Lithuanian

Swahili: New Testament

1 Corinthians

9

1Ar aš ne apaštalas? Ar aš ne laisvas? Ar nesu regėjęs Jėzaus Kristaus, mūsų Viešpaties? Ar jūs ne mano darbo vaisius Viešpatyje?
1Je, mimi si mtu huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sikumwona Yesu Bwana wetu? Je, ninyi si matokeo ya kazi yangu kwa ajili ya Bwana?
2Jei kitiems ir nesu apaštalas, tai jums, be abejo, esu, nes mano apaštalystės antspaudas esate jūs Viešpatyje.
2Hata kama kwa watu wengine mimi si mtume, lakini walau kwenu ninyi mimi ni mtume. Ninyi ni uthibitisho wa mtume wangu kwa sababu ya kuungana kwenu na Bwana.
3Štai mano pasiteisinimas prieš tuos, kurie mane kaltina.
3Hoja yangu kwa wale wanaonipinga ndiyo hii:
4Argi mes neturime teisės valgyti ir gerti?
4Je, hatuna haki ya kula na kunywa?
5Ar neturime teisės vaikščioti kartu su seserimi, žmona, kaip kiti apaštalai ir Viešpaties broliai bei Kefas?
5Je, hatuna ruhusa kumchukua mke Mkristo katika ziara zetu, kama vile wafanyavyo mitume wengine, ndugu zake Bwana, na pia Kefa?
6O gal tik aš ir Barnabas neturime teisės nedirbti?
6Au ni mimi tu na Barnaba ambao tunapaswa kujipatia maslahi yetu kwa kufanya kazi?
7Kas gi tarnauja kariuomenėje už savo paties pinigus? Kas sodina vynuogyną ir nevalgo jo vaisių? Arba kas gano bandą ir negeria bandos pieno?
7Je, mwanajeshi gani anayelipia utumishi wake jeshini? Mkulima gani asiyekula matunda ya shamba lake la mizabibu? Mchungaji gani asiyekunywa maziwa ya mifugo yake?
8Ar aš tai sakau vien kaip žmogus? Argi to paties nesako ir Įstatymas?
8Je, nasema mambo haya kibinadamu tu? Je, Sheria nayo haisemi hivyo?
9Mozės Įstatyme parašyta: “Neužrišk nasrų kuliančiam jaučiui!” Bet ar Dievui terūpi jaučiai?
9Imeandikwa katika Sheria ya Mose: "Usimfunge kinywa ng'ombe anapoliwata nafaka." Je, ndio kusema Mungu anajishughulisha na ng'ombe?
10O gal Jis iš tiesų taiko tai mums? Juk dėl mūsų parašyta, kad artojas artų su viltimi ir kūlėjas kultų su viltimi, jog gaus savo dalį.
10Je, hakuwa anatufikiria sisi aliposema hivyo? Naam, haya yaliandikwa kwa ajili yetu; kwani yule anayelima na yule anayevuna, wote wawili wana haki ya kutumaini kupata sehemu ya mavuno.
11Jei mes jums pasėjome dvasinių gėrybių, tai ar didelis dalykas, kad pjausime pas jus medžiaginių?
11Ikiwa sisi tumepanda mbegu ya kiroho kati yenu, je, ni jambo kubwa tukichuma kwenu faida ya kidunia?
12Jei kiti turi teisių į jus, tai ar ne juo labiau mes? Vis dėlto mes nesinaudojome savo teise, bet viską pakeliame, kad tik Kristaus Evangelijai nedarytume kliūčių.
12Ikiwa wengine wanayo haki ya kutazamia hayo kutoka kwenu, je, sisi hatuna haki zaidi kuliko hao? Lakini, sisi hatukuitumia haki hiyo, Badala yake, tumestahimili kila kitu ili tusiiwekee kizuizi chochote Habari Njema ya Kristo.
13Ar nežinote, kad tie, kurie tarnauja šventykloje, valgo iš šventyklos pajamų ir kad aukuro tarnai gauna dalį aukų?
13Je, hamjui kwamba wanaotumikia Hekaluni hupata chakula chao Hekaluni, na kwamba wanaotolea sadaka madhabahuni hupata sehemu ya hiyo sadaka?
14Taip ir Viešpats patvarkė, kad Evangelijos skelbėjai gyventų iš Evangelijos.
14Bwana aliagiza vivyo hivyo; wahubiri wa Habari Njema wapate riziki zao kutokana nayo.
15Bet aš nesinaudojau šiomis teisėmis. Ir tai rašau ne tam, kad sau pritaikyčiau. Man geriau mirti, negu leisti, kad kas atimtų iš manęs šį pasigyrimą.
