Darby's Translation

Swahili: New Testament

Colossians

2

1For I would have you know what combat I have for you, and those in Laodicea, and as many as have not seen my face in flesh;
1Napenda mjue jinsi ninavyofanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa ajili ya watu wa Laodikea na kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona kwa macho.
2to the end that their hearts may be encouraged, being united together in love, and unto all riches of the full assurance of understanding, to [the] full knowledge of the mystery of God;
2Nafanya hivi kusudi mioyo yao ifarijiwe na kuvutwa pamoja katika upendo, ili wajazwe uthabiti mwingi uletwao na elimu ya kweli. Hapo wataijua siri ya Mungu ambayo ni Kristo mwenyewe.
3in which are hid all the treasures of wisdom and of knowledge.
3Ndani yake zimefichika hazina zote za hekima na elimu.
4And I say this to the end that no one may delude you by persuasive speech.
4Basi, nawaambieni, msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa maneno ya uongo hata kama ni ya kuvutia sana.
5For if indeed in the flesh I am absent, yet I am with you in spirit, rejoicing and seeing your order, and the firmness of your faith in Christ.
5Maana, ingawa mimi niko mbali nanyi kwa mwili, lakini niko pamoja nanyi kwa roho, na ninafurahi kuona uthabiti kamili mnaosimama nao pamoja katika imani yenu kwa Kristo.
6As therefore ye have received the Christ, Jesus the Lord, walk in him,
6Maadamu ninyi mmemkubali Kristo Yesu kuwa Bwana, basi, ishini katika muungano naye.
7rooted and built up in him, and assured in the faith, even as ye have been taught, abounding in it with thanksgiving.
7Mnapaswa kuwa na mizizi ndani yake, kujijenga juu yake na kuwa imara katika imani yenu kama mlivyofundishwa. Muwe na shukrani tele.
8See that there be no one who shall lead *you* away as a prey through philosophy and vain deceit, according to the teaching of men, according to the elements of the world, and not according to Christ.
8Angalieni basi, mtu asiwapotoshe kwa udanganyifu mtupu wa hekima ya kibinadamu, ambayo chanzo chake ni mafundisho ya mapokeo ya watu na ya pepo watawala, na wala si Kristo mwenyewe!
9For in him dwells all the fulness of the Godhead bodily;
9Maana, ndani yake Kristo katika ubinadamu wake, umo ukamilifu wote wa Mungu,
10and ye are complete in him, who is the head of all principality and authority,
10nanyi mmepewa uzima kamili katika kuungana naye. Yeye yuko juu ya pepo watawala wote na wakuu wote.
11in whom also ye have been circumcised with circumcision not done by hand, in the putting off of the body of the flesh, in the circumcision of the Christ;
11Katika kuungana na Kristo ninyi mlitahiriwa, lakini si kwa tohara ifanywayo na watu, bali inayofanywa na Kristo mwenyewe, na ambayo inahusikana na kukombolewa kutoka katika utu wa dhambi.
12buried with him in baptism, in which ye have been also raised with [him] through faith of the working of God who raised him from among the dead.
12Maana, mlipobatizwa mlizikwa pamoja na Kristo, na katika ubatizo, mlifufuliwa pia pamoja naye kwa imani yenu katika nguvu ya Mungu ambaye alimfufua Kristo kutoka wafu.
13And you, being dead in offences and in the uncircumcision of your flesh, he has quickened together with him, having forgiven us all the offences;
13Wakati mmoja nanyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kwa sababu ninyi mlikuwa watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amewapa ninyi uzima pamoja na Kristo. Mungu ametusamehe dhambi zetu zote;
14having effaced the handwriting in ordinances which [stood out] against us, which was contrary to us, he has taken it also out of the way, having nailed it to the cross;
14alifutilia mbali ile hati ya deni iliyokuwa inatukabili na masharti yake, na kuifuta kabisa kwa kuipigilia msalabani.
15having spoiled principalities and authorities, he made a show of them publicly, leading them in triumph by it.
15Juu ya msalaba Kristo aliwapokonya nguvu zao hao pepo watawala na wakuu; aliwafanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuwaburuta kama mateka katika msafara wa ushindi wake.
16Let none therefore judge you in meat or in drink, or in matter of feast, or new moon, or sabbaths,
16Kwa hiyo, basi, msikubali kupewa masharti na mtu yeyote kuhusu vyakula au vinywaji, siku za sherehe, sikukuu ya Mwezi mpya au Sabato.
17which are a shadow of things to come; but the body [is] of Christ.
17Mambo ya aina hiyo ni kivuli tu cha yale yatakayokuja; ukweli wenyewe ndiye Kristo.
18Let no one fraudulently deprive you of your prize, doing his own will in humility and worship of angels, entering into things which he has not seen, vainly puffed up by the mind of his flesh,
18Msikubali kuhukumiwa na mtu yeyote anayejitakia kuwa wa maana kwa sababu ya maono ya pekee na ambaye anasisitiza juu ya unyenyekevu wa uongo na ibada kwa malaika. Mtu wa namna hiyo amepumbazika kwa fikira danganifu za kidunia
19and not holding fast the head, from whom all the body, ministered to and united together by the joints and bands, increases with the increase of God.
19na amejitenga na Kristo aliye kichwa cha huo mwili. Chini ya uongozi wa Kristo, mwili wote unalishwa na kuunganishwa pamoja kwa viungo na mishipa yake, nao hukua kama atakavyo Mungu.
20If ye have died with Christ from the elements of the world, why as [if] alive in [the] world do ye subject yourselves to ordinances?
20Ninyi mmekufa pamoja na Kristo na kukombolewa kutoka nguvu za pepo watawala wa ulimwengu. Kwa nini, basi, kuishi tena kama vile mngekuwa wa ulimwengu huu? Ya nini kuwekewa masharti:
21Do not handle, do not taste, do not touch,
21"Msishike hiki," "Msionje kile," "Msiguse kile!"
22(things which are all for destruction in the using [of them]:) according to the injunctions and teachings of men,
22Mambo hayo yote yanahusika na vitu vyenye kuharibika mara tu vinapotumiwa; hayo ni maagizo na mafundisho ya kibinadamu tu.
23(which have indeed an appearance of wisdom in voluntary worship, and humility, and harsh treatment of the body, not in a certain honour,) to [the] satisfaction of the flesh.
23Kweli, masharti hayo yaonekana kuwa ya hekima katika namna ya ibada ya kujitakia wenyewe, unyenyekevu wa uongo na kuutendea mwili kwa ukali; lakini kwa kweli, haifai chochote kuzuia tamaa za mwili.