Lithuanian

Swahili: New Testament

1 John

3

1Žiūrėkite, kokia meile apdovanojo mus Tėvas: mes vadinamės Dievo vaikai­ir esame! Pasaulis nepažįsta mūsų, nes ir Jo nepažino.
1Oneni basi, jinsi Baba alivyotupenda mno hata tunaitwa watoto wa Mungu! Na kweli, ndivyo tulivyo. Ndiyo maana ulimwengu haututambui sisi, kwani haumjui Mungu.
2Mylimieji, dabar mes esame Dievo vaikai, bet dar nepasirodė, kas būsime. Mes žinome, kad, kai Jis pasirodys, būsime panašūs į Jį, nes matysime Jį tokį, koks Jis yra.
2Wapenzi wangu, sisi ni watoto wa Mungu sasa, lakini bado haijaonekana wazi jinsi tutakavyokuwa. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwani tutamwona vile alivyo.
3Kiekvienas, kas turi Jame tokią viltį, skaistina pats save, nes ir Jis yra skaistus.
3Basi, kila mtu aliye na tumaini hili katika Kristo, hujiweka safi kama vile Kristo alivyo safi kabisa.
4Kiekvienas, kuris daro nuodėmę, laužo įstatymą. Nuodėmė­ tai įstatymo laužymas.
4Kila mtu atendaye dhambi anavunja sheria ya Mungu, maana dhambi ni uvunjaji wa sheria.
5Jūs žinote, jog Jis pasirodė, kad sunaikintų mūsų nuodėmes, ir Jame nėra nuodėmės.
5Mnajua kwamba Kristo alikuja kuziondoa dhambi zetu, na kwamba kwake hamna dhambi yoyote.
6Kas pasilieka Jame, tas nenusideda. Kiekvienas nuodėmiaujantis Jo neregėjo ir nepažino.
6Basi, kila aishiye katika muungano na Kristo hatendi dhambi; lakini kila mtu atendaye dhambi hakupata kamwe kumwona, wala kumjua Kristo.
7Vaikeliai! Tegul niekas jūsų nesuklaidina! Vykdantis teisumą yra teisus, kaip ir Jis teisus.
7Basi, watoto wangu, msikubali kupotoshwa na mtu yeyote. Mtu atendaye matendo maadilifu ni mwadilifu kama vile Kristo alivyo mwadilifu kabisa.
8Kas daro nuodėmę, tas iš velnio, nes velnias nuodėmiauja nuo pat pradžios. Todėl ir pasirodė Dievo Sūnus, kad sugriautų velnio darbus.
8Lakini atendaye dhambi ni wa Ibilisi, maana Ibilisi ametenda dhambi tangu mwanzo. Lakini Mwana wa Mungu alikuja duniani kuiharibu kazi ya Ibilisi.
9Kas yra gimęs iš Dievo, nedaro nuodėmės, nes jame laikosi Dievo sėkla. Jis negali nuodėmiauti, nes yra gimęs iš Dievo.
9Kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, maana anayo hali ya kimungu ndani yake; hawezi kutenda dhambi kwa sababu yeye ni mtoto wa Mungu.
10Taip išaiškėja Dievo vaikai ir velnio vaikai: tas, kuris nevykdo teisumo, nėra iš Dievo; taip pat tas, kuris savo brolio nemyli.
10Lakini yeyote asiyetenda mambo maadilifu, au asiyempenda ndugu yake, huyo si mtoto wa Mungu. Hiyo ndiyo tofauti iliyoko kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi.
11Tokia yra žinia, kurią girdėjote nuo pradžios: mes turime mylėti vieni kitus.
11Na, ujumbe mliousikia tangu mwanzo ndio huu: Tunapaswa kupendana!
12Ne kaip Kainas, kuris buvo iš piktojo ir nužudė savo brolį. Kodėl nužudė? Todėl, kad jo darbai buvo pikti, o brolio­teisūs.
