1Vergai, esantys po jungu, telaiko savo šeimininkus vertais visokeriopos pagarbos, kad nebūtų piktžodžiaujama Dievo vardui ir mokymui.
1Watumwa wote wanapaswa kuwaheshimu wakuu wao ili kusiwe na sababu ya watu kulitukana jina la Mungu na mafundisho yetu.
2O tie, kurie turi tikinčius šeimininkus, tegul jų neniekina, kadangi jie yra broliai; geriau tegul jiems dar uoliau tarnauja, nes, gaunantys naudą, yra tikintys ir mylimi. Taip mokyk ir taip ragink!
2Watumwa ambao wakuu wao ni Wakristo wasiwadharau kwani ni ndugu zao. Badala yake, wanapaswa kuwatumikia hata vizuri zaidi, maana hao wanaopata faida kutokana na kazi yao ni waumini ambao wanawapenda. Unapaswa kufundisha na kuhubiri mambo haya.
3Jei kas nors moko kitaip ir nesutinka su sveikais mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus žodžiais bei dievotumo mokymu,
3Mtu yeyote anayefundisha kinyume cha mambo haya, na ambaye hakubaliani na maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo na mafundisho ya dini,
4tas yra išdidus, nieko neišmano, serga nuo ginčų ir nuo svaidymosi žodžiais, iš kurių atsiranda pavydas, nesutarimas, piktžodžiavimas, blogi įtarinėjimai
4huyo amejaa majivuno na wala hajui chochote. Ni mtu wa kupenda ubishi na magombano juu ya maneno matupu, na hiyo husababisha wivu, ugomvi, matusi, shuku mbaya,
5ir kivirčai tarp sugedusio proto žmonių, praradusių tiesos nuovoką ir manančių, jog dievotumas esąs pasipelnymas. Šalinkis tokių.
5na ubishi usio na kikomo kutoka kwa watu ambao akili zao zimeharibika, na ambao hawana tena ukweli. Wanadhani dini ni njia ya kujipatia utajiri.
6Žinoma, dievotumas yra didelis pasipelnymas, kai jį lydi pasitenkinimas.
6Kweli dini humfanya mtu awe tajiri sana, ikiwa anatosheka na vitu alivyo navyo.
7Juk nieko neatsinešėme į pasaulį ir, aišku, nieko neišsinešime.
7Maana hatukuleta kitu chochote hapa duniani, wala hatutachukua chochote.
8Turėdami maisto ir drabužį, būkime patenkinti.
8Kwa hiyo basi, kama tunacho chakula na mavazi, tunapaswa kuridhika navyo.
9Kas trokšta praturtėti, pakliūva į pagundymą ir į pinkles bei į daugelį kvailų ir kenksmingų geidulių, kurie paskandina žmones sugedime ir pražūtyje.
9Lakini wale wanaotaka kutajirika huanguka katika majaribu, na kunaswa katika mtego wa tamaa nyingi mbaya za kipumbavu, ambazo huwavuta mpaka kwenye uharibifu na maangamizi.
10Visų blogybių šaknis yra meilė pinigams. Kai kurie, jų geisdami, nuklydo nuo tikėjimo ir patys save drasko aibe skausmų.
10Kwa maana kupenda sana fedha ni chanzo cha uovu wote. Watu wengine wametamani sana kupata fedha hata wakatangatanga mbali na imani, na wameivunja mioyo yao kwa huzuni nyingi.
11Bet tu, Dievo žmogau, bėk nuo tų dalykų ir vykis teisumą, maldingumą, tikėjimą, meilę, kantrumą, romumą.
11Lakini wewe, mtu wa Mungu, jiepushe na mambo hayo. Zingatia uadilifu, uchaji wa Mungu, imani, mapendo, subira na unyenyekevu.
12Kovok gerą tikėjimo kovą, laikykis amžinojo gyvenimo, kuriam esi pašauktas ir išpažinai gerą išpažinimą daugelio liudytojų akyse.
12Piga mbio kadiri uwezavyo katika shindano la mbio za imani, ukajipatie tuzo la uzima wa milele, uliloitiwa wakati ulipokiri imani yako mbele ya mashahidi wengi.
13Aš prašau tavęs prieš Dievą, kuris viskam teikia gyvybę, ir prieš Kristų Jėzų, kuris prie Poncijaus Piloto pateikė gerą išpažinimą,
13Mbele ya Mungu anayevipa vitu vyote uhai, na mbele ya Yesu Kristo aliyetoa ushahidi na kukiri ukweli mbele ya Pontio Pilato,
14kad išlaikytum šį įsakymą be dėmės ir be priekaišto iki mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus pasirodymo.
14nakuamuru ushike maagizo yako na kuyatii kwa uaminifu mpaka Siku ile atakapotokea Bwana wetu Yesu Kristo.
15Jį savo laiku apreikš palaimintasis vienintelis Valdovas, karalių Karalius ir viešpačių Viešpats,
15Kutokea kwake kutafanyika wakati ufaao uliopangwa na Mungu mwenye heri na aliye Mtawala pekee, Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.
16vienintelis Nemirtingasis, gyvenantis neprieinamoje šviesoje, kurio joks žmogus neregėjo ir negali regėti. Jam šlovė ir amžinoji valdžia! Amen.
16Yeye peke yake anaishi milele, katika mwanga usioweza kukaribiwa na mtu. Hakuna mtu aliyepata kumwona au awezaye kumwona. Kwake iwe heshima na uwezo wa milele! Amina.
17Šio amžiaus turtuoliams įsakyk, kad nesididžiuotų ir nesudėtų vilčių į netikrus turtus, bet į gyvąjį Dievą, kuris apsčiai visko mums teikia mūsų džiaugsmui.
17Waamuru watu walio matajiri katika mambo ya maisha ya sasa, wasijivune, wasiweke tumaini lao katika mali isiyoweza kutegemewa; bali wamtegemee Mungu, ambaye kwa ukarimu hutupatia vitu vyote tuvifurahie.
18Tegul jie daro gera, turtėja gerais darbais, būna dosnūs, dalijasi su kitais.
18Waamuru watende mema, wawe matajiri katika matendo mema, na wawe wakarimu na walio tayari kuwashirikisha wengine mali zao.
19Taip jie pasidės gerus pamatus ateičiai, kad pasiektų tikrąjį gyvenimą.
19Kwa namna hiyo watajiwekea hazina ambayo itakuwa kwao msingi imara kwa wakati ujao. Hapo wataweza kujipatia uzima ambao ni uzima wa kweli.
20O Timotiejau, saugok tai, kas tau patikėta, vengdamas netinkamo tuščiažodžiavimo ir tariamojo pažinimo prieštaravimų,
20Timotheo, tunza salama yote yale uliyokabidhiwa. Jiepushe na majadiliano ya kidunia na ubishi wa kipumbavu juu ya kile wanachokiita watu wengine: "Elimu".
21nes kai kurie, jam atsidavę, nuklydo nuo tikėjimo. Malonė tebūna su jumis! Amen.
21Maana wengine wamejidai kuwa na hiyo elimu, na matokeo yake wamepoteza imani. Nawatakieni nyote neema!