1Buvo tautoje ir netikrų pranašų, kaip ir tarp jūsų bus netikrų mokytojų, kurie paslapčia įves pražūtingų erezijų, išsigindami net juos atpirkusio Viešpaties, ir užsitrauks greitą žlugimą.
1Palitokea manabii wa uongo kati ya watu, na vivyo hivyo walimu wa uongo watatokea kati yenu. Watu hao wataingiza mafundisho maharibifu na kumkana Bwana aliyewakomboa, na kwa njia hiyo watasababisha ghafla maangamizi yao wenyewe.
2Daugelis paseks jų pražūtingais keliais, ir dėl jų bus piktžodžiaujama tiesos keliui.
2Tena watu wengi watazifuata hizo njia zao mbaya, kwa sababu yao, wengine wataipuuza Njia ya ukweli.
3Iš godumo jie išnaudos jus suktais žodžiais. Bet nuo seno pasmerkimas jų laukia ir žuvimas nesnaudžia.
3Kwa tamaa yao mbaya watajipatia faida kwa kuwaambieni hadithi za uongo. Lakini kwa muda mrefu sasa Hakimu wao yu tayari, na Mwangamizi wao yu macho!
4Dievas nepagailėjo nusidėjusių angelų, bet surišo juos tamsos raiščiais giliausiose pragaro gelmėse, kur laiko juos teismui.
4Malaika walipotenda dhambi, Mungu hakuwahurumia, bali aliwatupa katika moto wa Jehanamu ambako wamefungwa wakingojea Siku ile ya Hukumu.
5Jis nepagailėjo senojo pasaulio, tik išsaugojo teisumo šauklį Nojų ir dar septynetą, kai siuntė bedievių pasauliui tvaną.
5Mungu hakuihurumia dunia ya hapo kale, bali alileta gharika kuu juu ya nchi ile ya watu wasiomcha Mungu; lakini Noa ambaye alihubiri uadilifu, Mungu alimwokoa pamoja na watu wengine saba.
6Paversdamas pelenais Sodomos ir Gomoros miestus, pasmerkė juos žlugti ir taip davė pavyzdį ateities bedieviams.
6Mungu aliadhibu miji ya Sodoma na Gomora, akaiteketeza kwa moto, akaifanya iwe mfano wa mambo yatakayowapata watu wasiomcha Mungu.
7Išgelbėjo teisųjį Lotą, varginamą nedorėlių palaido elgesio,
7Alimwokoa Loti, mtu mwema, ambaye alisikitishwa sana na mwenendo mbaya wa watu hao waasi.
8nes tarp jų gyvenantis šis teisusis diena iš dienos vargino savo teisią sielą, matydamas ir girdėdamas nedorus darbus.
8Loti aliishi miongoni mwa watu hao, na kwa siku nyingi moyo wake ulikuwa katika wasiwasi mkuu aliposikia matendo yao maovu.
9Viešpats žino, kaip išgelbėti pamaldžiuosius nuo išbandymo ir kaip išlaikyti nedoruosius teismo dienai ir bausmei,
9Kwa hiyo, basi, Bwana anajua jinsi ya kuwaokoa katika majaribu watu wanaomcha Mungu, na jinsi ya kuwaweka waovu katika adhabu hadi Siku ile ya hukumu,
10o ypač tuos, kurie pasiduoda nešvariems kūno geismams ir niekina viešpatystę. Įžūlūs ir savavaliai! Jie nesudreba, piktžodžiaudami šlovingiesiems,
10hasa wale wanaofuata tamaa mbaya za mwili na kupuuza mamlaka. Watu hao ni washupavu na wenye majivuno, huvitukana na hawaviheshimu viumbe vitukufu vya juu.
11tuo tarpu angelai, aukštesni jėga ir galia, Viešpaties akivaizdoje neištaria jiems piktžodiško kaltinimo.
11Lakini malaika, ambao wana uwezo na nguvu zaidi kuliko hao walimu wa uongo, hawawashtaki na kuwatukana hao mbele ya Bwana.
