanyikeni pamoja kwa karamu kuu ya Mungu.
18da se najedete mesa kraljeva, i mesa vojvoda, i mesa mogućnika, i mesa konja i konjanika njihovih, i mesa svih mogućih ljudi, slobodnjaka i robova, malih i velikih!"
18Njoni mkaitafune miili ya wafalme, ya majemadari, ya watu wenye nguvu, ya farasi na wapanda farasi wao; njoni mkaitafune miili ya watu wote: walio huru na watumwa, wadogo na wakubwa."
19I vidjeh: Zvijer i kraljevi zemlje i vojske njihove skupiše se u boj da se zarate s Onim što sjedi na konju i s vojskom njegovom.
19Kisha nikaona yule mnyama pamoja na mfalme wa dunia na askari wao wamekusanyika pamoja kusudi wapigane na yule aliyekuwa ameketi juu ya farasi, pamoja na jeshi lake.
20I Zvijer bi uhvaćena, a s njom i Lažni prorok koji je u njenoj nazočnosti činio znamenja i njima zavodio one što su primili žig Zvijeri i klanjali se njezinu kipu. Živi su oboje bačeni u ognjeno jezero što gori sumporom.
20Lakini huyo mnyama akachukuliwa mateka, pamoja na nabii wa uongo aliyekuwa akifanya miujiza mbele yake. (Kwa miujiza hiyo, alikuwa amewapotosha wale waliokuwa na chapa ya huyo mnyama, na ambao walikuwa wameiabudu sanamu yake.) Huyo mnyama pamoja na huyo nabii walitupwa wote wawili, wakiwa wazimawazima, ndani ya ziwa linalowaka moto wa kiberiti.
21A drugi su posječeni mačem što iziđe iz usta Onoga koji sjedi na konju i sve se ptice nasitiše mesa njihova.
21Majeshi yao yaliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule anayepanda farasi. Ndege wote wakajishibisha kwa nyama zao.