1Sekite manimi, kaip ir aš seku Kristumi.
1Niigeni mimi kama ninavyomwiga Kristo.
2Aš jus giriu, kad visame kame prisimenate mane ir laikotės nurodymų, kuriuos jums daviau.
2Nawapeni hongera kwa sababu mnanikumbuka na kwa sababu mnayashikilia yale maagizo niliyowapeni.
3Noriu, kad žinotumėte, jog kiekvieno vyro galva yra Kristus, moters galvavyras, o Kristaus galvaDievas.
3Lakini napenda pia mjue kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, na mwanamume ni kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo.
4Kiekvienas vyras, kuris meldžiasi ar pranašauja apdengta galva, paniekina savo galvą.
4Basi, kila mwanamume anayesali au anayetangaza ujumbe wa Mungu huku amefunika kichwa chake, huyo anamdharau Kristo.
5Ir kiekviena moteris, kuri meldžiasi ar pranašauja neapdengta galva, paniekina savo galvą: tai tas pats, kaip būti nuskustai.
5Na mwanamke akisali au kutangaza ujumbe wa Mungu bila kufunika kichwa chake, anamdharau mumewe; anayefanya hivyo ni sawa tu na mwanamke aliyenyoa kichwa chake.
6Jei moteris neapsigaubia, tai tegul ir nusikerpa! O jei moteriai gėda nusikirpti ar nusiskusti plaukus, teapsigaubia.
6Mwanamke asiyefunika kichwa chake, afadhali anyoe nywele zake. Lakini ni aibu kwa mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa; basi, afadhali afunike kichwa chake.
7Vyrui nereikia gaubti galvos, nes jis yra Dievo atvaizdas ir šlovė. O moteris yra vyro šlovė.
7Haifai mwanamume kufunika kichwa chake, kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na kioo cha utukufu wake Mungu; lakini mwanamke ni kioo cha utukufu wa mwanamume.
8Juk ne vyras iš moters, bet moteris iš vyro,
8Mwanamume hakutoka kwa mwanamke, ila mwanamke alitoka kwa mwanamume.
9taip pat ne vyras buvo sukurtas moteriai, o moteris vyrui.
9Mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, ila mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanamume.
10Todėl moteris privalo turėti ant galvos pavaldumo ženklą dėl angelų.
10Ndiyo maana mwanamke hufunika kichwa chake, iwe ishara ya mamlaka yaliyo juu yake, na pia kwa sababu ya malaika.
11Bet Viešpatyje nei vyras be moters, nei moteris be vyro.
11Hata hivyo, mbele ya Bwana mwanamke si kitu bila mwanamume, naye mwanamume si kitu bila mwanamke.
12Kaip moteris iš vyro, taip vyras per moterį, bet visaiš Dievo.
12Kama vile mwanamke alivyotokana na mwanamume, vivyo hivyo mwanamume huzaliwa na mwanamke; kila kitu hutoka kwa Mungu.
13Spręskite patys: argi tinka moteriai melstis Dievui neapsigaubusiai?
13Amueni wenyewe: Je, inafaa mwanamke kumwomba Mungu bila kuvaa kitu kichwani?
14Argi pati prigimtis jūsų nemoko, jog vyrui gėda nešioti ilgus plaukus?
14Hata maumbile yenyewe huonyesha wazi kwamba kwa mwanamume kuwa na nywele ndefu ni aibu kwake mwenyewe;
15Tuo tarpu moteriai garbė turėti ilgus plaukus. Nes plaukai jai duoti kaip dangalas.
15lakini kwa mwanamke kuwa na nywele ni heshima kwake; nywele zake ndefu amepewa ili zimfunike.
16Bet jei kas norėtų ginčytis,težino, jog nei mes, nei Dievo bažnyčios neturime tokio papročio.
16Kama mtu anataka kuleta ubishi juu ya jambo hili, basi, na ajue kwamba sisi hatuna desturi nyingine, wala makanisa ya Mungu hayana desturi nyingine.
17Duodamas šiuos nurodymus, aš jūsų negiriu, nes jūsų susirinkimai išeina ne į gera, bet į bloga.
17Nikiwa bado nawapeni maagizo haya, siwezi hata kidogo kuwapa ninyi hongera kuhusu haya yafuatayo: mikutano yenu ninyi waumini yaleta hasara zaidi kuliko faida.
18Pirmiausia man teko girdėti, kad, kai jūs susirenkate bažnyčioje, tarp jūsų būna susiskaldymų, ir iš dalies aš tuo tikiu.
