Lithuanian

Swahili: New Testament

1 John

2

1Mano vaikeliai, rašau jums tai, kad nenusidėtumėte. O jei kuris nusidėtų, tai mes turime Užtarėją pas Tėvą, teisųjį Jėzų Kristų.
1Watoto wangu, ninawaandikieni mambo haya, kusudi msitende dhambi. Lakini, ikijatokea mtu akatenda dhambi, tunaye mmoja ambaye hutuombea kwa Baba, ndiye Yesu Kristo aliye mwadilifu kabisa.
2Jis yra permaldavimas už mūsų nuodėmes, ir ne tik už mūsų, bet ir už viso pasaulio.
2Kristo ndiye sadaka iondoayo dhambi zetu; wala si dhambi zetu sisi tu, bali pia dhambi za ulimwengu wote.
3Iš to mes patiriame, kad Jį pažįstame, jei laikomės Jo įsakymų.
3Tukizitii amri za Mungu, basi, tunaweza kuwa na hakika kwamba tunamjua.
4Kas sako: “Aš Jį pažįstu”, bet Jo įsakymų nesilaiko, tas melagis, ir nėra jame tiesos.
4Mtu akisema kwamba anamjua, lakini hazitii amri zake, basi mtu huyo ni mwongo, na ukweli haumo ndani yake.
5O kas laikosi Jo žodžių, tame iš tiesų Dievo meilė tobula tapo. Iš to ir pažįstame, jog Jame esame.
5Lakini mtu yeyote anayeshika neno la Mungu, huyo ndiye aliye na upendo kamili wa Mungu ndani yake. Hivi ndivyo tunavyoweza kuwa na hakika kwamba tunaungana naye:
6Kas sako esąs Jame, tas turi pats taip elgtis, kaip ir Jis elgėsi.
6mtu yeyote anayesema kwamba ameungana na Mungu, anapaswa kuishi kama alivyoishi Yesu Kristo.
7Broliai, aš jums nerašau naujo įsakymo, bet seną įsakymą, kurį turėjote nuo pradžios. Senas įsakymas yra žodis, kurį girdėjote nuo pradžios.
7Wapenzi wangu, amri hii ninayowaandikieni si amri mpya; ni amri ileile ya zamani mliyokuwa nayo tangu mwanzo. Amri hiyo ya zamani ni ule ujumbe mliousikia.
8Ir vis dėlto rašau jums naują įsakymą, kuris tikras Jame ir jumyse, nes tamsa traukiasi, o tikroji šviesa jau šviečia.
8Hata hivyo, amri hii ninayowaandikieni ni amri mpya, na ukweli wake unaonekana ndani ya Kristo na ndani yenu pia. Maana giza linatoweka, na mwanga wa ukweli umekwisha anza kuangaza.
9Kas sakosi esąs šviesoje, o savo brolio nekenčia, tas dar tebėra tamsoje.
9Yeyote asemaye kwamba yumo katika mwanga, lakini anamchukia ndugu yake, mtu huyo bado yumo gizani.
10Kas myli savo brolį, tas pasilieka šviesoje, ir jame nėra nieko piktinančio.
10Yeyote ampendaye ndugu yake, yuko katika mwanga, na hamna chochote ndani yake kiwezacho kumkwaza mtu mwingine.
11O kas savo brolio nekenčia, tas yra tamsoje, vaikščioja tamsoje ir nežino, kur einąs, nes tamsa užgulė jam akis.
11Lakini anayemchukia ndugu yake, yumo gizani; anatembea gizani, na hajui anakokwenda, maana giza limempofusha.
12Rašau jums, vaikeliai, nes dėl Jo vardo atleistos jums nuodėmės.
12Ninawaandikieni ninyi watoto, kwa kuwa dhambi zenu zimeondolewa kwa jina la Kristo.
13Rašau jums, tėvai, nes pažinote Tą, kuris yra nuo pradžios. Ir jums, jaunuoliai, rašau, nes nugalėjote piktąjį. Rašau jums, vaikeliai, nes pažinote Tėvą.
13Nawaandikieni ninyi kina baba kwani mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo, Nawaandikieni ninyi vijana kwa sababu mmemshinda yule Mwovu.
14Parašiau jums, tėvai, nes pažinote Tą, kuris yra nuo pradžios. Parašiau jums, jaunuoliai, nes jūs stiprūs ir jumyse laikosi Dievo žodis, ir jūs nugalėjote piktąjį.
14Nawaandikieni ninyi watoto, kwa sababu mnamjua Baba. Nawaandikieni ninyi kina baba, kwa kuwa mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo. Nawaandikieni ninyi vijana kwa sababu mna nguvu; neno la Mungu limo ndani yenu na mmemshinda yule Mwovu.
15Nemylėkite pasaulio, nei to, kas yra pasaulyje. Jei kas myli pasaulį, nėra jame Tėvo meilės,
15Msiupende ulimwengu, wala chochote kilicho cha ulimwengu. Mtu anayeupenda ulimwengu, upendo wa Baba hauwezi kuwamo ndani yake.
