1Aš nenoriu, broliai, kad jūs neišmanytumėte apie dvasines dovanas.
1Ndugu, kuhusu vipaji vya kiroho, napenda mfahamu vizuri mambo haya:
2Jūs žinote, kad, kai buvote pagonys, ėjote prie nebylių stabų kaip vedami.
2Mnajua kwamba, kabla ya kuongoka kwenu, mlitawaliwa na kupotoshwa na sanamu tupu.
3Todėl aš jums aiškinu, kad nė vienas, kuris kalba Dievo Dvasia, neprakeikia Jėzaus. Ir nė vienas negali sakyti, kad Jėzus yra Viešpats, kaip tik Šventąja Dvasia.
3Basi, jueni kwamba mtu yeyote anayeongozwa na Roho wa Mungu hawezi kusema: "Yesu alaaniwe!" Hali kadhalika, mtu yeyote hawezi kusema: "Yesu ni Bwana," asipoongozwa na Roho Mtakatifu.
4Yra skirtingų dovanų, tačiau ta pati Dvasia.
4Vipaji vya kiroho ni vya namna nyingi, lakini Roho avitoaye ni mmoja.
5Yra skirtingų tarnavimų, tačiau tas pats Viešpats.
5Kuna namna nyingi za kutumikia, lakini Bwana anayetumikiwa ni mmoja.
6Ir yra skirtingi veiksmai, tačiau tas pats Dievas, kuris visa veikia visame kame.
6Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.
7Bet kiekvienam suteikiamas Dvasios pasireiškimas bendram labui.
7Kila mtu hupewa mwangaza wa Roho kwa faida ya wote.
8Vienam Dvasia suteikiamas išminties žodis, kitam ta pačia Dvasiapažinimo žodis,
8Roho humpa mmoja ujumbe wa hekima, na mwingine ujumbe wa elimu apendavyo Roho huyohuyo.
9kitamtikėjimas ta pačia Dvasia, kitamišgydymų dovanos ta pačia Dvasia,
9Roho huyohuyo humpa mmoja imani, na humpa mwingine kipaji cha kuponya;
10kitamstebuklų darymas, kitampranašavimas, kitamdvasių atpažinimas, kitamskirtingos kalbos, kitamkalbų aiškinimas.
10humpa mmoja kipaji cha kufanya miujiza, mwingine kipaji cha kusema ujumbe wa Mungu, mwingine kipaji cha kubainisha vipaji vitokavyo kwa Roho na visivyo vya Roho; humpa mmoja kipaji cha kusema lugha ngeni, na mwingine kipaji cha kuzifafanua.
11Bet visa tai daro viena ir ta pati Dvasia, kuri dalija kiekvienam atskirai, kaip Jai patinka.
11Hizo zote ni kazi za Roho huyohuyo mmoja, ambaye humpa kila mtu kipaji tofauti, kama apendavyo mwenyewe.
12Nes kaip kūnas yra vienas ir turi daug narių, o visi to vieno kūno nariai, nepaisant daugumo, sudaro vieną kūną, taip ir Kristus.
12Kama vile mwili ulivyo mmoja wenye viungo vingi, na viungo hivyo vyote--ingawaje ni vingi--hufanya mwili mmoja, ndivyo ilivyo pia kwa Kristo.
13Nes viena Dvasia mes visi esame pakrikštyti į vieną kūną,žydai ar graikai, vergai ar laisvieji; ir visi buvome pagirdyti viena Dvasia.
13Maana sisi, tukiwa Wayahudi au watu wa mataifa mengine, watumwa au watu huru, sote tumebatizwa kwa Roho mmoja katika mwili huo mmoja; na sote tukanyweshwa Roho huyo mmoja.
14Juk kūnas nėra sudėtas iš vieno nario, bet iš daugelio.
14Mwili hauna kiungo kimoja tu, bali una viungo vingi.
15Jei koja sakytų: “Kadangi nesu ranka, todėl nepriklausau kūnui”, argi dėl to ji nepriklausytų kūnui?
15Kama mguu ungejisemea: "Kwa kuwa mimi si mkono, basi mimi si mali ya mwili", je, ungekoma kuwa sehemu ya mwili? La hasha!
16O jeigu ausis sakytų: “Kadangi nesu akis, todėl nepriklausau kūnui”, argi dėl to ji nepriklausytų kūnui?
