1Mylimieji, tai jau antras laiškas, kurį jums rašau. Šiuose laiškuose žadinu jūsų tyras mintis prisiminimais,
1Wapenzi wangu, hii ni barua ya pili ninayowaandikia. Katika barua hizo mbili nimejaribu kufufua fikira safi akilini mwenu kwa kuwakumbusheni mambo haya.
2kad atsimintumėte šventųjų pranašų iš anksto paskelbtus žodžius ir mūsųViešpaties ir Gelbėtojo apaštalųįsakymą.
2Napenda mkumbuke maneno yaliyosemwa na manabii watakatifu, na ile amri ya Bwana na Mwokozi mliyopewa na mitume wenu.
3Pirmiausia žinokite, kad paskutinėmis dienomis pasirodys šaipūnai, gyvenantys savo geiduliais
3Awali ya yote jueni kwamba siku za mwisho watakuja watu ambao mienendo yao inatawaliwa na tamaa zao mbaya. Watawadhihaki ninyi
4ir kalbantys: “Kur Jo atėjimo pažadas? Juk nuo to laiko, kai užmigo protėviai, visa pasilieka kaip buvę nuo sutvėrimo pradžios”.
4na kusema: "Aliahidi kwamba atakuja! Je, sasa yuko wapi? Mambo ni yaleyale tangu babu zetu walipokufa; hali ya vitu ni ileile kama ilivyokuwa mwanzo wa ulimwengu!"
5Mat jiems, to norintiems, yra paslėpta, kad nuo seno buvo dangūs ir žemė, iš vandens ir per vandenį sutvarkyta Dievo žodžiu.
5Watu hao, kwa makusudi, husahau kwamba zamani Mungu alinena, nazo mbingu na nchi zikaumbwa. Dunia iliumbwa kutoka katika maji na kwa maji;
6Todėl ir ano meto pasaulis žuvo, vandeniu užtvindytas.
6na kwa maji hayo, yaani yale maji ya gharika kuu, dunia ya wakati ule iliangamizwa.
7O dabartiniai dangūs ir žemė tuo pačiu žodžiu palaikomi ugniai, saugomi teismo dienai ir bedievių žmonių žuvimui.
7Lakini mbingu na nchi za sasa zahifadhiwa kwa neno la Mungu kwa ajili ya kuharibiwa kwa moto. Zimewekwa kwa ajili ya Siku ile ambapo watu wasiomcha Mungu watahukumiwa na kuangamizwa.
8Tačiau, mylimieji, vienas dalykas neturi likti jūsų nepastebėtas: viena diena pas Viešpatį yra kaip tūkstantis metų, ir tūkstantis metųkaip viena diena.
8Lakini, wapenzi wangu, msisahau kitu kimoja! Mbele ya Bwana, hakuna tofauti kati ya siku moja na miaka elfu; kwake yote ni mamoja.
9Viešpats nedelsia ištesėti savo pažado, kaip kai kurie mano, bet kantriai elgiasi su mumis, nenorėdamas, kad kuris pražūtų, bet kad visi atsiverstų.
9Bwana hakawii kutimiza yale aliyoahidi kama watu wengine wanavyofikiri kuwa atakawia. Yeye ana saburi kwa ajili yenu, maana hapendi hata mmoja wenu apotee, bali huwavuta wote wapate kutubu.
10O Viešpaties diena ateis kaip vagis naktį. Tada dangūs praeis su smarkiu ūžesiu, elementai sutirps karštyje, ir žemė su savo kūriniais sudegs.
10Siku ya Bwana itakuja kama mwizi. Siku hiyo, mbingu zitatoweka kwa kishindo kikuu; vitu vyake vya asili vitateketezwa kwa moto, nayo dunia itatoweka pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake.
11Jeigu visa taip suirs, tai kaip reikėtų pasižymėti šventu elgesiu ir dievotumu jums,
11Maadamu kila kitu kitaharibiwa namna hiyo, je, ninyi mnapaswa kuwa watu wa namna gani? Mnapaswa kuishi kitakatifu na kumcha Mungu,
12laukiantiems ir skubinantiems Dievo dienos atėjimą, kai dangūs suirs liepsnose ir elementai sutirps iš karščio!
12mkiingojea Siku ile ya Mungu na kuifanya ije upesi--Siku ambayo mbingu zitateketezwa kwa moto na kuharibiwa, na vitu vyake vya asili vitayeyushwa kwa joto.
13Tačiau mes pagal Jo pažadą laukiame naujo dangaus ir naujos žemės, kuriuose gyvena teisumas.
13Lakini sisi, kufuatana na ahadi yake, twangojea mbingu mpya na dunia mpya ambayo imejaa uadilifu.
14Todėl, mylimieji, šito laukdami, stenkitės, kad Jis rastų jus taikoje, nesuteptus ir nepeiktinus.
14Kwa hiyo wapenzi wangu, mkiwa mnangojea Siku ile, fanyeni bidii kuwa safi kabisa bila hatia mbele ya Mungu, na kuwa na amani naye.
15Mūsų Viešpaties kantrumą laikykite išgelbėjimu, kaip jums parašė ir mūsų mylimas brolis Paulius pagal jam duotą išmintį;
15Mnapaswa kuuona uvumilivu wa Bwana kuwa ni nafasi anayowapeni mpate kuokolewa, kama Paulo ndugu yetu mpenzi alivyowaandikia akitumia hekima aliyopewa na Mungu.
16jis taip kalba apie šituos dalykus visuose laiškuose. Juose esama sunkiai suprantamų dalykų, kuriuos neišmokyti ir svyruojantys iškraipo, aiškindami, kaip ir kitus Raštus, savo pačių pražūčiai.
16Hayo ndiyo asemayo katika barua zake zote anapozungumzia suala hilo. Yapo mambo kadhaa katika barua zake yaliyo magumu kuyaelewa, mambo ambayo watu wajinga, wasio na msimamo, huyapotosha kama wanavyopotosha sehemu nyingine za Maandiko Matakatifu. Hivyo wanasababisha maangamizi yao wenyewe.
17Tad jūs, mylimieji, iš anksto tai žinodami, saugokitės, kad, nedorėlių paklydimo traukiami, nenupultumėte nuo savo stiprybės.
17Lakini ninyi, wapenzi wangu, mmekwisha jua jambo hili. Basi, muwe na tahadhari msije mkapotoshwa na makosa ya waasi, mkaanguka kutoka katika msimamo wenu imara.
18Aukite malone ir mūsų Viešpaties ir Gelbėtojo Jėzaus Kristaus pažinimu. Jam šlovė dabar ir per amžius! Amen.
18Lakini endeleeni kukua katika neema na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu uwe kwake, sasa na hata milele! Amina.