1If therefore ye have been raised with the Christ, seek the things [which are] above, where the Christ is, sitting at [the] right hand of God:
1Basi, ikiwa mmefufuka pamoja na Kristo, panieni mambo ya juu, kule Kristo aliko, ameketi upande wa kulia wa Mungu.
2have your mind on the things [that are] above, not on the things [that are] on the earth;
2Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani.
3for ye have died, and your life is hid with the Christ in God.
3Maana ninyi mmekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
4When the Christ is manifested who [is] our life, then shall *ye* also be manifested with him in glory.
4Uzima wenu halisi ni Kristo, na wakati atakapotokea ndipo nanyi pia mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
5Put to death therefore your members which [are] upon the earth, fornication, uncleanness, vile passions, evil lust, and unbridled desire, which is idolatry.
5Basi, komesheni kabisa kila kitu kilicho ndani yenu ambacho chahusika na mambo ya kidunia: uasherati, uchafu, shauku, tamaa mbaya na uchu (ambao ni sawa na kuabudu sanamu).
6On account of which things the wrath of God comes upon the sons of disobedience.
6Kwa sababu ya mambo hayo hasira ya Mungu huwajia wote wanaomwasi.
7In which *ye* also once walked when ye lived in these things.
7Wakati mmoja ninyi pia mliishi kufuatana na mambo hayo, mlipotawaliwa nayo.
8But now, put off, *ye* also, all [these] things, wrath, anger, malice, blasphemy, vile language out of your mouth.
8Lakini sasa mnapaswa kuachana na mambo haya yote: hasira, tamaa, uovu; kufuru au maneno yasiyofaa yasitoke kamwe vinywani mwenu.
9Do not lie to one another, having put off the old man with his deeds,
9Msiambiane uongo, kwani ninyi mmekwisha vua ule utu wa kale pamoja na matendo yake yote,
10and having put on the new, renewed into full knowledge according to [the] image of him that has created him;
10mkavaa utu mpya. Huu unaendelea kurekebishwa na Mungu, Muumba wake, kadiri ya mfano wake, ili mpate kumjua Mungu kwa ukamilifu.
11wherein there is not Greek and Jew, circumcision and uncircumcision, barbarian, Scythian, bondman, freeman; but Christ [is] everything, and in all.
11Katika hali hii, hakuna tena tofauti kati ya Mgiriki na Myahudi, aliyetahiriwa na asiyetahiriwa, msomi na asiye msomi, mtumwa na mtu aliye huru. Kristo ni kila kitu, na yumo katika yote.
12Put on therefore, as [the] elect of God, holy and beloved, bowels of compassion, kindness, lowliness, meekness, longsuffering;
12Ninyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
13forbearing one another, and forgiving one another, if any should have a complaint against any; even as the Christ has forgiven you, so also [do] *ye*.
13Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe ninyi.
14And to all these [add] love, which is the bond of perfectness.
14Zaidi ya hayo yote, zingatieni upendo kwani upendo huunganisha kila kitu katika umoja ulio kamili.
15And let the peace of Christ preside in your hearts, to which also ye have been called in one body, and be thankful.
15Nayo amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu; maana kwa ajili hiyo ninyi mmeitwa katika mwili huo mmoja. Tena muwe na shukrani!
16Let the word of the Christ dwell in you richly, in all wisdom teaching and admonishing one another, in psalms, hymns, spiritual songs, singing with grace in your hearts to God.
16Ujumbe wa Kristo ukae ndani yenu pamoja na utajiri wake wote. Fundishaneni na kushauriana kwa hekima yote. Imbeni zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Mungu mioyoni mwenu kwa shukrani.
17And everything, whatever ye may do in word or in deed, [do] all things in [the] name of [the] Lord Jesus, giving thanks to God the Father by him.
17Na, kila mfanyacho kwa neno au tendo, fanyeni vyote kwa jina la Bwana Yesu na kumshukuru Mungu Baba kwa njia yake.
18Wives, be subject to [your] husbands, as is fitting in [the] Lord.
18Enyi akina mama, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana.
19Husbands, love your wives, and be not bitter against them.
19Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao.
20Children, obey your parents in all things, for this is well-pleasing in [the] Lord.
20Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.
21Fathers, do not vex your children, to the end that they be not disheartened.
21Nanyi wazazi, msiwachukize watoto wenu, la sivyo watakata tamaa.
22Bondmen, obey in all things your masters according to flesh; not with eye-services, as men-pleasers, but in simplicity of heart, fearing the Lord.
22Enyi watumwa, watiini wakuu wenu wa kidunia katika mambo yote, na si tu wakati wanapowatazama kwa kuwa mnataka kujipendekeza kwao; ila fanyeni hivyo kwa moyo wote, kwa sababu ya kumcha Bwana.
23Whatsoever ye do, labour at it heartily, as [doing it] to the Lord, and not to men;
23Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wote, kwa sababu ya Bwana na si kwa ajili ya mtu.
24knowing that of [the] Lord ye shall receive the recompense of the inheritance; ye serve the Lord Christ.
24Kumbukeni kwamba atawapeni tuzo lile alilowawekea watu wake. Mtumikieni Kristo Bwana!
25For he that does a wrong shall receive the wrong he has done, and there is no respect of persons.
25Atendaye mabaya atalipwa kufuatana na ubaya wake; Mungu hana ubaguzi.