Lithuanian

Swahili: New Testament

2 Corinthians

6

1Būdami Jo bendradarbiai, jūsų taip pat prašome, kad nepriimtumėte Dievo malonės veltui!
1Basi, tukiwa wafanyakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msikubali ile neema mliyopokea kutoka kwa Mungu ipotee bure.
2Nes Jis sako: “Aš išklausiau tave priimtinu metu ir išgelbėjimo dieną Aš padėjau tau”. Štai dabar yra priimtinas metas, štai dabar išgelbėjimo diena!
2Mungu asema hivi: "Wakati wa kufaa nimekusikiliza, wakati wa wokovu nikakusaidia." Basi, sasa ndio wakati wa kufaa, sasa ndiyo siku ya wokovu!
3Mes niekuo neduodame akstino pasipiktinti, kad mūsų tarnavimas nebūtų peiktinas.
3Kusudi tusiwe na lawama yoyote katika utumishi wetu, hatupendi kumwekea mtu yeyote kizuio chochote.
4Bet visame kame pasirodome Dievo tarnai: su didele kantrybe, skausmuose, sunkumuose, suspaudimuose,
4Badala yake, tunajionyesha kuwa kweli watumishi wa Mungu kwa kila kitu: kwa uvumilivu mwingi wakati wa mateso, shida na taabu.
5plakimuose, įkalinimuose, sąmyšiuose, darbuose, budėjimuose, pasninkuose;
5Tumepigwa, tumetiwa gerezani na kuzomewa hadharani; tumefanya kazi tukachoka; tumekesha na kukaa bila kula.
6tyrumu, pažinimu, pakantumu, gerumu, Šventąja Dvasia, neveidmainiška meile,
6Tunajionyesha kuwa watumishi wa Mungu kwa usafi wa moyo, elimu, uvumilivu na wema; kwa Roho Mtakatifu, kwa upendo usio na unafiki,
7tiesos žodžiu, Dievo jėga, teisumo ginklais iš dešinės ir kairės;
7kwa ujumbe wa kweli na kwa nguvu ya Mungu. Uadilifu ndiyo silaha yetu upande wa kulia na upande wa kushoto.
8gerbiami ir negerbiami, šmeižiami ir giriami, laikomi apgavikais ir teisiais,
8Tuko tayari kupata heshima na kudharauliwa, kulaumiwa na kusifiwa. Twadhaniwa kuwa waongo, kumbe twasema kweli;
9nepažįstamais ir gerai žinomais, laikomi mirštančiais­bet štai mes gyvi; esame baudžiami, bet nenužudomi,
9kama wasiojulikana, kumbe twajulikana kwa wote, kama waliokufa, lakini mwonavyo, sisi ni wazima kabisa.
10mus liūdina, bet mes visada džiaugiamės, esame skurdžiai, bet daugelį praturtiname, neturime nieko­ir valdome viską.
10Ingawa tumeadhibiwa, hatukuuawa; ingawa tunayo huzuni, twafurahi daima; ingawa tu maskini hohehahe, lakini twatajirisha watu wengi; twaonekana kuwa watu tusio na chochote, kumbe tuna kila kitu.
11O korintiečiai! Mūsų lūpos atvirai jums prabilo, mūsų širdis plačiai atverta.
11Ndugu Wakorintho, tumezungumza nanyi kwa unyofu; mioyo yetu iko wazi kabisa.
12Ne mumyse jums ankšta; ankšta jūsų pačių širdyse.
12Kama mnaona kuna kizuizi chochote kile, kizuizi hicho kiko kwenu ninyi wenyewe, na si kwa upande wetu.
13Tad atsimokėkite tuo pačiu,­ kalbu kaip vaikams,­ir taip pat atsiverkite.
13Sasa nasema nanyi kama watoto wangu, wekeni mioyo yenu wazi kama nasi tulivyofanya.
14Nevilkite svetimo jungo su netikinčiais. Kas gi bendro tarp teisumo ir nusikaltimo? Ir kas bendro tarp šviesos ir tamsos?
14Msiambatane na watu wasioamini. Je, wema na uovu vyapatana kweli? Mwanga na giza vyawezaje kukaa pamoja?
15Kaipgi galima gretinti Kristų su Beliaru? Arba kokia dalis tikinčio su netikinčiu?
15Kristo anawezaje kupatana na Shetani? Muumini ana uhusiano gani na asiyeamini?
16Ir kaip suderinti Dievo šventyklą su stabais? Juk jūs esate gyvojo Dievo šventykla, kaip Dievas yra pasakęs: “Aš gyvensiu juose ir vaikščiosiu tarp jų; būsiu jų Dievas, ir jie bus manoji tauta”.
16Hekalu la Mungu lina uhusiano gani na sanamu za uongo? Maana sisi ni hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu mwenyewe alivyosema: "Nitafanya makao yangu kwao, na kuishi kati yao; Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu."
17Todėl: “Išeikite iš jų ir atsiskirkite,­sako Viešpats,­ir nelieskite to, kas netyra, ir Aš jus priimsiu
17Kwa hiyo Bwana asema pia: "Ondokeni kati yao, mkajitenge nao, msiguse kitu najisi, nami nitawapokea.
18ir būsiu jums Tėvas, o jūs būsite mano sūnūs ir dukterys,­sako visagalis Viešpats”.
18Mimi nitakuwa Baba yenu, nanyi mtakuwa watoto wangu, waume kwa wake, asema Bwana Mwenye Uwezo."