1Simonas Petras, Jėzaus Kristaus tarnas ir apaštalas, gavusiems su mumis lygiai brangų tikėjimą mūsų Dievo ir Gelbėtojo Jėzaus Kristaus teisumu.
1Mimi Simoni Petro, mtumishi na mtume wa Yesu Kristo, nawaandikia ninyi ambao, kwa wema wake Mungu wetu, na Mwokozi Yesu Kristo, mmejaliwa imani ileile ya thamani kuu tuliyojaliwa sisi.
2Malonė ir ramybė tepadaugėja jums Dievo ir mūsų Viešpaties Jėzaus pažinimu.
2Nawatakieni neema na amani tele katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu.
3Jo dieviška jėga padovanojo mums viską, ko reikia gyvenimui ir dievotumui, per pažinimą To, kuris pašaukė mus šlove ir dorybe.
3Kwa uwezo wake wa kimungu, Mungu ametujalia mambo yote tunayohitaji, ili tuishi maisha ya kumcha Mungu kwa kumjua yeye aliyetuita tuushiriki utukufu na wema wake yeye mwenyewe.
4Drauge Jis davė mums be galo didžius bei brangius pažadus, kad per juos taptume dieviškosios prigimties dalininkais, ištrūkę iš sugedimo, kuris sklinda pasaulyje geiduliais.
4Kwa namna hiyo ametujalia zawadi kuu na za thamani ambazo alituahidia, ili kwa zawadi hizo mpate kuziepa kabisa tamaa mbaya zilizomo duniani, na mpate kuishiriki hali yake ya kimungu.
5Todėl, parodydami visą stropumą, praturtinkite savo tikėjimą dorybe, dorybę—pažinimu,
5Kwa sababu hiyo, fanyeni bidii ya kuongeza fadhila katika imani yenu: ongezeni elimu katika fadhila yenu,
6pažinimąsusivaldymu, susivaldymąištverme, ištvermęmaldingumu,
6kuwa na kiasi katika elimu yenu, uvumilivu katika kuwa na kiasi, uchaji wa Mungu katika uvumilivu wenu,
7maldingumąbrolybe, brolybę meile.
7udugu katika uchaji wenu, na mapendo katika udugu wenu.
8Jei šie dalykai jumyse gyvuoja ir tarpsta, jie neduoda jums apsileisti ir likti bevaisiams mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus pažinime.
8Mkiwa na sifa hizo zote kwa wingi, zitawawezesheni kuwa watendaji na kupata faida katika kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
9O kam jų trūksta, tas aklas ir trumparegis, užmiršęs, kad yra apvalytas nuo savo senųjų nuodėmių.
9Lakini mtu asiye na sifa hizo ni kipofu, hawezi kuona na amesahau kwamba alikwisha takaswa dhambi zake za zamani.
10Todėl, broliai, dar uoliau stenkitės sutvirtinti savąjį pašaukimą ir išrinkimą. Tai darydami, jūs niekada nesuklupsite.
10Kwa hiyo basi, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuufanya huo wito wenu mlioitiwa na Mungu uwe jambo la kudumu katika maisha yenu; kama mkiishi namna hiyo hamtaanguka kamwe.
11Šitaip dar plačiau atsivers jums įėjimas į amžinąją mūsų Viešpaties ir Gelbėtojo Jėzaus Kristaus karalystę.
11Kwa namna hiyo mtafaulu kupewa haki kamili ya kuingia katika Utawala wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.
12Todėl aš niekad nesiliausiu jums priminęs šiuos dalykus, nors jūs ir žinote juos ir esate sutvirtinti turimoje tiesoje.
12Kwa hiyo nitaendelea kuwakumbusheni daima mambo haya, ingawa mmekwisha yafahamu, na mko imara katika ukweli mlioupokea.
13Manau, kad teisinga, kol esu šioje palapinėje, žadinti jus paraginimais.
13Nadhani ni jambo jema kwangu, muda wote niishio hapa duniani, kuwapeni moyo na kuwakumbusheni juu ya mambo haya.
14Žinau, kad greitai ateis mano palapinės nugriovimo metas, kaip ir mūsų Viešpats Jėzus Kristus man apreiškė.
14Najua kwamba karibu nitauweka kando mwili huu wenye kufa, kama Bwana alivyoniambia waziwazi.
15Bet aš pasistengsiu, kad ir man iškeliavus, jūs kiekvienu metu galėtumėte tai prisiminti.
15Basi, nitajitahidi kuwapatieni njia ya kuyakumbuka mambo haya kila wakati, baada ya kufariki kwangu.
16Juk mes skelbėme jums mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus galybę ir atėjimą, ne mėgdžiodami gudriai išgalvotas pasakas, bet kaip savo akimis matę Jo didybę liudytojai.
16Wakati tulipowafundisheni juu ya ukuu wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, hatukutegemea hadithi tupu zisizo na msingi. Sisi tuliuona utukufu wake kwa macho yetu wenyewe.
17Jis gavo iš Dievo Tėvo garbę ir šlovę, kai iš tobulybės šlovės nuskambėjo Jam balsas: “Šitas yra mano mylimasis Sūnus, kuriuo Aš gėriuosi”.
17Sisi tulikuwapo wakati alipopewa heshima na kutukuzwa na Mungu Baba, wakati sauti ilipomjia kutoka kwake yeye aliye Utukufu Mkuu, ikisema: "Huyu ni Mwanangu mpenzi, nimependezwa naye."
18Tą balsą mes girdėjome aidint iš dangaus, kai buvome su Juo ant šventojo kalno.
18Tena, sisi wenyewe tulisikia sauti hiyo kutoka mbinguni wakati tulipokuwa pamoja naye juu ya ule mlima mtakatifu.
19Taip pat mes turime dar tvirtesnį pranašų žodį. Jūs gerai darote, laikydamiesi jo tarsi žiburio, šviečiančio tamsioje vietoje, kol išauš diena ir jūsų širdyse užtekės aušrinė žvaigždė.
19Tena, ujumbe wa manabii watuthibitishia jambo hilo; nanyi mwafanya vema kama mkiuzingatia, maana ni kama taa inayoangaza mahali penye giza mpaka Siku ile itakapopambazuka na mwanga wa nyota ya asubuhi utakapong'ara mioyoni mwenu.
20Pirmiausia žinokite, kad jokia Rašto pranašystė negali būti savavališkai aiškinama,
20Zaidi ya hayo, lakini, kumbukeni kwamba hakuna mtu yeyote awezaye kufafanua mwenyewe unabii ulio katika Maandiko Matakatifu.
21nes pranašystė niekada nėra atėjusi žmogaus valia, bet kalbėjo Šventosios Dvasios įkvėpti šventi Dievo žmonės.
21Maana hakuna ujumbe wa kinabii unaotokana na matakwa ya binadamu, bali watu walinena ujumbe wa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.