Kabyle: New Testament

Swahili: New Testament

Revelation

14

1Walaɣ Izimer-nni ibedd ɣef wedrar n Siyun, llan yid-es meyya uṛebɛa uṛebɛin alef n yemdanen yesɛan isem n Izimer-nni akk-d isem n Baba-s țwaketben ɣef yinyiren-nsen.
1Kisha nikaona mlima Sioni, na Mwanakondoo amesimama juu yake; pamoja naye walikuwa watu mia moja arobaini na nne elfu ambao juu ya paji za nyuso zao walikuwa wameandikwa jina la Mwanakondoo na jina la Baba yake.
2Sliɣ i ṣṣut n tuɣac i d-yekkan seg igenni, am akken d ṣṣut n lebḥeṛ m'ara yekker, am tiyita n ṛṛɛud ; ṣṣut n tuɣac-nni, yecba ṣṣut i d-ițeffɣen seg waṭas n snitrat.
2Basi, nikasikia sauti kutoka mbinguni, sauti iliyokuwa kama sauti ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo kubwa. Sauti niliyosikia ilikuwa kama sauti ya wachezaji muziki wakipiga vinubi vyao.
3?ɣennin yiwen ccna ajdid zdat wemkan n lḥekma, zdat ṛebɛa lexluq zdat lecyux-nni. Yiwen ur izmir ad yeḥfeḍ ccna-nni anagar meyya uṛebɛa uṛebɛin alef-nni i d-yețțuselken si ddunit.
3Walikuwa wanaimba wimbo mpya mbele ya kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe hai wanne na wale wazee. Hakuna mtu aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao watu mia moja arobaini na nne elfu waliokombolewa duniani.
4Wigi, d wid ur nezni ara, qqimen ṣfan ; anda iṛuḥ Izimer ad ddun yid-es. ?țuselken si ger yemdanen iwakken ad țțuqeddmen d imezwura i Sidi Ṛebbi akk-d Izimer.
4Watu hao ndio wale waliojiweka safi kwa kutoonana kimwili na wanawake, nao ni mabikira. Wao humfuata Mwanakondoo kokote aendako. Wamekombolewa kutoka miongoni mwa binadamu wengine, wakawa wa kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwanakondoo.
5Ur d-yeffiɣ lekdeb seg imawen nsen, ur yelli deg-sen wayen ara sen-d yețwassukksen.
5Hawakupata kamwe kuwa waongo; hawana hatia yoyote.
6Walaɣ yiwen lmelk yețțafgen deg igenni ; yewwi-d yid-es yiwen lexbaṛ n lxiṛ yețdumun i dayem iwakken a t-ibecceṛ i imezdaɣ n ddunit, i mkul lǧens, i mkul tamurt, i mkul agdud n mkul tutlayt.
6Kisha nikamwona malaika mwingine anaruka juu angani akiwa na Habari Njema ya milele ya Mungu, aitangaze kwa watu wote waishio duniani, kwa mataifa yote, makabila yote, watu wa lugha zote na rangi zote.
7Yeqqaṛ ed s taɣect ɛlayen : Aggadet Ṛebbi, ḥemmdet-eț axaṭer yewweḍ-ed wass n lḥisab. Seǧǧdet, ɛebdet Win i d-ixelqen igenni d lqaɛa, lebḥeṛ akk-d leɛwanseṛ n waman.
7Akasema kwa sauti kubwa, "Mcheni Mungu na kumtukuza! Maana saa imefika ya kutoa hukumu yake. Mwabuduni yeye aliyeumba mbingu na nchi, bahari na chemchemi za maji."
8Lmelk wis sin yetbeɛ amezwaru yeqqaṛ : Teɣli, teɣli temdint-nni n Babilun tameqqrant, tin i gesderɛen ( yessenṭḍen ) i leǧnas meṛṛa leḥṛam ines.
8Malaika wa pili alimfuata huyo wa kwanza akisema, "Ameanguka! Naam, Babuloni mkuu ameanguka! Babuloni ambaye aliwapa mataifa yote wainywe divai yake--divai kali ya uzinzi wake!"
9Lmelk wis tlata, yetbeɛ-iten yeqqaṛ s ṣṣut ɛlayen : Win ara iseǧden zdat leɛqiṛa akk-d lmeṣnuɛ-ines yerna yeqbel ticṛeṭ ɣef wunyir-is neɣ ɣef wufus-is,
9Na malaika wa tatu aliwafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, "Yeyote anayemwabudu yule mnyama na sanamu yake na kukubali kutiwa alama yake juu ya paji la uso wake au juu ya mkono wake,
10a d-yemmir fell-as wurrif n Sidi Ṛebbi, ad isew lemṛaṛ, ad inɛețțab di tmes d ukubri zdat lmalayekkat iqedsen, zdat Izimer.