18Awali ya yote, nasikia kwamba mnapokutana pamoja hutokea mafarakano kati yenu. Nami naamini kiasi,
19Juk pas jus turi būti atskalų, kad išaiškėtų tie, kurie yra patikimi.
19maana ni lazima fikira tofauti ziweko miongoni mwenu, ili wale walio thabiti wapate kutambulikana.
20Jūs susirenkate kartu, bet ne Viešpaties vakarienės valgyti,
20Kweli mnakutana, lakini si kwa ajili ya kula chakula cha Bwana!
21nes kiekvienas paskuba suvalgyti savo maistą, ir vienas lieka alkanas, o kitas nusigeria.
21Maana mnapokula kila mmoja hukikalia chakula chake mwenyewe, hata hutokea kwamba baadhi yenu wana njaa, na wengine wamelewa!
22Argi neturite savo namų valgyti ir gerti? O gal norite paniekinti Dievo bažnyčią ir sugėdinti stokojančius? Kas man belieka sakyti? Pagirti? Ne! Už tai nepagirsiu.
22Je, hamwezi kula na kunywa nyumbani kwenu! Au je, mnalidharau kanisa la Mungu na kuwaaibisha hao wasio na kitu? Niwaambie nini? Niwasifu? La hasha! Si kuhusu jambo hili.
23Aš tai gavau iš Viešpaties ir perdaviau jums, kad Viešpats Jėzus tą naktį, kurią buvo išduotas, paėmė duoną
23Maana mimi nilipokea kwa Bwana yale maagizo niliyowaachieni: kwamba, usiku ule Bwana Yesu aliotolewa, alitwaa mkate,
24ir padėkojęs sulaužė ir tarė: “Imkite ir valgykite; tai yra mano kūnas, kuris už jus sulaužomas. Tai darykite mano atminimui”.
24akamshukuru Mungu, akaumega, akasema: "Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
25Taip pat po vakarienės jis paėmė taurę ir tarė: “Ši taurė yra Naujoji Sandora mano kraujyje. Kiek kartų gersite, darykite tai mano atminimui”.
25Vivyo hivyo, baada ya kula, akatwaa kikombe akasema: "Hiki ni kikombe cha agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu. Fanyeni hivi, kila mnapokunywa, kwa kunikumbuka."
26Taigi, kada tik valgote šitą duoną ir geriate šitą taurę, jūs skelbiate Viešpaties mirtį, kol Jis ateis.
26Maana kila mnapokula mkate huu na kunywa kikombe hiki, mwatangaza kifo cha Bwana, mpaka atakapokuja.
27Todėl kas nevertai valgo tos duonos ir geria iš Viešpaties taurės, tas bus kaltas prieš Viešpaties kūną ir kraują.
27Kwa hiyo, kila aulaye mkate huo au kunywa kikombe cha Bwana bila kustahili, atakuwa na hatia dhidi ya mwili na damu ya Bwana.
28Teištiria žmogus pats save ir tada tevalgo tos duonos ir tegeria iš tos taurės.
28Basi, kila mtu ajichunguze mwenyewe kwanza, ndipo ale mkate huo na anywe kikombe hicho;
29Nes kas valgo ir geria nevertai, Viešpaties kūno neišskirdamas, tas valgo ir geria sau pasmerkimą.
29maana anayekula na kunywa bila kutambua maana ya mwili wa Bwana, anakula na kunywa hukumu yake yeye mwenyewe.
30Todėl tarp jūsų daug silpnų bei ligotų ir daug užmigusių.
30Ndiyo maana wengi kati yenu ni dhaifu na wagonjwa, na wengine kadhaa wamekufa.
31Jei mes patys save teistume, nebūtume teisiami.
31Kama tungejichunguza wenyewe vizuri hatungeadhibiwa hivyo.
32Bet kai Viešpats mus teisia, tai ir sudraudžia, kad nebūtume pasmerkti kartu su pasauliu.
32Lakini tunapohukumiwa na Bwana, tunafunzwa tuwe na nidhamu, ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
33Todėl, mano broliai, kai susirenkate valgyti, palaukite vieni kitų.
33Kwa hiyo, ndugu zangu, mnapokutana kula chakula cha Bwana, kila mmoja amngoje mwenzake.
34O jeigu kas išalkęs, tepavalgo namie, kad nesirinktumėte pasmerkimui. Kitus reikalus sutvarkysiu atvykęs.
34Na kama kuna yeyote aliye na njaa, na ale nyumbani kwake, ili kukutana kwenu kusisababishe hukumu. Lakini, kuhusu yale mambo mengine, nitawapeni maelezo nitakapokuja.