1I vidjeh anđela: siđe s neba s ključima Bezdana i s velikim okovima u ruci.
1Kisha nikamwona malaika mmoja anashuka kutoka mbinguni akiwa na ufunguo wa kuzimu na mnyororo mkubwa mkononi mwake.
2Zgrabi Zmaja, Staru zmiju, to jest Ðavla, Sotonu, i okova ga za tisuću godina.
2Akalikamata lile joka--nyoka wa kale, yaani Ibilisi au Shetani--akalifunga kwa muda wa miaka elfu moja.
3Baci ga u Bezdan koji nad njim zatvori i zapečati da više ne zavodi narode dok se ne navrši tisuću godina. Nakon toga ima biti odriješen za malo vremena.
3Malaika akalitupa Kuzimu, akaufunga mlango wa kuingilia huko na kuutia mhuri ili lisiweze tena kuyapotosha mataifa mpaka hapo miaka elfu moja itakapotimia. Lakini baada ya miaka hiyo ni lazima lifunguliwe tena, lakini kwa muda mfupi tu.
4I vidjeh prijestolja - onima što sjedoše na njih dano je suditi - i duše pogubljenih zbog svjedočanstva Isusova i zbog Riječi Božje i sve koji se ne pokloniše Zvijeri ni kipu njezinu te ne primiše žiga na čela svoja ni na ruke. Oni oživješe i zakraljevaše s Kristom tisuću godina.
4Kisha nikaona viti vya enzi na watu walioketi juu yake; watu hao walipewa mamlaka ya hukumu. Niliona pia roho za wale waliokuwa wamenyongwa kwa sababu ya kumtangaza Yesu na kwa sababu ya neno la Mungu. Hawa hawakumwabudu yule mnyama na sanamu yake, wala hawakupigwa alama yake juu ya paji za nyuso zao, au juu ya mikono yao. Walipata tena uhai, wakatawala pamoja na Kristo kwa muda wa miaka elfu moja.
5Drugi mrtvi ne oživješe dok se ne navrši tisuću godina. To je ono prvo uskrsnuće.
5(Wale wengine waliokufa hawakupata uhai mpaka miaka elfu moja itimie.) Huu ndio ufufuo wa kwanza.
6Blažen i svet onaj tko je dionik toga prvog uskrsnuća! Nad njim druga smrt nema vlasti: oni će biti svećenici Božji i Kristovi i s njime će kraljevati tisuću godina.
6Wameneemeka sana, tena heri yao wote wanaoshiriki ufufuo huu wa kwanza. Kifo cha pili hakitakuwa na nguvu juu yao; watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, na watatawala pamoja naye kwa miaka elfu moja.
7A kad se navrši tisuću godina, Sotona će iz svoga zatvora biti pušten:
7Wakati miaka elfu mia moja itakapotimia, Shetani atafunguliwa kutoka gerezani mwake.
8izići će zavesti narode sa četiri kraja zemlje, Goga i Magoga, i skupiti ih u boj. Bit će ih kao pijeska morskoga.
8Basi, atatoka nje, ataanza kuyapotosha mataifa yote yaliyotawanyika kila mahali duniani, yaani Gogu na Magogu. Shetani atawakusanya pamoja kwa ajili ya vita; nao watakuwa wengi kama mchanga wa pwani.
9Skupiše se na prostrano polje zemlje i opkoliše tabor svetih i ljubljeni grad. Ali oganj siđe s neba te ih proguta.
9Walitawanyika katika nchi yote, wakaizunguka kambi ya watu wa Mungu na mji wa Mungu aupendao. Lakini moto ulishuka kutoka mbinguni, ukawaangamiza.
10A njihov zavodnik, Ðavao, bačen bi u jezero ognjeno i sumporno, gdje se nalaze i Zvijer i Lažni prorok: ondje će se mučiti danju i noću u vijeke vjekova.
10Ibilisi, aliyekuwa anawapotosha, akatupwa ndani ya ziwa linalowaka moto wa kiberiti, walimo yule mnyama na yule nabii wa uongo, nao watateswa mchana na usiku, milele na milele.
11I vidjeh veliko bijelo prijestolje i Onoga što sjede na nj: pred licem njegovim pobježe zemlja i nebo; ni mjesta im se više ne nađe.
11Kisha nikaona kiti cha enzi kikubwa cheupe, na yule aketiye juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele ya macho yake, na havikuonekana tena.
12I vidjeh mrtve, velike i male: stoje pred prijestoljem, a knjige se otvoriše. I otvori se jedna druga knjiga, knjiga života. I mrtvi bijahu suđeni po onome što stoji napisano u knjigama, po djelima svojim.
12Kisha nikawaona watu wakubwa na wadogo, wamesimama mbele ya kiti cha enzi, na vitabu vikafunguliwa. Halafu kitabu kingine, yaani kitabu cha uzima, kikafunguliwa pia. Wafu wakahukumiwa kadiri ya matendo yao, kama ilivyoandikwa ndani ya vitabu hivyo.
13More predade svoje mrtvace, a Smrt i Podzemlje svoje: i svaki bi suđen po djelima svojim.
13Bahari ikawatoa nje wafu waliokuwa ndani yake; kifo na kuzimu vikawatoa nje wafu waliokuwa ndani yao. Kila mmoja akahukumiwa kufuatana na matendo yake.
14A Smrt i Podzemlje bili su bačeni u jezero ognjeno. Jezero ognjeno - to je druga smrt:
14Kisha kifo na kuzimu vikatupwa ndani ya ziwa la moto. Ziwa hili la moto ndicho kifo cha pili.
15tko se god ne nađe zapisan u knjizi života, bio je bačen u jezero ognjeno.
15Mtu yeyote ambaye jina lake halikupatikana limeandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika ziwa la moto.