1I anđelu Crkve u Sardu napiši: "Ovo govori Onaj koji ima sedam duhova Božjih i sedam zvijezda: Znam tvoja djela: imaš ime da živiš, a mrtav si.
1"Kwa malaika wa kanisa la Sarde andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aliye na roho saba za Mungu na nyota saba. Nayajua mambo yako yote; najua unajulikana kuwa na uhai kumbe umekufa!
2Budan budi i utvrdi ostatak koji tek što ne umre. Doista, ne nađoh da su ti djela pred Bogom mojim savršena.
2Amka! Imarisha chochote chema kilichokubakia kabla nacho hakijatoweka kabisa. Maana, mpaka sasa, sijayaona matendo yako kuwa ni makamilifu mbele ya Mungu wangu.
3Spomeni se dakle: kako si primio Riječ i poslušao, tako je i čuvaj - i obrati se. Ne budeš li dakle budan, doći ću kao tat, a nećeš znati u koji ću čas doći na te.
3Kumbuka, basi, yale uliyofundishwa na jinsi ulivyoyasikia, uyatii na ubadili nia yako mbaya. Usipokesha nitakujia ghafla kama mwizi, na wala hutaijua saa nitakapokujia.
4Ali imaš u Sardu nekolicinu imena što ne okaljaše svojih haljina; oni će hoditi sa mnom u bjelini jer su dostojni."
4Lakini wako wachache huko Sarde ambao hawakuyachafua mavazi yao. Hao wanastahili kutembea pamoja nami wakiwa wamevaa mavazi meupe.
5"Tako će pobjednik biti odjeven u bijele haljine i neću izbrisati imena njegova iz knjige života i priznat ću ime njegovo pred Ocem svojim i anđelima njegovim."
5"Wale wanaoshinda, watavikwa mavazi meupe kama hao. Nami sitayafuta majina yao kutoka katika kitabu cha uzima; tena nitawakiri kwamba ni wangu mbele ya Baba yangu na mbele ya malaika wake.
6"Tko ima uho, nek posluša što Duh govori crkvama!"
6"Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
7I anđelu Crkve u Filadelfiji napiši: "Ovo govori Sveti, Istiniti, Onaj koji ima ključ Davidov i kad otvori, nitko neće zatvoriti; kad zatvori, nitko neće otvoriti:
7"Kwa malaika wa kanisa la Filadelfia andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aliye mtakatifu na wa kweli, ambaye anao ule ufunguo wa Daudi, na ambaye hufungua na hakuna mtu awezaye kufungua.
8Znam tvoja djela. Evo, otvorio sam pred tobom vrata kojih nitko zatvoriti ne može. Doista, malena je tvoja snaga, a očuvao si moju riječ i nisi zatajio mog imena.
8Nayajua mambo yako yote! Sasa, nimefungua mbele yako mlango ambao hakuna mtu awezaye kuufunga; najua kwamba ingawa huna nguvu sana, hata hivyo, umezishika amri zangu, umelitii neno langu wala hukulikana jina langu.
9Evo, dovest ću neke iz sinagoge Sotonine - koji sebe zovu Židovi, a nisu, nego lažu - evo, prisilit ću ih da dođu da ti se do nogu poklone te upoznaju da te ja ljubim.
9Sikiliza! Nitawapeleka kwako watu wa kundi lake Shetani, watu ambao hujisema kuwa ni Wayahudi, kumbe ni wadanganyifu. Naam, nitawapeleka kwako na kuwafanya wapige magoti mbele yako wapate kujua kwamba kweli nakupenda wewe.
10Budući da si očuvao moju riječ o postojanosti, i ja ću očuvati tebe od časa kušnje koji ima doći na sav svijet da se iskušaju svi pozemljari.
10Kwa kuwa wewe umezingatia agizo langu la kuwa na uvumilivu, nami pia nitakutegemeza salama wakati ule wa dhiki inayoujia ulimwengu mzima kuwajaribu wote wanaoishi duniani.
11Dolazim ubrzo. Čvrsto drži što imaš da ti nitko ne ugrabi vijenca."
11Naja kwako upesi! Linda, basi, ulicho nacho sasa, ili usije ukanyang'anywa na mtu yeyote taji yako ya ushindi.
12"Pobjednika ću postaviti stupom u hramu Boga moga i odande on više neće izići i napisat ću na njemu ime Boga svoga i ime grada Boga svoga, novog Jeruzalema koji siđe s neba od Boga mojega, i ime moje novo."
12"Wale wanaoshinda nitawafanya wawe minara katika Hekalu la Mungu wangu, na hawatatoka humo kamwe. Pia nitaandika juu yao jina la Mungu wangu na jina la mji wa Mungu wangu, yaani Yerusalemu mpya, mji ambao utashuka kutoka juu mbinguni kwa Mungu wangu. Tena nitaandika juu yao jina langu jipya.
13"Tko ima uho, nek posluša što Duh govori crkvama!"
13"Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
14I anđelu Crkve u Laodiceji napiši: "Ovo govori Amen, Svjedok vjerni i istiniti, Početak Božjeg stvorenja:
14"Kwa malaika wa kanisa la Laodikea andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aitwaye Amina. Yeye ni shahidi mwaminifu na wa kweli, ambaye ni chanzo cha viumbe vyote alivyoumba Mungu.
15Znam tvoja djela: nisi ni studen ni vruć. O da si studen ili vruć!
15Nayajua mambo yako yote! Najua kwamba wewe si baridi wala si moto. Afadhali ungekuwa kimojawapo: baridi au moto.
16Ali jer si mlak, ni vruć ni studen, povratit ću te iz usta.
16Basi, kwa kuwa hali yako ni vuguvugu, si baridi wala si moto, nitakutapika!
17Govoriš: 'Bogat sam, obogatih se, ništa mi ne treba!' A ne znaš da si nevolja i bijeda, i ubog, i slijep, i gol.
17Wewe unajisema, Mimi ni tajiri; ninajitosheleza, sina haja ya kitu chochote. Kumbe, hujui kwamba wewe ni mnyonge, unahitaji kuhurumiwa, maskini, kipofu tena uko uchi!
18Savjetujem ti: kupi od mene zlata u vatri žežena da se obogatiš i bijele haljine da se odjeneš da se ne vidi tvoja sramotna golotinja; i pomasti da oči pomažeš i vidiš.
18Nakushauri ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto upate kuwa tajiri kweli. Tena afadhali ununue pia vazi jeupe, uvae na kufunika aibu ya uchi wako. Nunua pia mafuta ukapake machoni pako upate kuona.
19Ja korim i odgajam one koje ljubim. Revan budi i obrati se!
19Mimi ndiye mwenye kumwonya na kumrudi yeyote ninayempenda. Kwa hiyo kaza moyo, achana na dhambi zako.
20Evo, na vratima stojim i kucam; posluša li tko glas moj i otvori mi vrata, unići ću k njemu i večerati s njim i on sa mnom."
20Sikiliza! Mimi nasimama mlangoni na kubisha hodi. Mtu akisikia sauti yangu na kufungua mlango, nitaingia nyumbani kwake na kula chakula pamoja naye, naye atakula pamoja nami.
21"Pobjednika ću posjesti sa sobom na prijestolje svoje, kao što i ja, pobijedivši, sjedoh s Ocem svojim na prijestolje njegovo."
21"Wale wanaoshinda nitawaketisha pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi mwenyewe nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
22"Tko ima uho, nek posluša što Duh govori crkvama!"
22"Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!"