Darby's Translation

Swahili: New Testament

Luke

22

1Now the feast of unleavened bread, which [is] called the passover, drew nigh,
1Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
2and the chief priests and the scribes sought how they might kill him; for they feared the people.
2Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
3And Satan entered into Judas, who was surnamed Iscariote, being of the number of the twelve.
3Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
4And he went away and spoke with the chief priests and captains as to how he should deliver him up to them.
4Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
5And they were rejoiced, and agreed to give him money.
5Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
6And he came to an agreement to do it, and sought an opportunity to deliver him up to them away from the crowd.
6Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
7And the day of unleavened bread came, in which the passover was to be killed.
7Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
8And he sent Peter and John, saying, Go and prepare the passover for us, that we may eat [it].
8Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, "Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka."
9But they said to him, Where wilt thou that we prepare [it]?
9Nao wakamwuliza, "Unataka tuiandae wapi?"
10And he said to them, Behold, as ye enter into the city a man will meet you, carrying an earthen pitcher of water; follow him into the house where he goes in;
10Akawaambia, "Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
11and ye shall say to the master of the house, The Teacher says to thee, Where is the guest-chamber where I may eat the passover with my disciples?
11Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
12And *he* will shew you a large upper room furnished: there make ready.
12Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo."
13And having gone they found it as he had said to them; and they prepared the passover.
13Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
14And when the hour was come, he placed himself at table, and the [twelve] apostles with him.
14Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
15And he said to them, With desire I have desired to eat this passover with you before I suffer.
15Akawaambia, "Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
16For I say unto you, that I will not eat any more at all of it until it be fulfilled in the kingdom of God.
16Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu."
17And having received a cup, when he had given thanks he said, Take this and divide it among yourselves.
17Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, "Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
18For I say unto you, that I will not drink at all of the fruit of the vine until the kingdom of God come.
18Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja."
19And having taken a loaf, when he had given thanks, he broke [it], and gave [it] to them, saying, This is my body which is given for you: this do in remembrance of me.
19Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, "Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
20In like manner also the cup, after having supped, saying, This cup [is] the new covenant in my blood, which is poured out for you.
20Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, "Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
21Moreover, behold, the hand of him that delivers me up [is] with me on the table;
21"Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
22and the Son of man indeed goes as it is determined, but woe unto that man by whom he is delivered up.
22Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti."
23And *they* began to question together among themselves who then it could be of them who was about to do this.
23Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
24And there was also a strife among them which of them should be held to be [the] greatest.
24Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
25And he said to them, The kings of the nations rule over them, and they that exercise authority over them are called benefactors.
25Yesu akawaambia, "Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
26But *ye* [shall] not [be] thus; but let the greater among you be as the younger, and the leader as he that serves.
26Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
27For which [is] greater, he that is at table or he that serves? [Is] not he that is at table? But *I* am in the midst of you as the one that serves.
27Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
28But *ye* are they who have persevered with me in my temptations.
28"Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
29And *I* appoint unto you, as my Father has appointed unto me, a kingdom,
29na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
30that ye may eat and drink at my table in my kingdom, and sit on thrones judging the twelve tribes of Israel.
30Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
31And the Lord said, Simon, Simon, behold, Satan has demanded to have you, to sift [you] as wheat;
31"Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
32but *I* have besought for thee that thy faith fail not; and *thou*, when once thou hast been restored, confirm thy brethren.
32Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako."
33And he said to him, Lord, with thee I am ready to go both to prison and to death.
33Naye Petro akamjibu, "Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa."
34And he said, I tell thee, Peter, [the] cock shall not crow to-day before that thou shalt thrice deny that thou knowest me.
34Yesu akamjibu, "Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu."
35And he said to them, When I sent you without purse and scrip and sandals, did ye lack anything? And they said, Nothing.
35Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, "Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?" Wakajibu, "La."
36He said therefore to them, But now he that has a purse let him take [it], in like manner also a scrip, and he that has none let him sell his garment and buy a sword;
36Naye akawaambia, "Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
