1And on the third day a marriage took place in Cana of Galilee, and the mother of Jesus was there.
1Siku ya tatu kulikuwa na arusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,
2And Jesus also, and his disciples, were invited to the marriage.
2naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
3And wine being deficient, the mother of Jesus says to him, They have no wine.
3Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, "Hawana divai!"
4Jesus says to her, What have I to do with thee, woman? mine hour has not yet come.
4Yesu akamjibu, "Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado."
5His mother says to the servants, Whatever he may say to you, do.
5Hapo mama yake akawaambia watumishi, "Lolote atakalowaambieni, fanyeni."
6Now there were standing there six stone water-vessels, according to the purification of the Jews, holding two or three measures each.
6Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
7Jesus says to them, Fill the water-vessels with water. And they filled them up to the brim.
7Yesu akawaambia, "Ijazeni mitungi hiyo maji." Nao wakaijaza mpaka juu.
8And he says to them, Draw out now, and carry [it] to the feast-master. And they carried [it].
8Kisha akawaambia, "Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu."
9But when the feast-master had tasted the water which had been made wine (and knew not whence it was, but the servants knew who drew the water), the feast-master calls the bridegroom,
9Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,
10and says to him, Every man sets on first the good wine, and when [men] have well drunk, then the inferior; thou hast kept the good wine till now.
10akamwambia, "Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!"
11This beginning of signs did Jesus in Cana of Galilee, and manifested his glory; and his disciples believed on him.
11Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonyesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini.
12After this he descended to Capernaum, he and his mother and his brethren and his disciples; and there they abode not many days.
12Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache.
13And the passover of the Jews was near, and Jesus went up to Jerusalem.
13Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
14And he found in the temple the sellers of oxen and sheep and doves, and the money-changers sitting;
14Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao.
15and, having made a scourge of cords, he cast [them] all out of the temple, both the sheep and the oxen; and he poured out the change of the money-changers, and overturned the tables,
15Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya Hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazimwaga sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao.
16and said to the sellers of doves, Take these things hence; make not my Father's house a house of merchandise.
16Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, "Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!"
17[And] his disciples remembered that it is written, The zeal of thy house devours me.
17Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: "Upendo wangu kwa nyumba yako waniua."
18The Jews therefore answered and said to him, What sign shewest thou to us, that thou doest these things?
18Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, "Utafanya muujiza gani kuonyesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?"
19Jesus answered and said to them, Destroy this temple, and in three days I will raise it up.
19Yesu akawaambia, "Vunjeni Hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu."
20The Jews therefore said, Forty and six years was this temple building, and thou wilt raise it up in three days?
20Hapo Wayahudi wakasema, "Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?"
21But *he* spoke of the temple of his body.
21Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya Hekalu ambalo ni mwili wake.
22When therefore he was raised from among [the] dead, his disciples remembered that he had said this, and believed the scripture and the word which Jesus had spoken.
22Basi, alipofufuliwa kutoka wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno aliyokuwa akisema Yesu.
23And when he was in Jerusalem, at the passover, at the feast, many believed on his name, beholding his signs which he wrought.
23Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizozifanya.
24But Jesus himself did not trust himself to them, because he knew all [men],
24Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote.
25and that he had not need that any should testify of man, for himself knew what was in man.
25Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.