1My brethren, do not have the faith of our Lord Jesus Christ, [Lord] of glory, with respect of persons:
1Ndugu zangu, mkiwa mnamwamini Bwana Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwabague watu kamwe.
2for if there come unto your synagogue a man with a gold ring in splendid apparel, and a poor man also come in in vile apparel,
2Tuseme mtu mmoja ambaye amevaa pete ya dhahabu na mavazi nadhifu anaingia katika mkutano wenu, na papo hapo akaingia mtu maskini aliyevaa mavazi machafu.
3and ye look upon him who wears the splendid apparel, and say, Do thou sit here well, and say to the poor, Do thou stand there, or sit here under my footstool:
3Ikiwa mtamstahi zaidi yule aliyevaa mavazi ya kuvutia na kumwambia: "Keti hapa mahali pazuri," na kumwambia yule maskini: "Wewe, simama huko," au "Keti hapa sakafuni miguuni pangu,"
4have ye not made a difference among yourselves, and become judges having evil thoughts?
4je, huo si ubaguzi kati yenu? Je, na huo uamuzi wenu haujatokana na fikira mbaya?
5Hear, my beloved brethren: Has not God chosen the poor as to the world, rich in faith, and heirs of the kingdom, which he has promised to them that love him?
5Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni! Mungu amechagua watu ambao ni maskini katika ulimwengu huu ili wapate kuwa matajiri katika imani na kupokea Utawala aliowaahidia wale wanaompenda.
6But *ye* have despised the poor [man]. Do not the rich oppress you, and [do not] *they* drag you before [the] tribunals?
6Lakini ninyi mnawadharau watu maskini! Je, matajiri si ndio wanaowakandamizeni na kuwapeleka mahakamani?
7And [do not] *they* blaspheme the excellent name which has been called upon you?
7Je, si haohao wanaolitukana hilo jina lenu zuri mlilopewa?
8If indeed ye keep [the] royal law according to the scripture, Thou shalt love thy neighbour as thyself, ye do well.
8Kama mnaitimiza ile sheria ya Utawala kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: "Mpende binadamu mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe", mtakuwa mnafanya vema kabisa.
9But if ye have respect of persons, ye commit sin, being convicted by the law as transgressors.
9Lakini mkiwabagua watu, basi, mwatenda dhambi, nayo Sheria inawahukumu ninyi kuwa mna hatia.
10For whoever shall keep the whole law and shall offend in one [point], he has come under the guilt of [breaking] all.
10Anayevunja amri mojawapo ya Sheria, atakuwa na hatia ya kuivunja Sheria yote.
11For he who said, Thou shalt not commit adultery, said also, Thou shalt not kill. Now if thou dost not commit adultery, but killest, thou art become transgressor of [the] law.
11Maana yuleyule aliyesema: "Usizini," alisema pia "Usiue". Kwa hiyo, hata ikiwa hukuzini lakini umeua, wewe umeivunja Sheria.
12So speak ye, and so act, as those that are to be judged by [the] law of liberty;
12Basi, semeni na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria iletayo uhuru.
13for judgment [will be] without mercy to him that has shewn no mercy. Mercy glories over judgment.
13Maana, Mungu hatakuwa na huruma atakapomhukumu mtu asiyekuwa na huruma. Lakini huruma hushinda hukumu.
14What [is] the profit, my brethren, if any one say he have faith, but have not works? can faith save him?
14Ndugu zangu, kuna faida gani mtu kusema ana imani, lakini haonyeshi kwa vitendo? Je, hiyo imani yawezaje kumwokoa?
15Now if a brother or a sister is naked and destitute of daily food,
15Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula.
16and one from amongst you say to them, Go in peace, be warmed and filled; but give not to them the needful things for the body, what [is] the profit?
16Yafaa kitu gani ninyi kuwaambia hao: "Nendeni salama mkaote moto na kushiba," bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?
17So also faith, if it have not works, is dead by itself.
17Vivyo hivyo, imani peke yake bila matendo imekufa.
18But some one will say, *Thou* hast faith and *I* have works. Shew me thy faith without works, and *I* from my works will shew thee my faith.
18Lakini mtu anaweza kusema: "Wewe unayo imani, mimi ninayo matendo!" Haya! Nionyeshe jinsi mtu anavyoweza kuwa na imani bila matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.
19*Thou* believest that God is one. Thou doest well. The demons even believe, and tremble.
19Je, wewe unaamini kwamba yuko Mungu mmoja? Sawa! Lakini hata pepo huamini hilo, na hutetemeka kwa hofu.
20But wilt thou know, O vain man, that faith without works is dead?
20Mpumbavu wee! Je, wataka kuonyeshwa kwamba imani bila matendo imekufa?
21Was not Abraham our father justified by works when he had offered Isaac his son upon the altar?
21Je, Abrahamu baba yetu alipataje kukubalika mbele yake Mungu? Kwa matendo yake, wakati alipomtoa mwanae Isaka sadaka juu ya madhabahu.
22Thou seest that faith wrought with his works, and that by works faith was perfected.
22Waona basi, kwamba imani yake iliandamana na matendo yake; imani yake ilikamilishwa kwa matendo yake.
23And the scripture was fulfilled which says, Abraham believed God, and it was reckoned to him as righteousness, and he was called Friend of God.
23Hivyo yakatimia yale Maandiko Matakatifu yasemayo: "Abrahamu alimwamini Mungu na kwa imani yake akakubaliwa kuwa mtu mwadilifu; na hivyo Abrahamu akaitwa rafiki wa Mungu."
24Ye see that a man is justified on the principle of works, and not on the principle of faith only.
24Mnaona basi, kwamba mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa matendo yake na si kwa imani peke yake.
25But was not in like manner also Rahab the harlot justified on the principle of works, when she had received the messengers and put [them] forth by another way?
25Ilikuwa vivyo hivyo kuhusu yule malaya Rahabu; yeye alikubaliwa kuwa mwadilifu kwa sababu aliwapokea wale wapelelezi na kuwasaidia waende zao kwa kupitia njia nyingine.
26For as the body without a spirit is dead, so also faith without works is dead.
26Basi, kama vile mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo imani bila matendo imekufa.