Lithuanian

Swahili: New Testament

2 Corinthians

8

1Be to, pranešame jums, broliai, apie Dievo malonę, suteiktą Makedonijos bažnyčioms.
1Ndugu, tunapenda kuwapa habari juu ya neema ambazo Mungu ameyajalia makanisa ya Makedonia.
2Nors dideli vargai jas bandė, jos pasirodė kupinos džiaugsmo, ir jų gilus skurdas išsiliejo ypatingo dosnumo turtais.
2Waumini wa huko walijaribiwa sana kwa taabu; lakini furaha yao ilikuwa kubwa hivi hata wakawa wakarimu kupita kiasi, ingawaje walikuwa maskini sana.
3Aš liudiju, kad jie pagal išgales ir viršydami išgales, savo noru,
3Naweza kushuhudia kwamba walikuwa wakarimu kadiri ya nguvu zao na hata zaidi. Kwa hiari yao wenyewe,
4prašyte prašė mus, kad mes priimtume dovaną ir jų dalyvavimą tarnavime šventiesiems.
4walitusihi sana wapewe nafasi ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watu wa Mungu.
5Ir ne tik taip, kaip mes tikėjomės, bet visų pirma atsidavė Viešpačiui, o paskui Dievo valia ir mums.
5Hilo lilikuwa jambo ambalo hatukulitazamia kabisa! Kwanza walijitolea wao wenyewe kwa Bwana, kisha wakajitolea wenyewe kwetu pia, kufuatana na mapenzi ya Mungu.
6Todėl mes paprašėme Titą, kad taip, kaip pradėjo, taip ir baigtų pas jus šią malonę.
6Kwa sababu hiyo, tulimsihi Tito aliyeianza kazi hiyo awasaidieni pia muitekeleze huduma hii ya upendo miongoni mwenu.
7Tad, būdami visa ko pertekę­tikėjimo, žodžio, pažinimo, visokeriopo uolumo ir meilės mums,­ būkite pertekę ir šios malonės.
7Ninyi mna kila kitu: imani, uwezo wa kusema, elimu; bidii yote ya kutenda mema, na upendo wenu kwetu. Hivyo, tunatazamia muwe wakarimu katika huduma hii ya upendo.
8Tai sakau ne įsakydamas, bet norėdamas kitų uolumu patikrinti jūsų meilės nuoširdumą.
8Siwapi ninyi amri, lakini nataka tu kuonyesha jinsi wengine walivyo na bidii ya kusaidia ili nipate kujua jinsi upendo wenu ulivyo wa kweli.
9Nes jūs pažįstate mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus malonę, jog Jis, būdamas turtingas, dėl jūsų tapo vargšu, kad jūs per Jo neturtą taptumėte turtingi.
9Maana, ninyi mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo: yeye, ingawa alikuwa na kila kitu, alijifanya maskini kwa ajili yenu, ili kutokana na umaskini wake, awatajirishe.
10Ir čia aš duodu patarimą, nes tai naudinga jums, kurie ne tik pradėjote daryti tai anksčiau, bet ir troškote jau nuo pernai.
10Kuhusu jambo hili, basi, nawapeni shauri hili: inafaa kwenu kutekeleza sasa yale mliyoanza mwaka jana. Ninyi mlikuwa wa kwanza kuchukua hatua na kuamua kufanya hivyo.
11Taigi dabar pabaikite šį darbą, kad jūsų nuovokus troškimas būtų įvykdytas iš to, ką turite.
11Basi, kamilisheni shughuli hiyo; na kama vile mlivyokuwa na hamu kubwa ya kusaidia, basi, fanyeni bidii vivyo hivyo, kadiri ya uwezo wenu, kuikamilisha.
12Nes jei yra sąmoningas noras, jis priimtinas pagal tai, ką žmogus turi, o ne pagal tai, ko neturi.
