Lithuanian

Swahili: New Testament

1 Corinthians

10

1Aš nenoriu, kad liktumėte nežinioje, broliai,­visi mūsų tėvai buvo po debesim ir visi perėjo jūrą.
1Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
2Ir visi buvo pakrikštyti į Mozę, debesyje ir jūroje;
2Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
3visi valgė tą patį dvasinį maistą
3Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
4ir visi gėrė tą patį dvasinį gėrimą. Jie gėrė iš dvasinės juos lydinčios uolos, o ta uola buvo Kristus.
4wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
5Vis dėlto daugumas iš jų nepatiko Dievui, ir “jų kūnai liko gulėti dykumoje”.
5Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
6Tie įvykiai yra mums pavyzdžiai, kad negeistume blogio, kaip anie geidė.
6Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
7Nebūkite stabmeldžiai, kaip kai kurie iš jų,­kaip parašyta: “Tauta sėdosi valgyti ir gerti ir kėlėsi žaisti”.
7Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: "Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza."
8Neištvirkaukime, kaip kai kurie iš jų ištvirkavo ir žuvo vieną dieną dvidešimt trys tūkstančiai.
8Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
9Negundykime Kristaus, kaip kai kurie iš jų gundė ir mirė nuo gyvačių.
9Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
10Nemurmėkite, kaip kai kurie iš jų murmėjo ir žuvo nuo naikintojo.
10Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
11Visa tai jiems atsitiko kaip pavyzdžiai, ir užrašyti pamokyti mums, gyvenantiems amžių pabaigoje.
11Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili.
12Todėl, kas tariasi stovįs, težiūri, kad nekristų.
12Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
13Jums tekęs pagundymas tėra tik žmogiškas. Bet Dievas ištikimas. Jis neleis jūsų gundyti daugiau nei jūsų jėgos leidžia, bet kartu su pagundymu duos ir išeitį, kad sugebėtumėte jį atlaikyti.
13Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
14Todėl, mano mylimieji, bėkite nuo stabmeldystės!
14Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
15Kalbu kaip išmintingiems; apsvarstykite patys, ką sakau.
15Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
16Argi laiminimo taurė, kurią laiminame, nėra bendravimas Kristaus kraujyje? Argi duona, kurią laužome, nėra bendravimas Kristaus kūne?
16Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
17Nors mūsų daug, mes visi esame viena duona ir vienas kūnas: juk mes visi dalijamės viena duona.
17Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
18Pažiūrėkite į Izraelį pagal kūną: argi tie, kurie valgo aukas, nėra aukuro bendrininkai?
18Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
19Ką gi sakau? Ar stabas ką nors reiškia? Ar ką nors reiškia auka stabams?
19Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
20Ne, bet pagonys, aukodami aukas, aukoja demonams, o ne Dievui. Ir aš nenoriu, kad jūs būtumėte demonų bendrininkai.
20Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
21Jūs negalite gerti Viešpaties taurės ir demonų taurės. Negalite sėdėti prie Viešpaties stalo ir prie demonų stalo.
21Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
22Nejaugi kurstysime Viešpaties pavydą? Ar mes už Jį stipresni?
22Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
23Viskas man leistina, bet ne viskas naudinga. Viskas man leistina, bet ne viskas ugdo!
23Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
24Niekas teneieško, kaip jam geriau, bet kaip kitam.
24Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
25Valgykite visa, kas parduodama mėsos prekyvietėje, sąžinės labui nieko neklausinėdami.
25Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
26Juk “Viešpaties yra žemė ir visa, ko ji pilna”.
26maana Maandiko yasema: "Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana."
27Jeigu jus pasikviečia netikintis žmogus ir jūs norite jį aplankyti, valgykite visa, kas jums padedama, sąžinės labui nieko neklausinėdami.
27Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
28Bet jei kas jums pasakytų: “Tai auka stabams”, tada nevalgykite dėl žmogaus, kuris tai pasakė, ir dėl sąžinės,­juk “Viešpaties yra žemė ir visa, ko ji pilna”.
28Lakini mtu akiwaambieni: "Chakula hiki kimetambikiwa sanamu," basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
29Čia aš kalbu ne apie tavo paties sąžinę, bet apie kito sąžinę. Kodėl gi mano laisvė turėtų būti teisiama kitos sąžinės?
29Nasema, "kwa ajili ya dhamiri," si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: "Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
30Jeigu aš dėkodamas valgau, kodėl man priekaištaujama dėl maisto, už kurį dėkoju?
30Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?"
31Todėl ar valgote, ar geriate, ar šiaip ką darote, visa darykite Dievo šlovei.
31Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
32Nepiktinkite nei žydų, nei graikų, nei Dievo bažnyčios,
32Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
33kaip ir aš stengiuosi visiems viskuo patikti, neieškodamas sau naudos, bet to, kas naudinga daugeliui, kad jie būtų išgelbėti.
33Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.