Croatian

Swahili: New Testament

Revelation

2

1Anđelu Crkve u Efezu napiši: "Ovo govori Onaj koji drži sedam zvijezda u desnici, Onaj koji stupa posred sedam zlatnih svijećnjaka:
1"Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye ashikaye nyota saba katika mkono wake wa kulia, na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu.
2Znam tvoja djela, tvoj trud i postojanost tvoju i da ne možeš podnijeti opakih. Iskušao si one koji se prave apostolima, a nisu, i otkrio si da su lažljivci.
2Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo.
3Postojan si, podnio si za ime moje i nisi smalaksao.
3Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.
4Ali imam protiv tebe: prvu si ljubav svoju ostavio.
4Lakini ninayo hoja moja juu yako: wewe hunipendi tena sasa kama pale awali.
5Spomeni se dakle odakle si pao, obrati se i čini prva djela. Inače dolazim k tebi i - uklonit ću tvoj svijećnjak s mjesta njegova ako se ne obratiš.
5Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukayaache madhambi yako, na kufanya kama ulivyofanya pale awali. La sivyo, naja kwako na kukiondoa kinara chako mahali pake.
6Ali ovo imaš: mrziš nikolaitska djela koja i ja mrzim."
6Lakini nakusifu juu ya kitu kimoja: wewe unayachukia wanayoyatenda Wanikolai kama ninavyoyachukia mimi.
7"Tko ima uho, nek posluša što Duh govori crkvama! Pobjedniku ću dati jesti od stabla života koje je u raju Božjem."
7"Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! "Wale wanaoshinda nitawapa haki ya kula matunda ya mti wa uzima ulioko ndani ya bustani ya Mungu.
8I anđelu Crkve u Smirni napiši: "Ovo govori Prvi i Posljednji, Onaj koji bijaše mrtav i oživje:
8"Kwa malaika wa kanisa la Smurna andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye wa kwanza na wa mwisho, ambaye alikufa na akaishi tena.
9Znam tvoju nevolju i siromaštvo - ali ti si bogat! - i pogrde od onih koji se nazivaju Židovima, a nisu, nego su sinagoga Sotonina.
9Najua taabu zako; najua pia umaskini wako, ingawaje kwa kweli wewe ni tajiri; najua kashfa walizokufanyia wale wanaojiita Wayahudi lakini si Wayahudi wa kweli, bali ni kundi lake Shetani.
10Ne boj se onoga što ti je trpjeti! Evo, Sotona, će neke od vas baciti u tamnicu da budete iskušani. Bit ćete u nevolji deset dana. Budi vjeran do smrti i dat ću ti vijenac života."
10Usiogope hata kidogo yale ambayo itakulazimu kuteseka. Sikiliza! Ibilisi anataka kuwajaribu kwa kuwatia baadhi yenu gerezani; nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Muwe waaminifu hata mpaka kufa, nami nitawapeni taji ya uzima.
11"Tko ima uho, nek posluša što Duh govori crkvama! Pobjedniku neće nauditi druga smrt."
11"Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! "Wale wanaoshinda hawataumizwa na kifo cha pili.
12I anđelu Crkve u Pergamu napiši: "Ovo govori Onaj u koga je mač dvosjek, oštar:
12"Kwa malaika wa kanisa la Pergamoni andika hivi: "Huu ndio ujumbe wake yeye aliye na upanga mkali wenye kuwili.
13Znam gdje prebivaš - ondje gdje je Sotonino prijestolje - a čvrsto se držiš moga imena te nisi zanijekao moje vjere ni u one dane kad je Antipa, moj svjedok, vjerni moj, ubijen kod vas - gdje Sotona prebiva.
13Najua unakoishi: Wewe unaishi kwenye makao makuu ya Shetani! Lakini bado unashikilia jina langu; hukuikana imani yako kwangu hata siku zile Antipa shahidi wangu mwaminifu, alipouawa pale mahali anapoishi Shetani.
14Ali imam nešto malo protiv tebe: imaš ondje nekih što drže nauk Bileama što pouči Balaka da stupicu stavi sinovima Izraelovim te blaguju od mesa žrtvovana idolima i bludu se podadu.
