Lithuanian

Swahili: New Testament

1 Corinthians

7

1Atsakau į jūsų laišką. Gerai daro vyras, neliesdamas moters.
1Yahusu sasa mambo yale mliyoandika: naam, ni vizuri kama mtu haoi;
2Tačiau ištvirkavimui išvengti kiekvienas teturi sau žmoną ir kiekviena sau vyrą.
2lakini kwa sababu ya hatari ya uzinzi, basi, kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.
3Vyras teatlieka pareigą žmonai, o žmona vyrui.
3Mume atimize wajibu alio nao kwa mkewe, naye mke atimize wajibu alio nao kwa mumewe.
4Žmona neturi valios savo kūnui, bet vyras. Panašiai ir vyras neturi valios savo kūnui, bet žmona.
4Mke hana mamlaka juu ya mwili wake, bali mumewe anayo; hali kadhalika naye mume, hana mamlaka juu ya mwili wake, bali mkewe anayo.
5Nesitraukite vienas nuo kito, nebent abiems susitarus kuriam laikui, kad atsidėtumėte pasninkui ir maldai, paskui vėl būkite drauge, kad šėtonas negundytų jūsų nesusilaikymu.
5Msinyimane haki zenu, isipokuwa kama mnaafikiana kufanya hivyo kwa kitambo tu, ili mpate nafasi nzuri ya kusali. Kisha rudianeni tena mara, ili Shetani asije akawajaribu kwa sababu ya udhaifu wenu.
6Tai sakau leisdamas, o ne įsakydamas.
6Ninayowaambieni sasa ni mawaidha, si amri.
7Norėčiau, kad visi žmonės būtų tokie kaip aš. Bet kiekvienas turi iš Dievo savo dovaną, vienas tokią, kitas kitokią.
7Ningependa watu wote wawe kama mimi nilivyo; lakini kila mmoja anacho kipaji chake kutoka kwa Mungu; mmoja kipaji hiki na mwingine kile.
8Nesusituokusiems ir našlėms sakau: jie gerai darys, pasilikdami tokie kaip aš.
8Basi, wale ambao hawajaoana na wale walio wajane nawaambia kwamba ni vema kuendelea kuwa kama mimi nilivyo.
9Bet, jei negali susilaikyti, tegul tuokiasi. Geriau tuoktis negu degti.
9Hata hivyo, kama mtu hawezi kujizuia basi, na aoe; maana ni afadhali zaidi kuoa kuliko kuwaka tamaa.
10Susituokusiems įsakau ne aš, bet Viešpats, kad žmona nesiskirtų nuo vyro,
10Kwa wale waliooa ninayo amri, tena si yangu, ila ni ya Bwana: mke asiachane na mumewe;
11o jei atsiskirtų, kad liktų netekėjusi arba susitaikytų su vyru;­ taip pat ir vyras tenepalieka žmonos.
11lakini kama akiachana naye, basi abaki bila kuolewa; ama la, apatanishwe na mume wake. Mume naye asimpe talaka mkewe.
12Kitiems sakau aš, ne Viešpats: jei kuris brolis turi netikinčią žmoną ir ji sutinka gyventi su juo, tenesiskiria su ja.
12Kwa wale wengine, (mimi binafsi, si Bwana) nasema hivi: Ikiwa mwanamume Mkristo anaye mke asiyeamini, na huyo mwanamke akakubali kuendelea kuishi naye, asimpe talaka.
13Taip pat ir moteris, turinti netikintį vyrą, kuris sutinka su ja gyventi, tenesiskiria su juo.
13Na, kama mwanamke Mkristo anaye mume asiyeamini, na huyo mwanamume akakubali kuendelea kuishi naye, basi, asimpe talaka mumewe.
14Mat netikintis vyras pašventinamas žmona, o netikinti žmona pašventinama vyru. Kitaip jūsų vaikai būtų netyri, o dabar jie šventi.
14Kwa maana huyo mume asiyeamini hupokelewa kwa Mungu kwa kuungana na mkewe; na huyo mke asiyeamini hupokelewa kwa Mungu kwa kuungana na mumewe. Vinginevyo watoto wao wangekuwa si wa Mungu; kumbe sasa ni watoto wake Mungu.
15Bet, jei netikintis nori skirtis, tesiskiria. Tokiais atvejais brolis ar sesuo nėra surišti, nes Dievas mus pašaukė ramybei.
