Lithuanian

Swahili: New Testament

2 Corinthians

7

1Taigi, mylimieji, turėdami tokius pažadus, apsivalykime nuo visos kūno ir dvasios nešvaros, tobulindami šventumą Dievo baimėje.
1Basi, wapenzi wangu, tukiwa tumepewa ahadi hizi zote, na tujitakase na chochote kiwezacho kuchafua miili na roho zetu, tuwe watakatifu kabisa, na tuishi kwa kumcha Mungu.
2Priimkite mus. Mes nė vieno nenuskriaudėme, nė vienam nepakenkėm, nė vieno neapgavome.
2Tunaomba mtupe nafasi mioyoni mwenu! Hatujamkosea mtu yeyote, hatujamdhuru wala kumdanganya mtu yeyote.
3Tai sakau, ne norėdamas jus smerkti. Nes jau esu sakęs, jog esate mūsų širdyse, kad kartu mirtume ir kartu gyventume.
3Sisemi mambo haya kwa ajili ya kumhukumu mtu; maana, kama nilivyokwisha sema, ninyi mko mioyoni mwetu, tufe pamoja, tuishi pamoja.
4Aš labai pasitikiu jumis ir labai jumis didžiuojuosi. Esu kupinas paguodos ir džiaugsmo visuose mūsų sunkumuose.
4Nina imani kubwa sana ninaposema nanyi; naona fahari kubwa juu yenu! Katika taabu zetu nimepata kitulizo kikubwa na kufurahi mno.
5Kai atvykome į Makedoniją, mūsų kūnui neteko patirti nė kiek ramybės; mes buvome visokeriopai varginami: iš išorės­kovos, viduje­baimė.
5Hata baada ya kufika Makedonia hatukuweza kupumzika. Kila upande tulikabiliwa na taabu: nje ugomvi; ndani hofu.
6Bet Dievas, pažemintųjų guodėjas, paguodė mus Tito atvykimu.
6Lakini Mungu, mwenye kuwapa shime wanyonge alitupa moyo sisi pia kwa kuja kwake Tito.
7Ir ne vien jo atvykimu, bet ir ta paguoda, kuria jis buvo paguostas pas jus. Jis pranešė mums apie jūsų karštą troškimą, dejones, jūsų uolumą man. Taigi aš pradžiugau dar labiau.
7Si tu kwa kule kuja kwake Tito, bali pia kwa sababu ya moyo mliompa ninyi. Yeye ametuarifu jinsi mnavyotamani kuniona, jinsi mlivyo na huzuni, na mnavyotaka kunitetea. Jambo hili linanifurahisha sana.
8Todėl jeigu nuliūdinau jus laišku, tai šito nesigailiu, nors ir apgailestavau. Nes matau, kad tas laiškas jus nuliūdino, bet tik kuriam laikui.
8Maana, hata kama kwa barua ile yangu nimewahuzunisha, sioni sababu ya kujuta. Naam, naona kwamba barua hiyo iliwatia huzuni lakini kwa muda.
9Dabar aš džiaugiuosi, žinoma, ne todėl, kad jums teko nuliūsti, bet kad jūsų nuliūdimas atvedė jus į atgailą. Jūs buvote nuliūdę dievišku liūdesiu, todėl iš mūsų pusės nebuvo jums jokios skriaudos.
9Sasa nafurahi, si kwa sababu mmehuzunika, ila kwa kuwa huzuni yenu imewafanya mbadili nia zenu na kutubu. Mmehuzunishwa kadiri ya mpango wa Mungu, na kwa sababu hiyo hatukuwadhuru ninyi kwa vyovyote.
10Dieviškas liūdesys gimdo atgailą išgelbėjimui, dėl kurio nereikia gailėtis; o pasaulio liūdesys gimdo mirtį.
10Kuwa na huzuni jinsi atakavyo Mungu, husababisha badiliko la moyo, badiliko lenye kuleta wokovu; hivyo hakuna sababu ya kujuta. Lakini huzuni ya kidunia huleta kifo.
11Ir štai kaip tik tas dieviškas nuliūdimas pagimdė jumyse tokį susirūpinimą, tokį teisinimąsi, apmaudą, baimę, tokį stiprų troškimą, uolumą, tokį atpildą! Jūs visais atžvilgiais pasirodėte švarūs šiame reikale.
11Sasa mnaweza kuona matokeo ya kuona huzuni jinsi Mungu atakavyo: ninyi mmepata kuwa sasa watu wenye jitihada, wenye hoja, mnashtuka na kuogopa, mna bidii na mko tayari kuona kwamba haki yatekelezwa. Ninyi mmethibitisha kwa kila njia kwamba hamna hatia kuhusu jambo hili.
12Todėl, jeigu jums parašiau, tai ne dėl įžeidėjo ir ne dėl įžeistojo, bet kad jums paaiškėtų mūsų rūpestis jumis Dievo akivaizdoje.
12Hivyo, ingawa niliandika ile barua, haikuwa kwa ajili ya yule aliyekosa, au kwa ajili ya yule aliyekosewa. Niliandika kusudi ionekane wazi mbele ya Mungu jinsi mlivyo na bidii kwa ajili yetu.
13Todėl mes pasiguodėme jūsų paguoda ir dar labiau nudžiugome dėl Tito džiaugsmo, nes jo dvasia buvo jūsų visų atgaivinta.
13Ndiyo maana sisi tulifarijika sana. Siyo kwamba tulifarijika tu, ila pia Tito alitufurahisha kwa furaha aliyokuwa nayo kutokana na jinsi mlivyomchangamsha moyo.
14Taigi nelikau sugėdintas, kad jam buvau pasigyręs jumis, bet kaip ir viską jums teisingai kalbėjome, taip ir mūsų pasigyrimas Titui pasirodė teisingas.
14Mimi nimewasifu sana mbele yake, na katika jambo hilo sikudanganyika. Tumewaambieni ukweli daima, na kule kuwasifia ninyi mbele ya Tito kumekuwa jambo la ukweli mtupu.
15Ir jo širdis dar labiau prisirišusi prie jūsų, nes jis prisimena jūsų paklusnumą ir kaip priėmėte jį su baime ir drebėdami.
15Hivyo upendo wake wa moyo kwenu unaongezeka zaidi akikumbuka jinsi ninyi nyote mlivyo tayari kutii, na jinsi mlivyomkaribisha kwa hofu nyingi na kutetemeka.
16Todėl džiaugiuosi, kad visais atžvilgiais galiu jumis pasitikėti.
16Nafurahi sana kwamba naweza kuwategemea ninyi kabisa katika kila jambo.