Darby's Translation

Swahili: New Testament

Romans

12

1I beseech you therefore, brethren, by the compassions of God, to present your bodies a living sacrifice, holy, acceptable to God, [which is] your intelligent service.
1Kwa hiyo, ndugu zangu, maadam Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: jitoleeni nafsi zenu kwa Mungu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu.
2And be not conformed to this world, but be transformed by the renewing of [your] mind, that ye may prove what [is] the good and acceptable and perfect will of God.
2Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu, kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu.
3For I say, through the grace which has been given to me, to every one that is among you, not to have high thoughts above what he should think; but to think so as to be wise, as God has dealt to each a measure of faith.
3Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni ninyi nyote: msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kufuatana na kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.
4For, as in one body we have many members, but all the members have not the same office;
4Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake.
5thus we, [being] many, are one body in Christ, and each one members one of the other.
5Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.
6But having different gifts, according to the grace which has been given to us, whether [it be] prophecy, [let us prophesy] according to the proportion of faith;
6Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kufuatana na neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake.
7or service, [let us occupy ourselves] in service; or he that teaches, in teaching;
7Mwenye kipaji cha utumishi na atumikie. mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe.
8or he that exhorts, in exhortation; he that gives, in simplicity; he that leads, with diligence; he that shews mercy, with cheerfulness.
8Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha.
9Let love be unfeigned; abhorring evil; cleaving to good:
9Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.
10as to brotherly love, kindly affectioned towards one another: as to honour, each taking the lead in paying it to the other:
10Pendaneni kidugu; kila mmoja amfikirie mwenzake kwanza kwa heshima.
11as to diligent zealousness, not slothful; in spirit fervent; serving the Lord.
11Msilegee katika bidii, muwe wachangamfu rohoni katika kumtumikia Bwana.
12As regards hope, rejoicing: as regards tribulation, enduring: as regards prayer, persevering:
12Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida na kusali daima.
13distributing to the necessities of the saints; given to hospitality.
13Wasaidieni watu wa Mungu katika mahitaji yao; wapokeeni wageni kwa ukarimu.
14Bless them that persecute you; bless, and curse not.
14Watakieni baraka wote wanaowadhulumu ninyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani.
15Rejoice with those that rejoice, weep with those that weep.
15Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
16Have the same respect one for another, not minding high things, but going along with the lowly: be not wise in your own eyes:
16Muwe na wema uleule kwa kila mtu. Msijitakie makuu, bali jishugulisheni na watu wadogo. Msijione kuwa wenye hekima sana.
17recompensing to no one evil for evil: providing things honest before all men:
17Msilipe ovu kwa ovu. Zingatieni mambo mema mbele ya wote.
18if possible, as far as depends on you, living in peace with all men;
18Kadiri inavyowezekana kwa upande wenu, muwe na amani na watu wote.
19not avenging yourselves, beloved, but give place to wrath; for it is written, Vengeance [belongs] to me, *I* will recompense, saith the Lord.
19Wapenzi wangu, msilipize kisasi, bali mwachieni Mungu jambo hilo; maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kulipiza kisasi ni shauri langu; mimi nitalipiza asema Bwana."
20If therefore thine enemy should hunger, feed him; if he should thirst, give him drink; for, so doing, thou shalt heap coals of fire upon his head.
20Tena, Maandiko yasema: "Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Maana kwa kufanya hivyo utamfanya apate aibu kali kama makaa ya moto juu ya kichwa chake."
21Be not overcome by evil, but overcome evil with good.
21Usikubali kushindwa na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.