Darby's Translation

Swahili: New Testament

Luke

18

1And he spoke also a parable to them to the purport that they should always pray and not faint,
1Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.
2saying, There was a judge in a city, not fearing God and not respecting man:
2Alisema: "Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.
3and there was a widow in that city, and she came to him, saying, Avenge me of mine adverse party.
3Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.
4And he would not for a time; but afterwards he said within himself, If even I fear not God and respect not man,
4Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,
5at any rate because this widow annoys me I will avenge her, that she may not by perpetually coming completely harass me.
5lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!"
6And the Lord said, Hear what the unjust judge says.
6Basi, Bwana akaendelea kusema, "Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.
7And shall not God at all avenge his elect, who cry to him day and night, and he bears long as to them?
7Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?
8I say unto you that he will avenge them speedily. But when the Son of man comes, shall he indeed find faith on the earth?
8Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?"
9And he spoke also to some, who trusted in themselves that they were righteous and made nothing of all the rest [of men], this parable:
9Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.
10Two men went up into the temple to pray; the one a Pharisee, and the other a tax-gatherer.
10"Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.
11The Pharisee, standing, prayed thus to himself: God, I thank thee that I am not as the rest of men, rapacious, unjust, adulterers, or even as this tax-gatherer.
11Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.
12I fast twice in the week, I tithe everything I gain.
12Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.
13And the tax-gatherer, standing afar off, would not lift up even his eyes to heaven, but smote upon his breast, saying, O God, have compassion on me, the sinner.
13Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.
14I say unto you, This [man] went down to his house justified rather than that [other]. For every one who exalts himself shall be humbled, and he that humbles himself shall be exalted.
14Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa."
15And they brought to him also infants that he might touch them, but the disciples when they saw [it] rebuked them.
15Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.
16But Jesus calling them to [him] said, Suffer little children to come to me, and do not forbid them, for of such is the kingdom of God.
16Lakini Yesu akawaita kwake akisema: "Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.
17Verily I say to you, Whosoever shall not receive the kingdom of God as a little child shall in no wise enter therein.
17Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo."
18And a certain ruler asked him saying, Good teacher, having done what, shall I inherit eternal life?
18Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, "Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?"
19But Jesus said to him, Why callest thou me good? There is none good but one, God.
19Yesu akamwambia, "Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
20Thou knowest the commandments: Do not commit adultery, Do not kill, Do not steal, Do not bear false witness, Honour thy father and thy mother.
20Unazijua amri: Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako."
21And he said, All these things have I kept from my youth.
21Yeye akasema, "Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu."
22And when Jesus had heard this, he said to him, One thing is lacking to thee yet: Sell all that thou hast and distribute to the poor, and thou shalt have treasure in the heavens, and come, follow me.
22Yesu aliposikia hayo akamwambia, "Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate."
23But when he heard this he became very sorrowful, for he was very rich.
23Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.
24But when Jesus saw that he became very sorrowful, he said, How difficultly shall those who have riches enter into the kingdom of God;
24Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, "Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
25for it is easier for a camel to enter through a needle's eye than for a rich man to enter into the kingdom of God.
25Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu."
26And those who heard it said, And who can be saved?
26Wale watu waliposikia hayo, wakasema, "Nani basi, atakayeokolewa?"
27But he said, The things that are impossible with men are possible with God.
27Yesu akajibu, "Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu."
28And Peter said, Behold, *we* have left all things and have followed thee.
28Naye Petro akamwuliza, "Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!"
29And he said to them, Verily I say to you, There is no one who has left home, or parents, or brethren, or wife, or children, for the kingdom of God's sake,
29Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
30who shall not receive manifold more at this time, and in the coming age life eternal.
30atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao."
31And he took the twelve to [him] and said to them, Behold, we go up to Jerusalem, and all things that are written of the Son of man by the prophets shall be accomplished;
31Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, "Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
32for he shall be delivered up to the nations, and shall be mocked, and insulted, and spit upon.
32Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
33And when they have scourged [him] they will kill him; and on the third day he will rise again.
33Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka."
34And they understood nothing of these things. And this word was hidden from them, and they did not know what was said.
34Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
35And it came to pass when he came into the neighbourhood of Jericho, a certain blind man sat by the wayside begging.
35Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
36And when he heard the crowd passing, he inquired what this might be.
36Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, "Kuna nini?"
37And they told him that Jesus the Nazaraean was passing by.
37Wakamwambia, "Yesu wa Nazareti anapita."
38And he called out saying, Jesus, Son of David, have mercy on me.
38Naye akapaza sauti akisema, "Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!"
39And those [who were] going before rebuked him that he might be silent; but *he* cried out so much the more, Son of David, have mercy on me.
39Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: "Mwana wa Daudi, nihurumie;"
40And Jesus stood still, and commanded him to be led to him. And when he drew nigh he asked him [saying],
40Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,
41What wilt thou that I shall do to thee? And he said, Lord, that I may see.
41"Unataka nikufanyie nini?" Naye akamjibu, "Bwana, naomba nipate kuona tena."
42And Jesus said to him, See: thy faith has healed thee.
42Yesu akamwambia, "Ona! Imani yako imekuponya."
43And immediately he saw, and followed him, glorifying God. And all the people when they saw [it] gave praise to God.
43Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.