15Lakini, mimi sikutumia hata mojawapo ya haki hizo. Na wala siandiki nijipatie haki hizo; kwangu mimi ni afadhali kufa kuliko kumfanya yeyote aone kwamba najisifu bure.
16Jeigu skelbiu Evangeliją, neturiu pagrindo girtis, nes tai mano būtina pareiga, ir vargas man, jei Evangelijos neskelbčiau!
16Ikiwa ninaihubiri Habari Njema, hilo si jambo la kujivunia; hilo ni jukumu nililopewa. Na, ole wangu kama sitaihubiri Habari Njema!
17Jeigu tai darau savo valia, turiu atlygį; bet jei darau ne savo valia, tai atlieku man patikėtą tarnavimą.
17Ningekuwa nimeichagua kazi hii kwa hiari, basi, ningetazamia malipo; lakini maadam naifanya ikiwa ni wajibu, hiyo ina maana kwamba ni jukumu nililopewa nitekeleze.
18Koks tada mano atlygis? Ogi kad, skelbdamas Kristaus Evangeliją, pateikiu ją veltui ir nesinaudoju savo teise, kurią man duoda Evangelijos skelbimas.
18Mshahara wangu ni kitu gani, basi? Mshahara wangu ni fursa ya kuihubiri Habari Njema bure, bila kudai haki ninazostahili kwa kuihubiri.
19Būdamas nuo nieko nepriklausomas, pasidariau visų vergas, kad tik daugiau jų laimėčiau.
19Kwa hiyo, ingawa mimi si mtumwa wa mtu yeyote, nimejifanya mtumwa wa kila mtu ili nimpatie Kristo watu wengi iwezekanavyo.
20Žydams buvau kaip žydas, kad laimėčiau žydus. Tiems, kurie laikosi įstatymo, tapau besilaikančiu įstatymo, kad laimėčiau besilaikančius įstatymo, nors pats nesu jam pavaldus.
20Kwa Wayahudi nimeishi kama Myahudi ili niwapate Wayahudi; yaani, ingawa mimi siko chini ya Sheria, nimejiweka chini ya Sheria kwao, ili niwapate hao walio chini ya Sheria.
21Tiems, kurie neturi įstatymo, buvau kaip neturintis įstatymo,­ pats būdamas ne be Dievo įstatymo, bet surištas Kristaus įstatymu,­kad laimėčiau tuos, kurie neturi įstatymo.
21Na kwa wale walio nje ya Sheria, naishi kama wao, nje ya Sheria, ili niwapate hao walio nje ya Sheria. Hii haimaanishi kwamba mimi niko nje ya sheria ya Mungu, maana nabanwa na sheria ya Kristo.
22Silpniesiems pasidariau kaip silpnas, kad laimėčiau silpnuosius. Visiems tapau viskuo, kad vienaip ar kitaip kai kuriuos išgelbėčiau.
22Kwao walio dhaifu nimejifanya dhaifu ili niwapate hao walio dhaifu. Nimejifanya kila kitu kwa wote ili nipate kuwaokoa baadhi yao kwa kila njia.
23Visa tai darau dėl Evangelijos, kad būčiau jos dalininkas.
23Nafanya haya yote kwa ajili ya Habari Njema, nipate kushiriki baraka zake.
24Argi nežinote, kad lenktynėse bėga visi, bet tik vienas gauna laimėtojo apdovanojimą? Taigi bėkite taip, kad laimėtumėte!
24Je, hamjui kwamba katika uwanja wa michezo, ingawa wapiga mbio wote hukimbia, ni mmoja tu anayejinyakulia zawadi?
25Kiekvienas varžybų dalyvis nuo visko susilaiko; jie taip daro, norėdami gauti vystantį vainiką, o mes­nevystantį.
25Wanariadha hujipa mazoezi na nidhamu kali; hufanya hivyo ili wajipatie taji iharibikayo! Lakini sisi twafanya hivyo tupate taji ya kudumu daima.
26Todėl aš bėgu nedvejodamas ir grumiuosi ne kaip į orą smūgiuodamas,
26Ndivyo basi, ninavyopiga mbio nikiwa na nia ya kushinda; ndivyo ninavyopigana, na si kama bondia anayetupa ngumi zake hewani.
27bet tramdau savo kūną ir darau jį klusnų, kad, kitiems skelbdamas, pats netapčiau atmestinas.
27Naupa mwili wangu mazoezi magumu na kuutia katika nidhamu kamili, nisije mimi mwenyewe nikakataliwa baada ya kuwahubiria wengine.