Darby's Translation

Swahili: New Testament

1 Corinthians

10

1For I would not have you ignorant, brethren, that all our fathers were under the cloud, and all passed through the sea;
1Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
2and all were baptised unto Moses in the cloud and in the sea;
2Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
3and all ate the same spiritual food,
3Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
4and all drank the same spiritual drink, for they drank of a spiritual rock which followed [them]: (now the rock was the Christ;)
4wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
5yet God was not pleased with the most of them, for they were strewed in the desert.
5Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
6But these things happened [as] types of us, that we should not be lusters after evil things, as they also lusted.
6Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
7Neither be ye idolaters, as some of them; as it is written, The people sat down to eat and to drink, and rose up to play.
7Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: "Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza."
8Neither let us commit fornication, as some of them committed fornication, and fell in one day three and twenty thousand.
8Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
9Neither let us tempt the Christ, as some of them tempted, and perished by serpents.
9Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
10Neither murmur ye, as some of them murmured, and perished by the destroyer.
10Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
11Now all these things happened to them [as] types, and have been written for our admonition, upon whom the ends of the ages are come.
11Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili.
12So that let him that thinks that he stands take heed lest he fall.
12Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
13No temptation has taken you but such as is according to man's nature; and God is faithful, who will not suffer you to be tempted above what ye are able [to bear], but will with the temptation make the issue also, so that [ye] should be able to bear [it].
13Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
14Wherefore, my beloved, flee from idolatry.
14Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
15I speak as to intelligent [persons]: do *ye* judge what I say.
15Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
16The cup of blessing which we bless, is it not [the] communion of the blood of the Christ? The bread which we break, is it not [the] communion of the body of the Christ?
16Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
17Because we, [being] many, are one loaf, one body; for we all partake of that one loaf.
17Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
18See Israel according to flesh: are not they who eat the sacrifices in communion with the altar?
18Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
19What then do I say? that what is sacrificed to an idol is anything, or that an idol is anything?
19Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
20But that what [the nations] sacrifice they sacrifice to demons, and not to God. Now I do not wish you to be in communion with demons.
20Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
21Ye cannot drink [the] Lord's cup, and [the] cup of demons: ye cannot partake of [the] Lord's table, and of [the] table of demons.
21Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
22Do we provoke the Lord to jealousy? are we stronger than he?
22Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
23All things are lawful, but all are not profitable; all things are lawful, but all do not edify.
23Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
24Let no one seek his own [advantage], but that of the other.
24Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
25Everything sold in the shambles eat, making no inquiry for conscience sake.
25Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
26For the earth [is] the Lord's and its fulness.
26maana Maandiko yasema: "Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana."
27But if any one of the unbelievers invite you, and ye are minded to go, all that is set before you eat, making no inquiry for conscience sake.
27Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
28But if any one say to you, This is offered to holy purposes, do not eat, for his sake that pointed it out, and conscience sake;
28Lakini mtu akiwaambieni: "Chakula hiki kimetambikiwa sanamu," basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
29but conscience, I mean, not thine own, but that of the other: for why is my liberty judged by another conscience?
29Nasema, "kwa ajili ya dhamiri," si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: "Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
30If *I* partake with thanksgiving, why am I spoken evil of for what *I* give thanks for?
30Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?"
31Whether therefore ye eat, or drink, or whatever ye do, do all things to God's glory.
31Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
32Give no occasion to stumbling, whether to Jews, or Greeks, or the assembly of God.
32Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
33Even as *I* also please all in all things; not seeking my own profit, but that of the many, that they may be saved.
33Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.