10yeye mwenyewe atakunywa divai ya ghadhabu ya Mungu, ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake bila kuchanganywa na maji. Mtu huyo atateseka ndani ya moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele ya Mwanakondoo.
11Dexxan n tmes s wayes ara nɛețțaben ad yeqqim si lǧil ɣer lǧil ; wid yețseǧǧiden zdat leɛqiṛa d lmeṣuɛ ines akk-d kra win iqeblen ticṛeṭ n isem-is, ur steɛfayen ara iḍ d wass.
11Moshi wa moto unaowatesa kupanda juu milele na milele. Watu hao waliomwabudu huyo mnyama na sanamu yake, na kutiwa alama ya jina lake, hawatakuwa na nafuu yoyote usiku na mchana."
12Deg wannect-agi i d-yețban ṣṣbeṛ n wid yextaṛ Sidi Ṛebbi, wid i gḍuɛen lumuṛ-is yerna ṭṭfen di liman i sɛan di Lmasiḥ.
12Kutokana na hayo, ni lazima watu wa Mungu, yaani watu wanaotii amri ya Mungu na kumwamini Yesu, wawe na uvumilivu.
13Sliɣ i yiwet taɣect i d-yekkan seg igenni teqqaṛ : Aru ayagi, d iseɛdiyen si tura wid ara yemten yili nutni umnen s Lmasiḥ ! Ṛṛuḥ iqedsen yenna : ?-țideț, tura zemren ad steɛfun si leɛtab-nsen axaṭer lecɣal-nni yelhan i xedmen a ten-afen.
13Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, "Andika! Heri watu ambao tangu sasa wanakufa wakiwa wameungana na Bwana." Naye Roho asema, "Naam! Watapumzika kutoka taabu zao; maana matunda ya jasho lao yatawafuata."
14Walaɣ asigna d amellal, ɣef wusigna-nni yeqqim yiwen lxelq ițemcabi i wemdan. Yesɛa taɛeṣṣabt n ddheb ɣef wuqeṛṛuy-is, yeṭṭef amger iqeḍɛen deg ufus-is.
14Kisha nikatazama, na kumbe palikuwapo wingu jeupe hapo. Na juu ya wingu hilo kulikuwa na kiumbe kama mtu. Alikuwa amevaa taji ya dhahabu kichwani, na kushika mundu mkononi mwake.
15Yiwen lmelk nniḍen yeffeɣ-ed si lǧameɛ iqedsen, yețɛeggiḍ s ṣṣut ɛlayen i win yeqqimen ɣef wusigna yeqqaṛ-as : Ssexdem amger-ik tmegreḍ, axaṭer yewweḍ-ed lweqt n tmegra, imi ddunit tewjed i tmegra.
15Kisha malaika mwingine akatoka Hekaluni, na kwa sauti kubwa akamwambia yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu, "Tafadhali, tumia mundu wako ukavune mavuno, maana wakati wa mavuno umefika; mavuno ya dunia yameiva."
16Win akken yeqqimen ɣef wusigna yesɛedda amger-is ɣef ddunit dɣa ddunit meṛṛa tețwamger.
16Basi, yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu akautupa mundu wake duniani, na mavuno ya dunia yakavunwa.
17Yeffeɣ-ed lmelk nniḍen si lǧameɛ iqedsen yellan deg igenni ; ula d nețța yesɛa amger iqeḍɛen.
17Kisha malaika mwingine akatoka katika Hekalu mbinguni akiwa na mundu wenye makali.
18Lmelk nniḍen iḥekkmen ɣef tmes, yeffeɣ-ed seg wemkan anda yella udekkan n iseflawen, yenna s ṣṣut ɛlayen i lmelk-nni yesɛan amger iqeḍɛen : Ssexdem amger-ik tgezmeḍ iguza n tfeṛṛant n ddunit, axaṭer wwant tẓuṛin.
18Kisha malaika mwingine msimamizi wa moto, akatoka madhabahuni akamwambia kwa sauti kubwa yule malaika mwenye mundu wenye makali, "Nawe tia huo mundu wako mkali, ukakate vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva!"
19 Lmelk-nni yesɛedda amger-is ɣef ddunit, igzem iguza n tfeṛṛant n ddunit, iḍeggeṛ tizuṛin-nni zdaxel n teḥḍunt n wurrif n Sidi Ṛebbi, wwin-ț ɣer beṛṛa n temdint, iwakken ad ṛekḍen tizuṛin-nni, ffɣen-d seg-s idammen, ulin lqedd n lmitra d wezgen, uzzlen d leḥmali azal n telt-meyya n kilumitrat.
19Basi, malaika huyo akautupa mundu wake duniani, akakata zabibu za dunia, akazitia ndani ya chombo kikubwa cha kukamulia zabibu, chombo cha ghadhabu ya Mungu.
20Zabibu zikakamuliwa ndani ya hilo shinikizo lililoko nje ya mji, na damu ikatoka katika shinikizo hilo mtiririko mrefu kiasi cha mita mia tatu na kina chake kiasi cha mita mia mbili.