1Wherefore, holy brethren, partakers of [the] heavenly calling, consider the Apostle and High Priest of our confession, Jesus,
1Ndugu zangu watu wa Mungu ambao mmeitwa na Mungu, fikirini juu ya Yesu ambaye Mungu alimtuma awe Kuhani Mkuu wa imani tunayoiungama.
2who is faithful to him that has constituted him, as Moses also in all his house.
2Yeye alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua kufanya kazi yake kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
3For *he* has been counted worthy of greater glory than Moses, by how much he that has built it has more honour than the house.
3Mjenzi wa nyumba hupata heshima zaidi kuliko hiyo nyumba yenyewe. Hali kadhalika naye Yesu anastahili heshima kubwa zaidi kuliko Mose.
4For every house is built by some one; but he who has built all things [is] God.
4Kila nyumba hujengwa na mjenzi fulani--na Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote.
5And Moses indeed [was] faithful in all his house, as a ministering servant, for a testimony of the things to be spoken after;
5Mose alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Bwana kama mtumishi, na alinena juu ya mambo ambayo Mungu atayasema hapo baadaye.
6but Christ, as Son over his house, whose house are *we*, if indeed we hold fast the boldness and the boast of hope firm to the end.
6Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana mwenye mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tukizingatia uhodari wetu na uthabiti wetu katika kile tunachotumainia.
7Wherefore, even as says the Holy Spirit, To-day if ye will hear his voice,
7Kwa hiyo, basi, kama asemavyo Roho Mtakatifu: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo,
8harden not your hearts, as in the provocation, in the day of temptation in the wilderness;
8msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu; kama walivyokuwa siku ile kule jangwani,
9where your fathers tempted [me], by proving [me], and saw my works forty years.
9Huko wazee wenu walinijaribu na kunichunguza, asema Bwana, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu kwa miaka arobaini.
10Wherefore I was wroth with this generation, and said, They always err in heart; and *they* have not known my ways;
10Kwa sababu hiyo niliwakasirikia watu hao nikasema, Fikira za watu hawa zimepotoka, hawajapata kamwe kuzijua njia zangu.
11so I swore in my wrath, If they shall enter into my rest.
11Basi, nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko."
12See, brethren, lest there be in any one of you a wicked heart of unbelief, in turning away from [the] living God.
12Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai.
13But encourage yourselves each day, as long as it is called To-day, that none of you be hardened by the deceitfulness of sin.
13Maadamu hiyo "Leo" inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi.
14For we are become companions of the Christ if indeed we hold the beginning of the assurance firm to the end;
14Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni.
15in that it is said, To-day if ye will hear his voice, do not harden your hearts, as in the provocation;
15Maandiko yasema hivi: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu."
16(for who was it, who, having heard, provoked? but [was it] not all who came out of Egypt by Moses?
16Ni akina nani basi, waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri.
17And with whom was he wroth forty years? [Was it] not with those who had sinned, whose carcases fell in the wilderness?
17Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arobaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani.
18And to whom sware he that they should not enter into his rest, but to those who had not hearkened to the word?
18Mungu alipoapa: "Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko," alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi.
19And we see that they could not enter in on account of unbelief;)
19Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.