1Apaštalai ir broliai, kurie buvo Judėjoje, išgirdo, kad ir pagonys priėmė Dievo žodį.
1Mitume na ndugu kule Yudea walisikia kwamba watu wa mataifa mengine pia walikuwa wamelipokea neno la Mungu.
2Todėl, kai Petras atvyko į Jeruzalę, žydų kilmės tikintieji ėmė ginčytis su juo, sakydami:
2Basi, Petro aliporudi Yerusalemu, wale Wayahudi waumini waliopendelea watu wa mataifa mengine watahiriwe, walimlaumu wakisema:
3“Tu nuėjai pas neapipjaustytus vyrus ir su jais valgei!”
3"Wewe umekwenda kukaa na watu wasiotahiriwa na hata umekula pamoja nao!
4Tada Petras pradėjo jiems iš eilės aiškinti:
4Hapo Petro akawaeleza kinaganaga juu ya yale yaliyotendeka tangu mwanzo:
5“Aš kartą meldžiausi Jopės mieste ir Dvasios pagavoje mačiau regėjimą. Kažkoks indas, tarsi didžiulė marška, už keturių kampų leidžiama iš dangaus, nusileido prie manęs.
5"Siku moja nikiwa nasali mjini Yopa, niliona maono; niliona kitu kama shuka kubwa likishushwa chini kutoka mbinguni likiwa limeshikwa pembe zake nne, likawekwa kando yangu.
6Atidžiai įsižiūrėjęs, pamačiau jame keturkojų žemės gyvių, laukinių žvėrių, roplių ir padangės paukščių.
6Nilichungulia ndani kwa makini nikaona wanyama wenye miguu minne, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani.
7Ir išgirdau balsą, kuris man sakė: ‘Kelkis, Petrai, pjauk ir valgyk!’
7Kisha nikasikia sauti ikiniambia: Petro amka, chinja, ule.
8Aš atsakiau: ‘Jokiu būdu, Viešpatie! Dar niekada suteptas ir nešvarus maistas nebuvo mano burnoje’.
8Lakini mimi nikasema: La, Bwana; maana chochote kilicho najisi au kichafu hakijapata kamwe kuingia kinywani mwangu.
9Bet balsas iš dangaus prabilo antrą kartą: ‘Ką Dievas apvalė, tu nevadink suteptu!’
9Ile sauti ikasikika tena kutoka mbinguni: Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
10Taip atsitiko tris kartus, ir vėl viskas pakilo į dangų.
10Jambo hilo lilifanyika mara tatu, na mwishowe vyote vilirudishwa juu mbinguni.
11Ir štai prie namų, kuriuose aš buvau, tuojau atėjo trys vyrai. Jie buvo siųsti pas mane iš Cezarėjos.
11Ghafla, watu watatu waliokuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisarea waliwasili kwenye nyumba niliyokuwa nakaa.
12Dvasia man pasakė nė kiek nedvejojant keliauti su jais. Su manimi ėjo ir šitie šeši broliai, ir mes kartu atvykome į vieno vyro namus.
12Roho aliniambia niende pamoja nao bila kusita. Hawa ndugu sita waliandamana nami pia kwenda Kaisarea na huko tuliingia nyumbani mwa Kornelio.
13Jis mums papasakojo savo namuose regėjęs stovintį angelą, kuris jam liepė: ‘Nusiųsk į Jopę žmones ir pasikviesk Simoną, vadinamą Petru.
13Yeye alitueleza jinsi alivyokuwa amemwona malaika amesimama nyumbani mwake na kumwambia: Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
14Jis pasakys tau žodžius, kuriais išsigelbėsi tu ir visi tavo namai’.
14Yeye atakuambia maneno ambayo kwayo wewe na jamaa yako yote mtaokolewa.
15Kai pradėjau kalbėti, Šventoji Dvasia nužengė ant jų, kaip ir pradžioje ant mūsų.
15Na nilipoanza tu kuongea, Roho Mtakatifu aliwashukia kama alivyotushukia sisi pale awali.
16Tada prisiminiau Viešpaties žodžius: ‘Jonas krikštijo vandeniu, o jūs būsite pakrikštyti Šventąja Dvasia’.