37for I say unto you, that this that is written must yet be accomplished in me, And he was reckoned with [the] lawless: for also the things concerning me have an end.
37Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake."
38And they said, Lord, behold here are two swords. And he said to them, It is enough.
38Nao wakasema, "Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili." Naye akasema, "Basi!"
39And going forth he went according to his custom to the mount of Olives, and the disciples also followed him.
39Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
40And when he was at the place he said to them, Pray that ye enter not into temptation.
40Alipofika huko akawaambia, "Salini, msije mkaingia katika kishawishi."
41And he was withdrawn from them about a stone's throw, and having knelt down he prayed,
41Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
42saying, Father, if thou wilt remove this cup from me: -- but then, not my will, but thine be done.
42"Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu."
43And an angel appeared to him from heaven strengthening him.
43Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
44And being in conflict he prayed more intently. And his sweat became as great drops of blood, falling down upon the earth.
44Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
45And rising up from his prayer, coming to the disciples, he found them sleeping from grief.
45Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
46And he said to them, Why sleep ye? rise up and pray that ye enter not into temptation.
46Akawaambia, "Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi."
47As he was yet speaking, behold, a crowd, and he that was called Judas, one of the twelve, went on before them, and drew near to Jesus to kiss him.
47Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
48And Jesus said to him, Judas, deliverest thou up the Son of man with a kiss?
48Lakini Yesu akamwambia, "Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?"
49And they who were around him, seeing what was going to follow, said [to him], Lord, shall we smite with [the] sword?
49Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, "Bwana, tutumie panga zetu?"
50And a certain one from among them smote the bondman of the high priest and took off his right ear.
50Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
51And Jesus answering said, Suffer thus far; and having touched his ear, he healed him.
51Hapo, Yesu akasema, "Acha! Hii inatosha." Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
52And Jesus said to the chief priests and captains of the temple and elders, who were come against him, Have ye come out as against a robber with swords and sticks?
52Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: "Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
53When I was day by day with you in the temple ye did not stretch out your hands against me; but this is your hour and the power of darkness.
53Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza."
54And having laid hold on him, they led him [away], and they led [him] into the house of the high priest. And Peter followed afar off.
54Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
55And they having lit a fire in the midst of the court and sat down together, Peter sat among them.
55Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
56And a certain maid, having seen him sitting by the light, and having fixed her eyes upon him, said, And this [man] was with him.
56Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, "Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu."
57But he denied [him], saying, Woman, I do not know him.
57Lakini Petro akakana akisema, "Wee! simjui mimi."
58And after a short time another seeing him said, And *thou* art of them. But Peter said, Man, I am not.
58Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, "Wewe ni mmoja wao." Lakini Petro akajibu "Bwana we; si mimi!"
59And after the lapse of about one hour another stoutly maintained it, saying, In truth this [man] also was with him, for also he is a Galilaean.
59Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, "Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati."
60And Peter said, Man, I know not what thou sayest. And immediately, while he was yet speaking, [the] cock crew.
60Lakini Petro akasema, "Bwana wee; sijui hata unachosema!" Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
61And the Lord, turning round, looked at Peter; and Peter remembered the word of the Lord, how he said to him, Before [the] cock crow thou shalt deny me thrice.
61Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: "Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
62And Peter, going forth without, wept bitterly.
62Hapo akatoka nje, akalia sana.
63And the men who held him mocked him, beating [him];
63Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
64and covering him up, asked him saying, Prophesy, who is it that struck thee?
64Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, "Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!"
65And they said many other injurious things to him.
65Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
66And when it was day, the elderhood of the people, both [the] chief priests and scribes, were gathered together, and led him into their council, saying,
66Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
67If *thou* art the Christ, tell us. And he said to them, If I tell you, ye will not at all believe;
67Nao wakamwambia, "Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?" Lakini Yesu akawaambia, "Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
68and if I should ask [you], ye would not answer me at all, nor let me go;
68na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
69but henceforth shall the Son of man be sitting on the right hand of the power of God.
69Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi."
70And they all said, *Thou* then art the Son of God? And he said to them, *Ye* say that I am.
70Hapo wote wakasema, "Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?" Naye akasema, "Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye."
71And they said, What need have we any more of witness, for we have heard ourselves out of his mouth?
71Nao wakasema, "Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe."