1I say then, Has God cast away his people? Far be the thought. For *I* also am an Israelite, of [the] seed of Abraham, of [the] tribe of Benjamin.
1Basi, nauliza: je, Mungu amewakataa watu wake? Hata kidogo! Mini binafsi ni Mwisraeli mzawa wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.
2God has not cast away his people whom he foreknew. Know ye not what the scripture says in [the history of] Elias, how he pleads with God against Israel?
2Mungu hakuwakataa watu wake aliowateua tangu mwanzo. Mnakumbuka yasemavyo Maandiko Matakatifu juu ya Eliya wakati alipomnung'unikia Mungu kuhusu Israeli:
3Lord, they have killed thy prophets, they have dug down thine altars; and *I* have been left alone, and they seek my life.
3"Bwana, wamewaua manabii wako na kubomoa madhabahu yako. Ni mimi tu peke yangu niliyebaki, nao wanataka kuniua?"
4But what says the divine answer to him? I have left to myself seven thousand men, who have not bowed knee to Baal.
4Je, Mungu alimjibu nini? Alimwambia: "Nimejiwekea elfu saba ambao hawakumwabudu Baali."
5Thus, then, in the present time also there has been a remnant according to election of grace.
5Basi, ndivyo ilivyo pia wakati huu wa sasa: ipo idadi ya waliobaki ambao Mungu aliwateua kwa sababu ya neema yake.
6But if by grace, no longer of works: since [otherwise] grace is no more grace.
6Uteuzi wake unatokana na neema yake, na si kwa sababu ya matendo yao. Maana, kama uteuzi wake ungetegemea matendo ya watu, neema yake haingekuwa neema tena.
7What [is it] then? What Israel seeks for, that he has not obtained; but the election has obtained, and the rest have been blinded,
7Sasa, je? Watu wa Israeli hawakukipata kile walichokuwa wanakitafuta; lakini wote walioteuliwa walikipata. Wengine walipumbazwa,
8according as it is written, God has given to them a spirit of slumber, eyes not to see, and ears not to hear, unto this day.
8kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mungu ameifanya mioyo yao kuwa mizito, na mpaka leo hii hawawezi kuona kwa macho yao wala kusikia kwa masikio yao."
9And David says, Let their table be for a snare, and for a gin, and for a fall-trap, and for a recompense to them:
9Naye Daudi anasema: "Karamu zao na ziwe mtego wa kuwanasa, waanguke na kuadhibiwa.
10let their eyes be darkened not to see, and bow down their back alway.
10Macho yao yatiwe giza wasiweze kuona. Migongo yao ipindike kwa taabu daima!"
11I say then, Have they stumbled in order that they might fall? Far be the thought: but by their fall [there is] salvation to the nations to provoke them to jealousy.
11Basi, nauliza: je, Wayahudi wamejikwaa hata wakaangamia kabisa? Hata kidogo! Kutokana na kosa lao ukombozi umewajia watu wa mataifa mengine, ili Wayahudi wapate kuwaonea wivu.
12But if their fall [be the] world's wealth, and their loss [the] wealth of [the] nations, how much rather their fulness?
12Kosa la Wayahudi limesababisha baraka nyingi kwa ulimwengu, na utovu wao kwa kiroho umeleta baraka nyingi kwa watu wa mataifa mengine. Basi, ni dhahiri zaidi kwamba utimilifu wao utasababisha baraka nyingi zaidi.
13For I speak to you, the nations, inasmuch as *I* am apostle of nations, I glorify my ministry;
13Basi, sasa nawaambieni ninyi watu wa mataifa mengine: Maadamu mimi nimekuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine, ninajivunia huduma yangu,
14if by any means I shall provoke to jealousy [them which are] my flesh, and shall save some from among them.
14nipate kuwafanya wananchi wenzangu wawaonee ninyi wivu, na hivyo nipate kuwaokoa baadhi yao.
15For if their casting away [be the] world's reconciliation, what [their] reception but life from among [the] dead?
15Maana ikiwa kukataliwa kwao kulisababisha ulimwengu upatanishwe na Mungu, itakuwaje wakati watakapokubaliwa na Mungu? Wafu watafufuka!
16Now if the first-fruit [be] holy, the lump also; and if the root [be] holy, the branches also.
16Ikiwa kipande cha kwanza cha mkate kimewekwa wakfu, mkate wote umewekwa wakfu; mizizi ya mti ikiwa mizuri, na matawi yake huwa mazuri pia.
17Now if some of the branches have been broken out, and *thou*, being a wild olive tree, hast been grafted in amongst them, and hast become a fellow-partaker of the root and of the fatness of the olive tree,
17Naam, baadhi ya matawi ya mzeituni bustanini yalikatwa, na mahali pake tawi la mzeituni mwitu likapandikizwa. Ninyi watu wa mataifa mengine ndio hilo tawi la mzeituni mwitu; na sasa mnashiriki nguvu na utomvu wa mzeituni bustanini.
18boast not against the branches; but if thou boast, [it is] not *thou* bearest the root, but the root thee.
18Basi, msiwadharau wale waliokatwa kama matawi! Na, hata kama kuna la kujivunia, kumbukeni kwamba si ninyi mnaoitegemeza mizizi, bali mizizi ndiyo inayowategemeza ninyi.
19Thou wilt say then, The branches have been broken out in order that *I* might be grafted in.
19Lakini utasema: "Matawi yalikatwa kusudi mimi nipandikizwe mahali pake."
20Right: they have been broken out through unbelief, and *thou* standest through faith. Be not high-minded, but fear:
20Sawa! Yalikatwa kwa sababu ya kukosa imani, bali wewe unasimama kwa imani yako. Lakini usijivune; ila uwe na tahadhari.
21if God indeed has not spared the natural branches; lest it might be he spare not thee either.
21Kwa maana, ikiwa Mungu hakuwahurumia Wayahudi ambao ni kama matawi ya asili, je, unadhani atakuhurumia wewe?
22Behold then [the] goodness and severity of God: upon them who have fallen, severity; upon thee goodness of God, if thou shalt abide in goodness, since [otherwise] *thou* also wilt be cut away.
22Kumbuka, basi, jinsi Mungu alivyo mwema na mkali. Yeye ni mkali kwa wale walioanguka, na ni mwema kwako wewe ikiwa utaendelea katika wema wake; la sivyo, nawe pia utakatwa.
23And *they* too, if they abide not in unbelief, shall be grafted in; for God is able again to graft them in.
23Nao Wayahudi, hali kadhalika; wakiacha utovu wao wa imani, watapandikizwa tena. Maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena.
24For if *thou* hast been cut out of the olive tree wild by nature, and, contrary to nature, hast been grafted into the good olive tree, how much rather shall they, who are according to nature be grafted into their own olive tree?
24Ninyi watu wa mataifa mengine, kwa asili ni kama tawi la mzeituni mwitu, lakini mmeondolewa huko, mkapandikizwa katika mzeituni bustanini mahali ambapo kwa asili si penu. Lakini, Wayahudi kwa asili ni kama mzeituni bustanini, na itakuwa jambo rahisi zaidi kwao kupandikizwa tena katika mti huohuo wao.
25For I do not wish you to be ignorant, brethren, of this mystery, that ye may not be wise in your own conceits, that blindness in part is happened to Israel, until the fulness of the nations be come in;
25Ndugu zangu, napenda mjue ukweli huu uliofichika msije mkajiona wenye akili sana. Ukaidi wa Wayahudi ulikuwa ni wa muda tu, mpaka watu wa mataifa mengine watakapokuwa wamemfikia Mungu.
26and so all Israel shall be saved. According as it is written, The deliverer shall come out of Zion; he shall turn away ungodliness from Jacob.
26Hapo ndipo taifa lote la Israeli litakapookolewa, kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: "Mkombozi atakuja kutoka Sioni, atauondoa uovu wa Yakobo.
27And this is the covenant from me to them, when I shall have taken away their sins.
27Hili ndilo agano nitakalofanya nao wakati nitakapoziondoa dhambi zao."
28As regards the glad tidings, [they are] enemies on your account; but as regards election, beloved on account of the fathers.
28Kwa sababu wanaikataa Habari Njema, Wayahudi wamekuwa adui wa Mungu, lakini kwa faida yenu nyinyi watu wa mataifa. Lakini, kwa kuwa waliteuliwa, bado ni rafiki wa Mungu kwa sababu ya baba zao.
29For the gifts and the calling of God [are] not subject to repentance.
29Maana Mungu akisha wapa watu zawadi zake na kuwateua, hajuti kwamba amefanya hivyo.
30For as indeed *ye* [also] once have not believed in God, but now have been objects of mercy through the unbelief of *these*;
30Hapo awali ninyi mlikuwa mmemwasi Mungu, lakini sasa mmepata huruma yake kutokana na kuasi kwao.
31so these also have now not believed in your mercy, in order that *they* also may be objects of mercy.
31Hali kadhalika, kutokana na huruma mliyojaliwa ninyi, Wayahudi wanamwasi Mungu sasa ili nao pia wapokee sasa huruma ya Mungu.
32For God hath shut up together all in unbelief, in order that he might shew mercy to all.
32Maana Mungu amewafunga watu wote katika uasi wao ili wapate kuwahurumia wote.
33O depth of riches both of [the] wisdom and knowledge of God! how unsearchable his judgments, and untraceable his ways!
33Utajiri, hekima na elimu ya Mungu ni kuu mno! Huruma zake hazichunguziki, na njia zake hazieleweki! Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:
34For who has known [the] mind of [the] Lord, or who has been his counsellor?
34"Nani aliyepata kuyajua mawazo ya Bwana? Nani awezaye kuwa mshauri wake?
35or who has first given to him, and it shall be rendered to him?
35Au, nani aliyempa yeye kitu kwanza hata aweze kulipwa tena kitu hicho?"
36For of him, and through him, and for him [are] all things: to him be glory for ever. Amen.
36Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, vyote vipo kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Utukufu na uwe kwake hata milele! Amina.