Darby's Translation

Swahili: New Testament

Ephesians

5

1Be ye therefore imitators of God, as beloved children,
1Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.
2and walk in love, even as the Christ loved us, and delivered himself up for us, an offering and sacrifice to God for a sweet-smelling savour.
2Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.
3But fornication and all uncleanness or unbridled lust, let it not be even named among you, as it becomes saints;
3Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.
4and filthiness and foolish talking, or jesting, which are not convenient; but rather thanksgiving.
4Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.
5For this ye are [well] informed of, knowing that no fornicator, or unclean person, or person of unbridled lust, who is an idolater, has inheritance in the kingdom of the Christ and God.
5Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.
6Let no one deceive you with vain words, for on account of these things the wrath of God comes upon the sons of disobedience.
6Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.
7Be not ye therefore fellow-partakers with them;
7Basi, msishirikiane nao.
8for ye were once darkness, but now light in [the] Lord; walk as children of light,
8Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:
9(for the fruit of the light [is] in all goodness and righteousness and truth,)
9maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.
10proving what is agreeable to the Lord;
10Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.
11and do not have fellowship with the unfruitful works of darkness, but rather also reprove [them],
11Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.
12for the things that are done by them in secret it is shameful even to say.
12Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.
13But all things having their true character exposed by the light are made manifest; for that which makes everything manifest is light.
13Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;
14Wherefore he says, Wake up, [thou] that sleepest, and arise up from among the dead, and the Christ shall shine upon thee.
14na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: "Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza."
15See therefore how ye walk carefully, not as unwise but as wise,
15Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.
16redeeming the time, because the days are evil.
16Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.
17For this reason be not foolish, but understanding what [is] the will of the Lord.
17Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.
18And be not drunk with wine, in which is debauchery; but be filled with the Spirit,
18Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.
19speaking to yourselves in psalms and hymns and spiritual songs, singing and chanting with your heart to the Lord;
19Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
20giving thanks at all times for all things to him [who is] God and [the] Father in the name of our Lord Jesus Christ,
20Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
21submitting yourselves to one another in [the] fear of Christ.
21Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.
22Wives, [submit yourselves] to your own husbands, as to the Lord,
22Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.
23for a husband is head of the wife, as also the Christ [is] head of the assembly. *He* [is] Saviour of the body.
23Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.
24But even as the assembly is subjected to the Christ, so also wives to their own husbands in everything.
24Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.
25Husbands, love your own wives, even as the Christ also loved the assembly, and has delivered himself up for it,
25Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.
26in order that he might sanctify it, purifying [it] by the washing of water by [the] word,
26Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,
27that *he* might present the assembly to himself glorious, having no spot, or wrinkle, or any of such things; but that it might be holy and blameless.
27kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.
28So ought men also to love their own wives as their own bodies: he that loves his own wife loves himself.
28Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.
29For no one has ever hated his own flesh, but nourishes and cherishes it, even as also the Christ the assembly:
29(Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,
30for we are members of his body; [we are of his flesh, and of his bones.]
30maana sisi ni viungo vya mwili wake.)
31Because of this a man shall leave his father and mother, and shall be united to his wife, and the two shall be one flesh.
31Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja."
32This mystery is great, but *I* speak as to Christ, and as to the assembly.
32Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.
33But *ye* also, every one of you, let each so love his own wife as himself; but as to the wife [I speak] that she may fear the husband.
33Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.