16nes visa, kas pasaulyje, tai kūno geismas, akių geismas ir gyvenimo išdidumas, o tai nėra iš Tėvo, bet iš pasaulio.
16Vitu vyote vya ulimwengu-tamaa mbaya za mwili, vitu wanavyoviona watu na kuvitamani, majivuno yasababishwayo na mali-vyote hivyo havitoki kwa Baba, bali vyatoka kwa ulimwengu.
17Praeina pasaulis ir jo geismai, bet kas vykdo Dievo valią, tas išlieka per amžius.
17Ulimwengu pamoja na vitu vyake vyote vyenye kutamanika unapita; lakini mtu atendaye atakalo Mungu, anaishi milele.
18Vaikeliai, tai paskutinė valanda. Kaip esate girdėję, kad ateis antikristas, tai jau dabar pasirodė daug antikristų. Iš to sprendžiame, jog tai paskutinė valanda.
18Watoto, mwisho u karibu! Mlikwisha sikia kwamba adui wa Kristo anakuja, na sasa adui wengi wa Kristo wamekwisha fika, na hivyo twajua kwamba mwisho u karibu.
19Jie yra išėję iš mūsų, tačiau nebuvo mūsiškiai. Jeigu jie būtų buvę mūsiškiai, jie būtų likę su mumis. Bet turėjo paaiškėti, jog ne visi yra mūsiškiai.
19Watu hao wametokea kati yetu lakini hawakuwa kweli wa kwetu na ndiyo maana walituacha; Kama wangalikuwa wa kwetu, wangalibaki nasi. Lakini waliondoka, wakaenda zao, kusudi ionekane wazi kwamba hawakuwa kamwe wa kwetu.
20Bet jūs turite Šventojo patepimą ir žinote viską.
20Ninyi, lakini, mlipata kumiminiwa Roho Mtakatifu na Kristo, na hivyo mnaujua ukweli.
21Aš parašiau jums ne kaip nežinantiems tiesos, bet todėl, kad pažįstate ją, o iš tiesos negali kilti joks melas.
21Basi, nawaandikieni, si kwa kuwa hamuujui ukweli, bali kwa sababu mnaujua; na pia mnajua kwamba uongo wowote haupatikani katika ukweli.
22Kas yra melagis, jeigu ne tas, kuris neigia, kad Jėzus yra Pateptasis? Tas yra antikristas, kuris neigia Tėvą ir Sūnų.
22Mwongo ni nani? Ni yule anayekana kwamba Yesu ni Masiha. Mtu wa namna hiyo ni adui wa Kristo--anamkana Baba na Mwana.
23Kiekvienas, kas neigia Sūnų, neturi ir Tėvo. Kas išpažįsta Sūnų, tas turi ir Tėvą.
23Maana yeyote anayemkana Mwana, anamkana pia Baba; na yeyote anayemkubali Mwana, anampata Baba pia.
24Todėl tepasilieka jumyse tai, ką girdėjote nuo pradžios. Jeigu tai, ką girdėjote nuo pradžios, pasilieka jumyse, tada ir jūs pasiliksite Sūnuje ir Tėve.
24Basi, ujumbe ule mliousikia tangu mwanzo na ukae mioyoni mwenu. Kama ujumbe huo mliousikia tangu mwanzo ukikaa ndani yenu, basi, mtaishi daima katika umoja na Mwana na Baba.
25Štai pažadas, kurį Jis pats mums davė,­amžinasis gyvenimas.
25Na ahadi aliyotuahidia sisi ndiyo hii: uzima wa milele.
26Aš tai parašiau apie tuos, kurie jus klaidina.
26Nimewaandikieni mambo haya kuhusu wale wanaotaka kuwapotosha ninyi.
27Bet patepimas, kurį iš Jo gavote, pasilieka jumyse, ir nereikia, kad jus kas nors mokytų, nes pats Jo patepimas moko jus visko, ir jis yra tiesa, o ne melas. Ir kadangi jis jus pamokė, jūs Jame pasiliksite.
27Lakini, kwa upande wenu ninyi, Kristo aliwamiminieni Roho wake. Na kama akiendelea kukaa ndani yenu, hamhitaji kufundishwa na mtu yeyote. Maana Roho wake anawafundisheni kila kitu na mafundisho yake ni ya kweli, si ya uongo. Basi shikeni mafundisho ya huyo Roho na kubaki katika muungano na Kristo.
28Taigi dabar, vaikeliai, pasilikite Jame, kad, kai Jis pasirodys, turėtumėte pasitikėjimą ir, kai Jis ateis, nebūtume prieš Jį sugėdinti.
28Naam, watoto, kaeni ndani yake kusudi wakati atakapotokea tuwe hodari bila kuwa na sababu ya kujificha kwa aibu Siku ya kuja kwake.
29Jei žinote, kad Jis teisus, tai žinokite, kad kiekvienas, kuris vykdo teisumą, iš Jo yra gimęs.
29Mnajua kwamba Kristo ni mwadilifu kabisa; basi, mnapaswa kujua pia kwamba kila mtu atendaye mambo adili ni mtoto wa Mungu.