16Hapo nilikumbuka yale maneno Bwana aliyosema: Yohane alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.
17Jeigu tad Dievas suteikė jiems tokią pačią dovaną, kaip ir mums, įtikėjusiems Viešpatį Jėzų Kristų, tai kas gi aš toks, kad galėčiau trukdyti Dievui?!”
17Basi, kama Mungu amewapa pia watu wa mataifa mengine zawadi ileile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, je, mimi ni nani hata nijaribu kumpinga Mungu?"
18Tai išgirdę, jie nusiramino ir šlovino Dievą, sakydami: “Vadinasi, Dievas ir pagonims suteikė atgailą, kad jie gyventų”.
18Waliposikia hayo, waliacha ubishi, wakamtukuza Mungu wakisema, "Mungu amewapa watu wa mataifa mengine nafasi ya kutubu na kuwa na uzima!"
19Išblaškytieji persekiojimo, kuris buvo kilęs dėl Stepono, nukeliavo į Finikiją, Kiprą ir Antiochiją. Jie pamokslavo žodį vien tik žydams.
19Kutokana na mateso yaliyotokea wakati Stefano alipouawa, waumini walitawanyika. Wengine walikwenda mpaka Foinike, Kupro na Antiokia wakihubiri ule ujumbe kwa Wayahudi tu.
20Kai kurie iš jų, būtent kipriečiai ir kirėniečiai, atvykę į Antiochiją, kreipėsi ir į graikus, skelbdami Viešpatį Jėzų.
20Lakini baadhi ya waumini waliotoka Kupro na Kurene, walikwenda Antiokia wakautangaza huo ujumbe kwa watu wa mataifa mengine wakiwahubiria ile Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
21Viešpaties ranka buvo su jais: didelis žmonių skaičius įtikėjo ir atsivertė į Viešpatį.
21Bwana aliwasaidia na idadi kubwa ya watu iliamini na kumgeukia Bwana.
22Žinia apie juos pasiekė Jeruzalės bažnyčios ausis, ir ji išsiuntė Barnabą į Antiochiją.
22Habari ya jambo hilo ikasikika kwa lile kanisa la Yerusalemu. Hivyo wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23Atvykęs ir pamatęs Dievo malonę, jis apsidžiaugė ir visus ragino ryžtinga širdimi pasilikti su Viešpačiu.
23Alipofika huko na kuona jinsi Mungu alivyowaneemesha wale watu, alifurahi na kuwahimiza wote wadumu katika uaminifu wao kwa Bwana.
24Mat jis buvo geras vyras, pilnas Šventosios Dvasios ir tikėjimo. Ir Viešpačiui prisidėjo didelis būrys.
24Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana.
25Tada Barnabas nukeliavo į Tarsą ieškoti Sauliaus
25Kisha, Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Saulo
26ir, radęs jį, atsivedė į Antiochiją. Jiedu ištisus metus darbavosi bažnyčioje ir mokė gausų būrį. Antiochijoje pirmą kartą imta vadinti mokinius “krikščionimis”.
26Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. Huko Antiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.
27Tomis dienomis iš Jeruzalės į Antiochiją atvyko pranašų.
27Wakati huohuo, manabii kadhaa walikuja Antiokia kutoka Yerusalemu.
28Vienas iš jų, vardu Agabas, Dvasios įkvėptas, išpranašavo didelį badą, kuris ištiksiąs visą pasaulį. Ir badas atėjo, Klaudijui valdant.
28Basi, mmoja wao aitwaye Agabo alisimama, na kwa uwezo wa Roho akabashiri kwamba kutakuwa na njaa kubwa katika nchi yote (Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa akitawala).
29Tada mokiniai, kiekvienas pagal savo išteklius, nusprendė nusiųsti paramą Jeruzalės broliams.
29Wale wanafunzi waliamua kila mmoja kwa kadiri ya uwezo wake apeleke chochote ili kuwasaidia wale ndugu waliokuwa wanaishi Yudea.
30Jie taip ir padarė, per Barnabą bei Saulių nusiųsdami tai vyresniesiems.
30Basi, wakafanya hivyo na kupeleka mchango wao kwa wazee wa kanisa kwa mikono ya Barnaba na Saulo.