15Hata hivyo, ikiwa yule asiyeamini anataka kumwacha mwenzake aliye Mkristo, basi, na amwache tu. Hapo huyo Mkristo, mume au mke, atakuwa huru. Maana Mungu amewaiteni ninyi muishi kwa amani.
16Iš kur žinai, žmona, kad išgelbėsi vyrą? Arba iš kur tau žinoma, vyre, kad išgelbėsi žmoną?
16Wewe mama Mkristo, unawezaje kuwa na hakika kwamba hutaweza kumwokoa mume wako? Au wewe mume Mkristo, unawezaje kuwa na hakika kwamba hutaweza kumwokoa mkeo?
17Todėl, kaip Viešpats kuriam paskyrė, kokį Dievas kurį pašaukė, to jis ir toliau tesilaiko. Taip aš mokau visose bažnyčiose.
17Kwa vyovyote kila mmoja na aishi kufuatana na vipaji alivyogawiwa na Bwana, na kama alivyoitwa na Mungu. Hili ndilo agizo langu kwa makanisa yote.
18Jei kas buvo pašauktas apipjaustytas, tenesistengia nuslėpti apipjaustymo. Jei buvo pašauktas neapipjaustytas, tenedaro apipjaustymo.
18Kama mtu aliitwa akiwa ametahiriwa, basi asijisingizie kwamba hakutahiriwa; na kama alipoitwa hakuwa ametahiriwa, basi na asitahiriwe.
19Apipjaustymas yra niekas ir neapipjaustymas yra niekas, tik Dievo įsakymų laikymasis yra viskas.
19Maana kutahiriwa au kutotahiriwa si kitu; kilicho muhimu ni kuzishika amri za Mungu.
20Kiekvienas tepasilieka toks, koks buvo pašauktas.
20Basi, kila mmoja na abaki kama alivyokuwa wakati alipoitwa.
21Jei buvai pašauktas, būdamas vergas, nesijaudink dėl to, bet jei gali tapti laisvas, pasinaudok proga.
21Je, wewe ulikuwa mtumwa wakati ulipoitwa? Sawa, usijali; lakini ukipata fursa ya kuwa huru, itumie.
22Viešpatyje pašauktas vergas yra Jo išlaisvintas. Panašiai ir pašauktas laisvasis yra Kristaus vergas.
22Maana yeye aliyeitwa na Bwana akiwa mtumwa huyo huwa mtu huru wa Bwana. Hali kadhalika naye aliyeitwa akiwa mtu huru, huwa mtumwa wa Kristo.
23Jūs esate nupirkti už didelę kainą, todėl nepasidarykite žmonių vergais.
23Nyote mmenunuliwa kwa bei; kwa hiyo msiwe tena watumwa wa watu.
24Kiekvienas, broliai, kokie buvote pašaukti, tokie ir pasilikite prieš Dievą.
24Ndugu zangu, kila mmoja wenu basi, na abaki na Mungu kama alivyokuwa wakati alipoitwa.
25Dėl nesusituokusių neturiu Viešpaties įsakymo, bet duodu savo patarimą kaip tas, kuris iš Viešpaties gailestingumo vertas pasitikėjimo.
25Sasa, kuhusu mabikira na waseja, sina amri kutoka kwa Bwana; lakini natoa maoni yangu mimi ambaye kwa huruma yake Bwana nastahili kuaminiwa.
26Taigi manau, jog yra gerai, atsižvelgiant į šių laikų suspaudimus­gerai žmogui būti tokiam.
26Basi, kutokana na shida iliyopo sasa nadhani ingefaa mtu abaki kama alivyo.
27Jei esi susietas su žmona, neieškok skyrybų. Likai be žmonos­ neieškok žmonos.
27Je, umeoa? Basi, usitake kuachana na mkeo. Wewe hukuoa? Basi, usitake kuoa.
28Jei vedi, nenusidedi, ir jei mergina išteka, nenusideda. Tačiau šitokie žmonės turės kūno vargų, o aš norėčiau jus apsaugoti nuo jų.
28Lakini ikiwa utaoa hutakuwa umetenda dhambi; na msichana akiolewa hatakuwa ametenda dhambi. Hao watakaooana watapatwa na matatizo ya dunia hii, lakini mimi ningependa hayo yasiwapate ninyi.
