1Todėl, suprasdami, kad turime šį tarnavimą iš gailestingumo, mes nepailstame.
1Basi, Mungu, kwa huruma yake, ametukabidhi kazi hii na hivyo hatufi moyo.
2Atsisakę slaptų begėdysčių, nesileidžiame į gudravimus ir nekraipome Dievo žodžio, bet, atskleisdami tiesą, prisistatome kiekvieno žmogaus sąžinei Dievo akivaizdoje.
2Tumeyaacha kabisa mambo yote ya aibu na ya kisirisiri. Hatuishi tena kwa udanganyifu, wala kwa kulipotosha neno la Mungu; bali tunaudhihirisha ukweli kwa kuufanya ukweli, na hivyo kujiweka chini ya uamuzi wa dhamiri za watu mbele ya Mungu.
3O jeigu Evangelija yra paslėpta, tai ji paslėpta žūstantiems,
3Maana, kama Habari Njema tunayohubiri imefichika, imefichika tu kwa wale wanaopotea.
4kuriems šio amžiaus dievas apakino protus; netikintiems, kad jiems nesušvistų Kristaus, kuris yra Dievo atvaizdas, šlovės Evangelijos šviesa.
4Hao hawaamini kwa sababu yule mungu wa ulimwengu huu amezitia giza akili zao wasipate kuuona wazi mwanga wa Habari Njema ya utukufu wa Kristo, ambaye ni mfano kamili wa Mungu.
5Mes ne save pačius skelbiame, bet Kristų Jėzų kaip Viešpatį, o mesjūsų tarnai dėl Jėzaus.
5Maana hatujitangazi sisi wenyewe, ila tunamhubiri Yesu Kristo aliye Bwana, sisi wenyewe tukiwa watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.
6Nes tai Dievas, kuris įsakė iš tamsos nušvisti šviesai, sušvito mūsų širdyse, kad suteiktų mums Dievo šlovės pažinimo šviesą Kristaus veide.
6Mungu ambaye alisema, "Mwanga na uangaze kutoka gizani," ndiye mwenye kuiangaza mioyo yetu, na kutupatia mwanga wa ujuzi wa utukufu wa Mungu uangazao katika uso wa Kristo.
7Bet šitą turtą mes laikome moliniuose induose, kad būtų aišku, jog visa viršijanti jėgos apstybė iš Dievo, o ne iš mūsų.
7Basi, sisi tulio na hazina hii tuko tu kama vyombo vya udongo, ili ionekane wazi kwamba nguvu hiyo kuu yatoka kwa Mungu wala si kwetu sisi wenyewe.
8Mes visaip spaudžiami, bet nesugniuždyti; suglumę, bet nenusivylę;
8Daima twapata taabu, lakini hatugandamizwi; twapata mashaka, lakini hatukati tamaa;
9persekiojami, bet nepalikti; parblokšti, bet nežuvę.
9twateseka, lakini hatuachwi bila msaada; na ingawa tumeangushwa chini, hatukuangamizwa.
10Visada nešiojame savo kūne Viešpaties Jėzaus mirtį, kad ir Jėzaus gyvybė apsireikštų mūsų kūne.
10Kila wakati tumekuwa tukichukua mwilini mwetu kifo cha Kristo, ili uhai wake Yesu pia udhihirike katika miili yetu.
11Nes mes, gyvieji, dėl Jėzaus nuolat atiduodami mirčiai, kad ir Jėzaus gyvybė apsireikštų mūsų mirtingame kūne.
11Naam, katika maisha yetu yote tunakabiliwa na kifo daima kwa ajili ya Yesu, ili uzima wake Yesu udhihirike katika miili yetu inayokufa.
12Taigi mumyse veikia mirtis, o jumyse gyvybė.
12Hii ina maana kwamba ndani yetu kifo kinafanya kazi, lakini ndani yenu uhai unafanya kazi.
13Turėdami tą pačią tikėjimo dvasią, apie kurią parašyta: “Aš įtikėjau, todėl prakalbėjau”, mes irgi tikime ir todėl kalbame,
13Maandiko Matakatifu yasema: "Niliamini, ndiyo maana nilinena." Nasi pia, tukiwa na moyo huohuo wa imani, tunaamini, na kwa sababu hiyo twanena.
14žinodami, kad Tas, kuris prikėlė Viešpatį Jėzų, taip pat ir mus prikels per Jėzų ir pastatys kartu su jumis.
14Tunajua kwamba yule aliyemfufua Bwana Yesu atatufufua sisi pia pamoja na Yesu na kutuweka mbele yake pamoja nanyi.
15Nes viskas yra dėl jūsų, kad per daugelį pagausėjusi malonė pagausintų dėkojimą Dievo šlovei.
15Yote haya ni kwa faida yenu; ili kama vile neema ya Mungu inavyoenea kwa watu wengi zaidi na zaidi vivyo hivyo watu wengi zaidi watoe shukrani nyingi kwa utukufu wa Mungu.
16Todėl mes nepailstame. Nors mūsų išorinis žmogus ir nyksta, vidinis diena iš dienos atsinaujina.
16Kwa sababu hiyo hatufi moyo; na hata kama maumbile yetu ya nje yataoza, lakini kwa ndani tunafanywa wapya siku kwa siku.
17Mūsų trumpalaikis lengvas sielvartas ruošia mums visa pranokstančią amžinąją šlovę.
17Taabu tunayopata ni kidogo, tena ya muda tu: lakini itatupatia utukufu upitao matazamio yote, utukufu ambao hauna mwisho.
18Tuo tarpu mes nežiūrime į tai, kas regima, bet į tai, kas neregima, nes kas regima, yra laikina, o kas neregimaamžina.
18Hivyo tunatazamia kwa makini si vitu vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Maana vinavyoonekana ni vya muda tu; lakini vile visivyoonekana ni vya milele.