1Children, obey your parents in [the] Lord, for this is just.
1Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
2Honour thy father and thy mother, which is the first commandment with a promise,
2"Waheshimu Baba na mama yako," hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
3that it may be well with thee, and that thou mayest be long-lived on the earth.
3"Upate fanaka na miaka mingi duniani."
4And [ye] fathers, do not provoke your children to anger, but bring them up in [the] discipline and admonition of [the] Lord.
4Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
5Bondmen, obey masters according to flesh, with fear and trembling, in simplicity of your heart as to the Christ;
5Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
6not with eye-service as men-pleasers; but as bondmen of Christ, doing the will of God from [the] soul,
6Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
7serving with good will as to the Lord, and not to men;
7Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
8knowing that whatever good each shall do, this he shall receive of [the] Lord, whether bond or free.
8Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
9And, masters, do the same things towards them, giving up threatening, knowing that both their and your Master is in heaven, and there is no acceptance of persons with him.
9Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
10For the rest, brethren, be strong in [the] Lord, and in the might of his strength.
10Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
11Put on the panoply of God, that ye may be able to stand against the artifices of the devil:
11Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
12because our struggle is not against blood and flesh, but against principalities, against authorities, against the universal lords of this darkness, against spiritual [power] of wickedness in the heavenlies.
12Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza.
13For this reason take [to you] the panoply of God, that ye may be able to withstand in the evil day, and, having accomplished all things, to stand.
13Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
14Stand therefore, having girt about your loins with truth, and having put on the breastplate of righteousness,
14Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
15and shod your feet with [the] preparation of the glad tidings of peace:
15na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
16besides all [these], having taken the shield of faith with which ye will be able to quench all the inflamed darts of the wicked one.
16Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
17Have also the helmet of salvation, and the sword of the Spirit, which is God's word;
17Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
18praying at all seasons, with all prayer and supplication in [the] Spirit, and watching unto this very thing with all perseverance and supplication for all the saints;
18Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
19and for me in order that utterance may be given to me in [the] opening of my mouth to make known with boldness the mystery of the glad tidings,
19Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
20for which I am an ambassador [bound] with a chain, that I may be bold in it as I ought to speak.
20Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
21But in order that *ye* also may know what concerns me, how I am getting on, Tychicus, the beloved brother and faithful minister in [the] Lord, shall make all things known to you;
21Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
22whom I have sent to you for this very thing, that ye may know of our affairs and that he may encourage your hearts.
22Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
23Peace to the brethren, and love with faith, from God [the] Father and [the] Lord Jesus Christ.
23Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
24Grace with all them that love our Lord Jesus Christ in incorruption.
24Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.