16Kama sikio lingejisemea: "Kwa vile mimi si jicho, basi mimi si mali ya mwili", je, kwa hoja hiyo lingekoma kuwa sehemu ya mwili? La!
17Jeigu visas kūnas būtų akis, tai kur būtų klausa? Jeigu visas kūnas būtų klausa, tai kur būtų uoslė?
17Kama mwili wote ungekuwa jicho, sikio lingekuwa wapi? Na kama mwili wote ungekuwa sikio, mtu angewezaje kunusa?
18Bet dabar Dievas sudėliojo kūne narius ir kiekvieną iš jų, kaip panorėjo.
18Lakini kama ilivyo, Mungu alizipanga sehemu hizo tofauti katika mwili kama alivyopenda.
19Ir jei visi būtų vienas narys, kur beliktų kūnas?
19Kama sehemu zote zingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20Bet dabar narių daug, o kūnas vienas.
20Ukweli ni kwamba, sehemu za mwili ni nyingi, lakini mwili ni mmoja.
21Akis negali pasakyti rankai: “Man tavęs nereikia”, ar galva kojoms: “Man jūsų nereikia”.
21Basi, jicho haliwezi kuuambia mkono: "Sikuhitaji wewe", wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: "Siwahitaji ninyi."
22Priešingai, tie kūno nariai, kurie atrodo silpnesni, yra būtini.
22Zaidi ya hayo, inaonekana kwamba sehemu zile za mwili zinazoonekana kuwa ni dhaifu ndizo zilizo muhimu zaidi.
23Tuos kūno narius, kuriuos laikome mažiau garbingais, mes apsupame didesne pagarba, ir mūsų gėdingi nariai gaubiami didesnio padorumo,
23Tena, viungo vile tunavyovifikiria kuwa havistahili heshima kubwa, ndivyo tunavyovitunza kwa uangalifu zaidi; viungo vya mwili ambavyo havionekani kuwa vizuri sana, huhifadhiwa zaidi,
24kurio nereikia mūsų padoriesiems nariams. Taigi, tvarkydamas kūną, Dievas skyrė daugiau pagarbos tiems kūno nariams, kurie jos stokojo,
24ambapo viungo vingine havihitaji kushughulikiwa. Mungu mwenyewe ameuweka mwili katika mpango, akakipa heshima zaidi kiungo kile kilichopungukiwa heshima,
25kad kūne nebūtų susiskaldymų, bet patys nariai rūpintųsi vieni kitais.
25ili kusiweko na utengano katika mwili bali viungo vyote vishughulikiane.
26Todėl, jei kenčia vienas narys, su juo kenčia ir visi nariai. Ir jei kuris narys pagerbiamas, su juo džiaugiasi visi nariai.
26Kama kiungo kimoja kinaumia viungo vyote huumia pamoja nacho. Kiungo kimoja kikisifiwa viungo vingine vyote hufurahi pamoja nacho.
27Jūs esate Kristaus kūnas, o pavieniuinariai.
27Basi, ninyi nyote ni mwili wa Kristo; kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.
28Ir šiuos Dievas paskyrė bažnyčioje: pirmaapaštalais, antrapranašais, trečiamokytojais; po to stebuklai, paskuiišgydymų dovanos, visokia pagalba, vadovavimai, įvairios kalbos.
28Mungu ameweka katika kanisa: kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu; kisha ameweka wale wenye kipaji cha kufanya miujiza, kuponya, kusaidia; viongozi na wenye kusema lugha ngeni.
29Ar visi apaštalai? Ar visi pranašai? Ar visi mokytojai? Ar visi stebukladariai?
29Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni walimu? Wote ni wenye kipaji cha kufanya miujiza?
30Ar visi turi išgydymų dovanas? Ar visi kalba kalbomis? Ar visi aiškina?
30Je, wote ni wenye kipaji cha kuponya? Wote ni wenye kipaji cha kusema lugha ngeni? Je, wote hufafanua lugha?
31Taigi karštai trokškite aukštesniųjų dovanų! Ir visgi rodau jums dar pranašesnį kelią.
31Muwe basi, na tamaa ya kupata vipaji muhimu zaidi. Nami sasa nitawaonyesheni njia bora zaidi kuliko hizi zote.