12Maana ikiwa mtu ana moyo wa kusaidia, Mungu hupokea kila anachoweza kutoa: hadai zaidi.
13Aš nenoriu, kad kitiems tektų lengvatos, o jums naštos,
13Ninyi hampaswi kuongezewa taabu kusudi wengine wapunguziwe mzigo wao; sivyo, ila ni lazima tujali usawa na haki.
14bet kad būtų lygybė: kad šiuo metu jūsų perteklius patenkintų jų nepriteklių, o vėliau jų perteklius taip pat patenkintų jūsų nepriteklių ir būtų lygybė,
14Kila mlicho nacho sasa cha ziada kiwasaidie wale wanaohitaji, ili nao wakati watakapokuwa na ziada, wawasaidie ninyi katika mahitaji yenu, na hivyo kuwe na usawa.
15kaip parašyta: “Kas daug surinko, neturėjo atliekamo, o kas mažai­nekentėjo nepritekliaus”.
15Kama Maandiko yasemavyo: "Aliyekusanya kwa wingi hakuwa na ziada, na yule aliyekusanya kidogo hakupungukiwa."
16Dėkui Dievui, įdėjusiam į Tito širdį tą patį uolų rūpestį jumis.
16Namshukuru Mungu aliyeweka ndani ya moyo wa Tito hamu hiyo niliyo nayo mimi ya kuwasaidia.
17Jis ne tik paklausė mano raginimo, bet, būdamas labai uolus, nuvyko pas jus savo noru.
17Si tu kwamba alikubali ombi letu, ila pia alikuwa na hamu kubwa ya kusaidia, hata akaamua kwa hiari yake mwenyewe kuja kwenu.
18Kartu su juo pasiuntėme brolį, giriamą dėl Evangelijos skelbimo visose bažnyčiose.
18Pamoja naye, tunamtuma ndugu mmoja ambaye sifa zake katika kueneza Habari Njema zimeenea katika makanisa yote.
19Dar daugiau, jis yra bažnyčių paskirtas mūsų kelionių palydovu šiai malonei, kurią mes vykdome paties Viešpaties šlovei ir jūsų paslaugumui parodyti,
19Zaidi ya hayo, yeye amechaguliwa na makanisa awe mwenzetu safarini wakati tunapopeleka huduma hii yetu ya upendo, huduma tunayoifanya kwa ajili ya utukufu wa Bwana na uthibitisho wa nia yetu njema.
20sergėdamiesi, kad niekas mūsų nekaltintų dėl šios gausos, kurią mes tvarkome.
20Tunataka kuepa lawama zinazoweza kutokea kuhusu usimamizi wetu juu ya zawadi hii karimu.
21Mes rūpinamės tuo, kas gerbtina ne tik Viešpaties, bet ir žmonių akyse.
21Nia yetu ni kufanya vema, si tu mbele ya Bwana, lakini pia mbele ya watu.
22Taigi su jais pasiuntėme savo brolį, kurio uolumą daugel kartų įvairiai esame patikrinę ir kuris dabar yra dar uolesnis labai jumis pasitikėdamas.
22Basi, pamoja na ndugu hao, tumemtuma ndugu yetu mwingine ambaye mara nyingi tumempa majaribio mbalimbali, tukamwona kuwa ni mwenye hamu kubwa ya kusaidia; hata sasa amekuwa na moyo zaidi kwa sababu ana imani sana nanyi.
23Titas‰tai mano bendražygis ir jūsų pagalbininkas, o tie mūsų broliai‰bažnyčių pasiuntiniai, Kristaus šlovė.
23Tito ni mwenzangu; tunafanya kazi pamoja kwa ajili yenu; lakini kuhusu hawa ndugu zetu wengine, wanaokuja pamoja nao, hao ni wajumbe wa makanisa, na utukufu kwa Kristo.
24Todėl jų ir visų bažnyčių akyse įrodykite savo meilę ir mūsų pasigyrimą jumis.
24Basi, waonyesheni uthabiti wa upendo wenu, makanisa yapate kuona kweli kwamba fahari ninayoona juu yenu ni ya halali.