1Taigi aš nusprendžiau, kad neatvyksiu pas jus vėl su liūdesiu.
1Basi nimeamua nisiwatembelee tena kuwatia huzuni.
2O jei aš jus liūdinu, tai kas gi mane pralinksmins, jeigu ne mano nuliūdintasis?
2Maana nikiwahuzunisha ninyi, basi, ni nani atakayenifariji? Ni walewale niliowahuzunisha!
3Aš tai parašiau, kad atvykęs neturėčiau liūdėti dėl tų, kuriais derėtų džiaugtis, pasitikėdamas jumis visais, kad mano džiaugsmas yra ir visų jūsų džiaugsmas.
3Ndiyo maana niliwaandikia--sikutaka kuja kwenu na kuhuzunishwa na ninyi ambao ndio mngepaswa kuwa furaha yangu. Nina hakika kwamba, mimi nikifurahi, ninyi nyote pia mnafurahi.
4Nes aš jums rašiau iš didelio skausmo ir širdies sielvarto, su gausiomis ašaromis, ne tam, kad jus nuliūdinčiau, bet kad pažintumėte meilę, kurios taip apsčiai jums turiu.
4Nilipowaandikia hapo awali katika hali ya huzuni na sikitiko moyoni na kwa machozi mengi, haikuwa kwa ajili ya kuwahuzunisha ninyi, bali kwa ajili ya kuwaonyesheni kwamba nawapenda mno.
5Bet jeigu kas nuliūdino, tai nuliūdino ne mane, bet,—kad neperdėčiau,—bent iš daliesjus visus.
5Ikiwa kuna mtu aliyemhuzunisha mwingine, hakunihuzunisha mimi--ila amewahuzunisha ninyi nyote, na sipendi kuwa mkali zaidi.
6Tokiam žmogui pakanka daugumos paskirtos bausmės.
6Adhabu aliyokwisha pata kutoka kwa wengi wenu inamtosha.
7Net atvirkščiai, jūs turėtumėte jam atleisti ir jį paguosti, kad jo neapimtų pernelyg didelis liūdesys.
7Iliyobakia ni afadhali kwenu kumsamehe mtu huyo na kumpa moyo ili asije akahuzunika mno na kukata tamaa kabisa.
8Todėl aš prašau jus parodyti jam meilę.
8Kwa hiyo nawasihi: mwonyesheni kwamba mnampenda.
9Nes tuo tikslu jums ir parašiau, kad patikrinčiau, ar jūs visais atžvilgiais esate klusnūs.
9Madhumuni yangu kuandika ile barua yalikuwa kutaka kujua kama mko tayari kutii katika kila jambo.
10Kam jūs atleidžiate, tam atleidžiu ir aš; nes, jei kam atleidau, tai padariau dėl jūsų Kristaus akivaizdoje,
10Mkimsamehe mtu, nami pia ninamsamehe. Maana ninaposamehe--kama kweli ninacho cha kusamehe--nasamehe mbele ya Kristo kwa ajili yenu,
11kad neapgautų mūsų šėtonas. Nes mums nėra nežinomi jo kėslai.
11ili tusimpe nafasi Shetani atudanganye; maana twaijua mipango yake ilivyo.
12Kai atvykau į Troadę skelbti Kristaus Evangelijos, durys man buvo Viešpaties atvertos,
12Nilipofika Troa kuhubiri Habari Njema ya Kristo, nilikuta mlango u wazi kwa ajili ya kazi ya Bwana.
13bet aš neturėjau savo dvasioje ramybės, kadangi nesutikau savo brolio Tito; tad atsisveikinęs iškeliavau į Makedoniją.
13Lakini nilifadhaika sana kwa kutomkuta ndugu yetu Tito. Ndiyo maana niliwaaga wote pale nikaenda Makedonia.
14Dėkui Dievui, kuris visada veda mus Kristuje triumfo eisenoje ir per mus kiekvienoje vietoje skleidžia mielą Jo pažinimo kvapą.
14Lakini, shukrani kwa Mungu anayetuongoza daima katika msafara wa ushindi wa Kristo. Yeye hutufanya tuueneze ukweli wa Kristo kama harufu nzuri, kila mahali.
15Juk mes esame Kristaus malonus kvapas Dievui tarp išgelbėtų ir tarp žūstančių.
15Maana sisi ni kama harufu nzuri ya ubani ambayo Kristo anamtolea Mungu, harufu nzuri inayofikia wote wanaookolewa na wanaopotea.
16Vieniemsmirties kvapas mirčiai, kitiemsgyvenimo kvapas gyvenimui. O kas gi yra tam tinkamas?
16Kwa wale wanaopotea, harufu hiyo ni kifo; lakini kwa wale wanaookolewa, harufu hiyo ni uhai. Nani basi, awezaye kushiriki katika kazi ya namna hiyo?
17Mes neprekiaujame, kaip daugelis, Dievo žodžiu, bet nuoširdžiai, kaip iš Dievo, kalbame Kristuje, Dievo akivaizdoje.
17Sisi si kama wengine ambao hufanya biashara na ujumbe wa Mungu; sisi tunahubiri kwa unyofu mbele ya Mungu, kama watu tuliotumwa na Mungu, tukiwa tumeungana na Kristo.