14Lakini ninayo machache dhidi yako: baadhi yenu ni wafuasi wa Balaamu aliyemfundisha Balaki kuwatega wana wa Israeli wale vyakula vilivyotambikiwa sanamu za kufanya uzinzi.
15Tako i ti imaš takvih koji drže nauk nikolaitski.
15Vivyo hivyo, wako pia miongoni mwenu watu wanaofuata mafundisho ya Wanikolai.
16Obrati se dakle! Inače dolazim ubrzo k tebi da ratujem s njima mačem usta svojih."
16Basi, achana na madhambi yako. La sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga utokao kinywani mwangu.
17"Tko ima uho, nek posluša što Duh govori crkvama! Pobjedniku ću dati mane sakrivene i bijel ću mu kamen dati, a na kamenu napisano ime novo koje nitko ne zna doli onaj koji ga prima."
17"Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! "Wale wanaoshinda nitawapa ile mana iliyofichika. Nitawapa pia jiwe jeupe lililoandikwa jina jipya ambalo hakuna mtu aliyelijua isipokuwa tu wale wanaolipokea.
18I anđelu Crkve u Tijatiri napiši: "Ovo govori Sin Božji, Onaj u koga su oči kao plamen ognjeni, a noge mu nalik na mjed uglađenu:
18"Kwa malaika wa kanisa la Thuatira andika hivi: "Huu ndio ujumbe wa Mwana wa Mungu, ambaye macho yake yametameta kama moto, na miguu yake inang'aa kama shaba iliyosuguliwa.
19Znam tvoja djela: tvoju ljubav, i vjeru, i služenje, i postojanost - i tvoja posljednja djela obilatija od prvašnjih.
19Najua mambo yako yote. Najua upendo wako, imani yako, utumishi wako na uvumilivu wako. Wewe unafanya vizuri zaidi sasa kuliko pale awali.
20Ali imam protiv tebe: puštaš ženu Jezabelu, koja se pravi proročicom, da uči i zavodi moje sluge te se bludu podaju i blaguju od mesa žrtvovana idolima.
20Lakini nina hoja moja juu yako: wewe unamvumilia yule mwanamke Yezabeli anayejiita nabii wa Mungu. Yeye huwafundisha na kuwapotosha watumishi wangu wafanye uzinzi na kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu.
21Dadoh joj vremena za obraćenje, ali ona neće da se obrati od bludnosti svoje.
21Nimempa muda wa kutubu dhambi zake, lakini hataki kuachana na uzinzi wake.
22Evo, bacam je na postelju, a bludne drugare njene u veliku nevolju ako se ne odvrate od njezinih djela;
22Sikiliza! Sasa namtupa kitandani ambapo yeye pamoja na wote waliofanya uzinzi naye watapatwa na mateso makali. Naam, nitafanya hivyo, kama wasipotubu matendo yao mabaya waliyotenda naye.
23i djecu ću joj smrću pobiti. I znat će sve crkve: Ja sam Onaj koji istražuje bubrege i srca - i dat ću vam svakomu po djelima.
23Tena nitawaua wafuasi wake, ili makanisa yote yatambue kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo na fikira za watu.
24Vama pak velim - vama drugim u Tijatiri koji ne drže ovog nauka te ne upoznaše takozvanih dubina sotonskih: Ne stavljam na vas drugoga bremena
24"Lakini ninyi wengine mlioko huko Thuatira ambao hamfuati mafundisho yake Yezabeli, na ambao hamkujifunza kile wanachokiita Siri ya Shetani, nawaambieni kwamba sitawapeni mzigo mwingine.
25nego - što imate, čvrsto držite dok ne dođem."
25Lazima mzingatie yale mliyo nayo sasa mpaka nitakapokuja.
26"Pobjedniku, onomu što do kraja bude vršio moja djela, dat ću vlast nad narodima
26"Wanaoshinda, na wale watakaozingatia mpaka mwisho kutenda ninayotaka, nitawapa mamlaka juu ya mataifa.
27i vladat će njima palicom gvozdenom, kao posuđe glineno satirati ih -
27Naam, nitawapa uwezo uleule nilioupokea kwa Baba: yaani, watayatawala mataifa kwa fimbo ya chuma na kuyavunjavunja kama chombo cha udongo.
28kao što i ja to primih od Oca svoga. I dat ću mu zvijezdu Danicu.
28Tena nitawapa nyota ya asubuhi.
29Tko ima uho, nek posluša što Duh govori crkvama!"
29"Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!