1Ar pradėsime iš naujo jums prisistatinėti? Gal mums reikia, kaip kai kuriems, palydimųjų laiškų jums ir iš jūsų?
1Je, tunaanza tena kujipendekeza? Je, tunahitaji barua ya utambulisho kwenu, au kutoka kwenu, kama watu wengine?
2Jūs esate mūsų laiškas, įrašytas mūsų širdyse, visų žmonių suprantamas ir skaitomas.
2Ninyi wenyewe ni barua yetu; barua iliyoandikwa mioyoni mwetu kila mtu aione na kuisoma.
3Jūs pasirodote esą Kristaus laiškas, mūsų tarnavimu parašytas ne rašalu, bet gyvojo Dievo Dvasia, ne akmens plokštėse, bet gyvų širdžių plokštėse.
3Ni dhahiri kwamba ninyi ni barua ya Kristo aliyoipeleka kwa mikono yetu. Barua yenyewe imeandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu hai; imeandikwa si juu ya kipande cha jiwe, bali juu ya mioyo ya watu.
4Tokį pasitikėjimą Dievu mes turime per Kristų.
4Tunaweza kusema hayo kwa sababu ya tumaini letu tulilo nalo kwa Mungu kwa njia ya Kristo.
5Ne todėl, kad būtume patys tinkami ką nors sumanyti tarytum iš savęs, bet mūsų tinkamumas iš Dievo,
5Si kwamba sisi tunaweza kufanya chochote kwa nguvu zetu wenyewe, ila uwezo wetu wote hutoka kwa Mungu:
6kuris padarė mus tinkamus būti Naujosios Sandoros tarnaisne raidės, bet Dvasios, nes raidė žudo, o Dvasia teikia gyvybę.
6maana yeye ndiye aliyetuwezesha kulihudumia Agano Jipya ambalo si agano la sheria iliyoandikwa, bali Agano la Roho. Maana sheria iliyoandikwa huleta kifo, lakini Roho huleta uzima.
7Jeigu mirties tarnavimas, išraižytas raidėmis akmenyse, buvo toks šlovingas, kad Izraelio vaikai negalėjo pažvelgti Mozei į veidą dėl jo veido šlovės, kuri buvo praeinanti,
7Sheria iliwekwa kwa kuandikwa juu ya vipande vya mawe. Ingawaje mwisho wake umekuwa kifo, utukufu wake ulikuwa mkuu mno hata wana wa Israeli wasiweze kuutazama uso wa Mose kwa sababu ya mng'ao wake. Tena mng'ao huo ulikuwa wa muda tu. Basi, ikiwa huduma ya kile ambacho kimesababisha kifo imefanyika kwa utukufu mwingi kiasi hicho,
8tai kiek šlovingesnis bus Dvasios tarnavimas?
8basi, huduma ya Roho ina utukufu mkuu zaidi.
9Jeigu pasmerkimo tarnavimas šlovingas, tai daug daugiau šlovingesnis teisumo tarnavimas.
9Ikiwa basi, kulikuwa na utukufu katika huduma ile iliyoleta hukumu, ni wazi kwamba huduma ile iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu itakuwa na utukufu mkuu zaidi.
10Tai, kas buvo šlovinga, visai nešlovinga, lyginant su visa pranokstančia šlove.
10Sasa utukufu mkuu zaidi umechukua nafasi ya ule utukufu uliokuja hapo awali, ambao fahari yake imekwisha toweka.
11Jeigu praeinantis dalykas buvo šlovingas, tai kur kas šlovingesnis pasiliekantis.
11Maana ikiwa kile kilichokuwa cha muda tu kilikuwa na utukufu wake, bila shaka kile chenye kudumu milele kitakuwa na utukufu mkuu zaidi.
12Taigi, turėdami tokią viltį, mes kalbame labai tiesiai ir drąsiai,
12Kwa vile hili ndilo tumaini letu, sisi twasema kwa uhodari mkuu.
13ne kaip Mozė, kuris ant veido užsileisdavo gaubtuvą, kad Izraelio vaikai nepamatytų to, kas praeina.
13Sisi hatufanyi kama Mose ambaye alilazimika kuufunika uso wake kwa kitambaa ili watu wa Israeli wasiuone ule mwisho wa mng'ao uliokuwa unafifia.
14Bet jų protai buvo apakinti. Iki šios dienos tas pats gaubtuvas lieka nenuimtas skaitant Senąjį Testamentą, nes jis nuimamas Kristuje.
14Lakini akili zao zilipumbazwa. Mpaka leo hii lisomwapo Agano la Kale, kifuniko hicho bado kipo. Kifuniko hicho kitaondolewa tu mtu anapoungana na Kristo.
15Net iki šios dienos, kai skaitomas Mozė, gaubtuvas tebedengia jų širdį.
15Naam, mpaka hivi leo kila isomwapo Sheria ya Mose akili zao huwa zimefunikwa.
16Bet kai žmogus atsigręžia į Viešpatį, gaubtuvas nuimamas.
16Lakini, wakati mtu amgeukiapo Bwana, kifuniko hicho huondolewa.
17Viešpats yra Dvasia. O kur Viešpaties Dvasia, ten laisvė.
17Hapa "Bwana" ni Roho; na pale alipo Roho wa Bwana ndipo ulipo uhuru.
18Mes visi, atidengtu veidu lyg veidrodyje regėdami Viešpaties šlovę, esame keičiami į tą patį atvaizdą iš šlovės į šlovę, veikiami Viešpaties, kuris yra Dvasia.
18Basi, sisi sote ambao nyuso zetu hazikufunikwa, twaonyesha kama katika kioo, utukufu wa Bwana; tunabadilishwa tufanane zaidi na huo mfano wake kwa utukufu mwingi zaidi. Hiyo ni kazi yake Roho wa Bwana.