Lithuanian

Swahili: New Testament

1 Peter

5

1Jūsų vyresniuosius raginu aš, irgi vyresnysis, Kristaus kentėjimų liudytojas ir dalyvis šlovės, kuri bus apreikšta:
1wazee! Mimi niliye mzee ninalo ombi moja kwenu wazee wenzangu. Mimi mwenyewe nilishuhudia kwa macho yangu mateso ya Kristo na natumaini kuushiriki ule utukufu utakaofunuliwa. Mimi nawaombeni
2ganykite pas jus esančią Dievo kaimenę, prižiūrėdami ją ne iš prievartos, bet noriai, ne dėl nešvaraus pelno, bet uoliai,
2mlichunge lile kundi la Mungu mlilokabidhiwa, mlitunze si kwa kulazimika, bali kwa hiari kama atakavyo Mungu. Fanyeni kazi hiyo si kwa tamaa ya fedha, bali kwa moyo wenu wote.
3ne kaip viešpataujantys jums patikėtiems, bet būdami pavyzdžiu kaimenei.
3Msiwatawale kwa mabavu hao waliowekwa chini ya ulinzi wenu, bali muwe mfano kwa hilo kundi.
4O kai pasirodys Vyriausiasis Ganytojas, jūs gausite nevystantį šlovės vainiką.
4Na wakati Mchungaji Mkuu atakapotokea, ninyi mtapokea taji ya utukufu isiyofifia.
5Taip pat jūs, jaunesnieji, būkite klusnūs vyresniesiems. Ir visi, paklusdami vieni kitiems, apsivilkite nuolankumu, nes “Dievas išdidiems priešinasi, o nuolankiesiems teikia malonę”.
5Kadhalika nanyi vijana mnapaswa kujiweka chini ya mamlaka ya wazee. Ninyi nyote mnapaswa kuwa na unyenyekevu mpate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yasema: "Mungu huwapinga wenye majivuno, lakini huwajalia neema wanyenyekevu."
6Tad nusižeminkite po galinga Dievo ranka, kad Jis išaukštintų jus metui atėjus.
6Basi, nyenyekeeni chini ya mkono wa enzi wa Mungu, ili awainue wakati ufaao.
7Meskite ant Jo savo rūpesčius, nes Jis jumis rūpinasi.
7Mwekeeni matatizo yenu yote, maana yeye anawatunzeni.
8Būkite blaivūs ir budrūs, nes jūsų priešas velnias slankioja aplinkui kaip riaumojantis liūtas, tykodamas kurį nors praryti.
8Muwe macho; kesheni! Maana adui yenu, Ibilisi, huzungukazunguka kama simba angurumaye akitafuta mawindo.
9Pasipriešinkite jam tvirtu tikėjimu, žinodami, kad tokius pačius kentėjimus patiria jūsų broliai pasaulyje.
9Muwe imara katika imani na kumpinga, mkijua kwamba ndugu zenu pote duniani wanapatwa na mateso hayohayo.
10O visokeriopos malonės Dievas, pašaukęs mus į savo amžinąją šlovę Kristuje Jėzuje, pats jus, trumpai pakentėjusius, ištobulins, sutvirtins, sustiprins ir pastatys ant tvirto pagrindo.
10Lakini mkisha teseka muda mfupi, Mungu aliye asili ya neema yote na ambaye anawaiteni muushiriki utukufu wake wa milele katika kuungana na Kristo, yeye mwenyewe atawakamilisheni na kuwapeni uthabiti, nguvu na msingi imara.
11Jam šlovė ir valdžia per amžių amžius! Amen.
11Kwake uwe uwezo milele! Amina.
12Per Silvaną, ištikimąjį brolį,­tokiu jį laikau,­aš jums trumpai parašiau, ragindamas ir liudydamas, kad tai yra tikroji Dievo malonė, kurioje jūs stovite.
12Nimewaandikieni barua hii fupi kwa msaada wa Silwano, ndugu ambaye namjua na kumwamini. Nataka kuwapeni moyo na kushuhudia kwamba jambo hili ni neema ya Mungu kweli. Kaeni imara katika neema hiyo.
13Jus sveikina kartu išrinktoji Babilone ir mano sūnus Morkus.
13Jumuiya ya wenzenu walioteuliwa na Mungu hapa Babuloni wanawasalimuni. Vilevile mwanangu Marko anawasalimuni.
14Sveikinkite vieni kitus meilės pabučiavimu! Ramybė jums visiems, kurie esate Kristuje Jėzuje! Amen.
14Salimianeni kwa ishara ya upendo wa Kikristo. Nawatakieni amani ninyi mlio wake Kristo.