29Sakau jums, broliai: laikas trumpas! Belieka tiems, kurie turi žmonas, gyventi, tarsi jų neturėtų,
29Ndugu, nataka kusema hivi: muda uliobaki ni mfupi. Na tangu sasa wale waliooa na waishi kama vile hawakuoa;
30ir kurie verkia, tarsi neverktų, ir kurie džiaugiasi, tarsi nesidžiaugtų, ir kurie perka, tarsi neįsigytų,
30wenye kulia wawe kama hawalii, na wenye kufurahi wawe kama hawafurahi; wanaonunua wawe kama hawana kitu;
31ir kurie naudojasi šiuo pasauliu,­tarsi nesinaudotų. Nes šio pasaulio pavidalas praeina.
31nao wenye shughuli na dunia hii wawe kama vile hawana shughuli sana nayo. Maana ulimwengu huu, kama tuujuavyo, unapita.
32Norėčiau, kad jūs gyventumėte be rūpesčių. Nesusituokęs rūpinasi Viešpaties reikalais­stengiasi patikti Viešpačiui.
32Ningependa ninyi msiwe na wasiwasi. Mtu asiye na mke hujishughulisha na kazi ya Bwana jinsi atakavyompendeza Bwana.
33O susituokęs rūpinasi pasaulio reikalais­stengiasi patikti žmonai.
33Mtu aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia jinsi atakavyompendeza mkewe,
34Yra skirtumas tarp žmonos ir mergaitės. Netekėjusi moteris rūpinasi Viešpaties reikalais, kad būtų šventa kūnu ir dvasia, o ištekėjusi rūpinasi pasaulio reikalais­kaip patikti vyrui.
34naye amegawanyika. Mwanamke asiyeolewa au bikira hujishughulisha na mambo ya Bwana apate kujitolea mwili na roho kwa Bwana. Lakini mwanamke aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii jinsi atakavyompendeza mumewe.
35Tai kalbu jūsų pačių labui, ne norėdamas užnerti jums kilpą, bet dėl to, kad tai yra tinkama ir kad jūs neblaškomi galėtumėte atsiduoti Viešpačiui.
35Nawaambieni haya kwa faida yenu, na si kwa kuwawekeeni kizuio. Nataka tu muwe na mpango unaofaa, mpate kumtumikia Bwana kwa moyo na nia moja.
36Jei kas mano būsiant jam negarbinga, kad jo mergaitė liks senmergė, ir jei taip reikia, tedaro kaip nori,­nenusidės,­tegul jie susituokia.
36Kama mtu anaona kwamba hamtendei vyema mchumba wake asipomwoa, na kama tamaa zake zinamshinda, na afanye atakavyo; waoane tu; hatakuwa ametenda dhambi.
37Bet jei kas savo širdyje yra tvirtai apsisprendęs, ne iš prievartos, bet būdamas savo valios šeimininkas, ir savo širdyje nutaręs išsaugoti savo mergaitę, tas gerai padarys.
37Lakini kama huyo mwanamume akiamua kwa hiari moyoni mwake kutooa na kama anaweza kuzitawala tamaa zake na kuamua namna ya kufanya, basi, anafanya vizuri zaidi asipomwoa huyo mwenzake bikira.
38Taigi, kas išleidžia savo mergaitę, gerai daro, o kas neišleidžia savo mergaitės, geriau daro.
38Kwa maneno mengine: yule anayeamua kumwoa huyo mchumba wake anafanya vema; naye anayeamua kutomwoa anafanya vema zaidi.
39Žmona surišta įstatymu, kol jos vyras gyvas. Vyrui mirus, ji laisva ir gali tekėti už ko nori, tik Viešpatyje.
39Mwanamke huwa amefungwa na mumewe kwa muda wote mumewe aishipo. Lakini mumewe akifa, mama huyo yuko huru, na akipenda anaweza kuolewa na mtu yeyote, mradi tu iwe Kikristo.
40Bet, mano nuomone, ji bus laimingesnė netekėdama. Manau, kad ir aš turiu Dievo Dvasią.
40Lakini, nionavyo mimi, atakuwa na heri zaidi kama akibaki hivyo alivyo. Hayo ni maoni yangu, na nafikiri mimi pia ninaye Roho wa Mungu.