12Tusiwe kama Kaini ambaye, kwa kuongozwa na yule Mwovu, alimuua ndugu yake. Na, kwa nini alimuua? Kwa sababu matendo yake yalikuwa maovu, lakini yale ya ndugu yake yalikuwa mema!
13Nesistebėkite, broliai, jei pasaulis jūsų nekenčia.
13Basi, ndugu zangu, msishangae kama ulimwengu unawachukia ninyi.
14Mes žinome, jog iš mirties perėjome į gyvenimą, nes mylime brolius. Kas nemyli savo brolio, tas pasilieka mirtyje.
14Sisi tunajua kwamba tumekwisha pita kutoka katika kifo na kuingia katika uzima kwa sababu tunawapenda ndugu zetu. Mtu asiye na upendo hubaki katika kifo.
15Kiekvienas, kas nekenčia savo brolio, yra žmogžudys, o jūs žinote, kad joks žmogžudys neturi amžinojo gyvenimo, jame pasiliekančio.
15Kila anayemchukia ndugu yake ni muuaji; nanyi mnajua kwamba muuaji yeyote yule hana uzima wa milele ndani yake.
16Mes iš to pažinome meilę, kad Jis už mus paguldė savo gyvybę. Ir mes turime guldyti savo gyvybę už brolius.
16Sisi tumepata kujua upendo ni nini, kwani Kristo aliyatoa maisha yake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya ndugu zetu.
17Bet jei kas turi šio pasaulio turtų ir, matydamas savo brolį stokojantį, užrakina jam savo širdį,­ kaip jame pasiliks Dievo meilė?
17Basi, mtu akiwa na mali za hapa duniani, halafu akamwona ndugu yake ana shida, lakini akawa na moyo mgumu bila kumwonea huruma, anawezaje kusema kwamba anampenda Mungu?
18Mano vaikeliai, nemylėkime žodžiu ar liežuviu, bet darbu ir tiesa.
18Watoto wangu, upendo wetu usiwe maneno matupu, bali uwe upendo wa kweli na wa vitendo.
19Tuo mes pažįstame, jog esame iš tiesos, ir Jo akivaizdoje nuraminame savo širdį.
19Hivyo ndivyo tuwezavyo kuwa na hakika kwamba sisi ni watu wa ukweli; na hatutakuwa na wasiwasi mbele ya Mungu.
20Jei mūsų širdis mus smerkia, Dievas didesnis už mūsų širdį ir žino viską.
20Kwa maana, hata kama dhamiri yetu yatuhukumu, twajua kwamba Mungu ni mkuu zaidi kuliko dhamiri, na kwamba yeye ajua kila kitu.
21Mylimieji, jei mūsų širdis mūsų nesmerkia, pasitikime Dievu
21Wapenzi wangu, kama dhamiri yetu haina lawama juu yetu, basi, twaweza kuwa na uthabiti mbele ya Mungu,
22ir gauname iš Jo, ko tik prašome, nes laikomės Jo įsakymų ir darome, kas Jam patinka.
22na twaweza kupokea kwake chochote tunachoomba, maana tunazitii amri zake na kufanya yale yanayompendeza.
23O štai Jo įsakymas: kad tikėtume Jo Sūnaus Jėzaus Kristaus vardą ir mylėtume vieni kitus, kaip Jo įsakyta.
23Na, amri yake ndiyo hii: Kumwamini Mwanae Kristo, na kupendana kama alivyotuamuru.
24Kas laikosi Jo įsakymų, pasilieka Jame ir Jis tame. O kad Jis mumyse pasilieka, žinome iš Dvasios, kurią Jis mums davė.
24Anayezitii amri za Mungu anaishi katika muungano na Mungu na Mungu anaishi katika muungano naye. Kwa njia ya Roho ambaye Mungu ametujalia, sisi twajua kwamba Mungu anaishi katika muungano nasi.