12Bet jie, kaip neprotingi gyvuliai, gimę sugavimui ir užmušimui, piktžodžiauja tam, ko nesupranta, ir pražus savo sugedime,
12Watu hao ambao hutukana chochote kile wasichoelewa, ni sawa na wanyama wasio na akili, ambao huzaliwa na baadaye hukamatwa na kuchinjwa! Wataangamizwa kutokana na uharibifu wao wenyewe,
13gaudami atpildą už nusikaltimus. Jie laiko pramoga lėbauti dienos metu. Jie susitepę ir iškrypę, smarkaudami savo apgaulėmis vaišinasi su jumis.
13na watalipwa mateso kwa mateso ambayo wameyasababisha. Furaha yao ni kufanya, tena mchana kabisa, chochote kinachotosheleza anasa zao za mwili. Hao ni fedheha na aibu tupu kwa jumuiya yenu wakati wanapojiunga nanyi katika karamu zenu, bali wakifurahia njia zao za udanganyifu.
14Jų akys kupinos svetimavimo, nepasotinamos nuodėmės. Jie suvedžioja svyruojančias sielas. Jų širdis išlavinta godumo. Jie prakeikimo vaikai.
14Macho yao yamejaa uzinzi na uwezo wao wa kutenda dhambi hauna kikomo. Huwaongoza watu walio dhaifu mpaka mitegoni. Mioyo yao imezoea kuwa na tamaa ya mali. Wapo chini ya laana ya Mungu!
15Palikę teisingą kelią, jie nuklydo ir pasuko Bosoro sūnaus Balaamo keliu, kuris pamėgo neteisumo atlygį,
15Wameiacha njia iliyonyoka, wakapotoka na kuifuata njia aliyofuata Balaamu, mwana wa Beori, ambaye alipendelea kupata faida kwa kufanya udanganyifu,
16tačiau buvo subartas dėl savo nedorybės: nebylus asilas prabilo žmogaus balsu ir sutrukdė pranašo beprotystę.
16akakaripiwa kwa ajili ya uovu wake. Punda ambaye hasemi alinena kwa sauti ya binadamu, akaukomesha wazimu wa huyo nabii.
17Jie yra šaltiniai be vandens, audros genami debesys; jiems skirta juodžiausia tamsybė per amžius.
17Watu hao ni kama chemchemi zilizokauka, kama mawingu yanayopeperushwa na tufani; makao yao waliyowekewa ni mahali pa giza kuu.
18Skelbdami išpūstas ir tuščias kalbas, kūno geismais ir pasileidimu jie suvilioja tuos, kurie yra vos pasprukę nuo gyvenančių paklydime.
18Husema maneno ya majivuno na yasiyo na maana, na kutumia tamaa zao mbaya za kimwili kuwatega wale ambao wamejitenga hivi karibuni na watu waishio katika udanganyifu.
19Jie žada šiems laisvę, patys būdami sugedimo vergai: juk nugalėtasis tampa nugalėjusiojo vergu.
19Huwaahidi watu wengine eti watakuwa huru, kumbe wao wenyewe ni watumwa wa upotovu--maana mtu ni mtumwa wa chochote kile kinachomtawala.
20Bet jeigu, ištrūkę iš pasaulio purvyno Viešpaties ir Gelbėtojo Jėzaus Kristaus pažinimu, jie ir vėl jame įklimpę pralaimi, tai jiems paskui darosi blogiau negu pirma.
20Watu waliokwisha ponyoka katika upotovu wa ulimwengu kwa kupata kumjua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, kisha wakakubali kunaswa na kutawaliwa tena na upotovu huo, hali yao itakuwa mbaya zaidi kuliko awali.
21Jiems būtų buvę geriau iš viso nepažinti teisumo kelio, negu, jį pažinus, nusigręžti nuo jiems duoto švento įsakymo.
21Ingalikuwa afadhali kwao kama wasingalijua kamwe njia hiyo ya uadilifu kuliko kujua na kisha kuiacha na kupoteza amri takatifu waliyopokea.
22Jiems nutiko, kaip sako teisinga patarlė: “Šuo sugrįžta prie savo vėmalo”, ir: “Išmaudyta kiaulė vėl voliojasi purvyne”.
22Ipo mithali isemayo: "Mbwa huyarudia matapishi yake mwenyewe," na nyingine isemayo: "Nguruwe aliyekwisha oshwa hugaagaa tena katika matope!" Ndivyo ilivyo kwao sasa.