Lithuanian

Swahili: New Testament

Acts

12

1Tuo metu karalius Erodas pakėlė ranką prieš kai kuriuos bažnyčios žmones.
1Karibu wakati huohuo, mfalme Herode alianza kuwatesa baadhi ya Wakristo.
2Jis nukirsdino kalaviju Jokūbą, Jono brolį.
2Alimwua kwa upanga Yakobo ndugu yake Yohane.
3Pamatęs, kad tai patinka žydams, įsakė suimti ir Petrą. Buvo Neraugintos duonos dienos.
3Alipoona kuwa kitendo hiki kiliwapendeza Wayahudi, aliendelea, akamkamata Petro. (Hiyo ilifanyika wakati wa sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu.)
4Suėmęs jį, įmesdino į kalėjimą ir pavedė saugoti keturgubai sargybai po keturis kareivius, o po Paschos ketino išvesti jį prieš minią.
4Baada ya kutiwa nguvuni, Petro alifungwa gerezani, akawekwa chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari wannewanne. Herode alikusudia kumtoa hadharani baada ya sikukuu ya Pasaka.
5Taigi Petras buvo uždarytas kalėjime. O bažnyčia nepaliaujamai meldėsi už jį Dievui.
5Basi, Petro alipokuwa gerezani, kanisa lilikuwa linamwombea kwa Mungu kwa moyo.
6Paskutinę naktį prieš Erodui išvedant Petrą, tas, supančiotas dviem grandinėmis, miegojo tarp dviejų kareivių. Prie durų kalėjimą saugojo sargybiniai.
6Usiku, kabla ya siku ile ambayo Herode angemtoa Petro hadharani, Petro alikuwa amelala kati ya askari wawili. Alikuwa amefungwa minyororo miwili, na walinzi walikuwa wanalinda lango la gereza.
7Ir štai ten atsirado Viešpaties angelas, ir kamerą nutvieskė šviesa. Jis sudavė Petrui į šoną ir žadindamas tarė: “Kelkis greičiau!” Ir nukrito jam grandinės nuo rankų.
7Ghafla, malaika wa Bwana akasimama karibu naye na mwanga ukaangaza kile chumba cha gereza. Malaika akamgusa akisema, "Amka upesi!" Mara ile minyororo ikaanguka kutoka katika mikono yake.
8Angelas kalbėjo toliau: “Susijuosk ir apsiauk sandalus!” Jis taip ir padarė. Angelas tęsė: “Užsimesk apsiaustą ir eik paskui mane!”
8Malaika akamwambia, "Jifunge mshipi wako, vaa viatu vyako." Akafanya hivyo. Kisha huyo malaika akamwambia, "Vaa koti lako, unifuate."
9Petras išėjo ir sekė paskui jį, nesuvokdamas, kad angelo veiksmai tikri, nes jis tarėsi matąs regėjimą.
9Petro akamfuata nje lakini hakujua kama hayo yaliyofanywa na huyo malaika yalikuwa ya kweli; alidhani alikuwa anaota ndoto.
10Praėję pro pirmą ir antrą sargybą, jie prisiartino prie geležinių vartų į miestą, kurie savaime atsidarė. Išėję pro juos, jie leidosi tolyn viena gatve. Staiga šalia ėjęs angelas nuo jo pasitraukė.
10Walipita kituo cha kwanza cha ulinzi na cha pili, halafu wakafika kwenye mlango wa chuma wa kuingilia mjini. Huo mlango ukawafungukia wenyewe, nao wakatoka nje. Wakawa wanatembea katika barabara moja na mara yule malaika akamwacha Petro peke yake.
11Petras atsipeikėjęs tarė: “Dabar tikrai žinau, kad Viešpats atsiuntė savo angelą ir išvadavo mane iš Erodo rankų ir nuo viso to, ko tikėjosi žydų minia”.
11Hapo ndipo Petro alipotambua yaliyotukia, akasema, "Sasa najua kwa hakika kwamba Bwana amemtuma malaika wake akaniokoa kutoka katika mkono wa Herode na kutoka katika mambo yale yote watu wa Israeli waliyotazamia."
12Tai supratęs, jis atėjo prie Morkumi vadinamo Jono motinos Marijos namų, kuriuose daug susirinkusiųjų meldėsi.
12Alipotambua hivyo alikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Maria mama yake Yohane aitwaye Marko. Humo watu wengi walikuwa wamekusanyika wakisali.
13Petrui beldžiantis į vartų duris, tarnaitė, vardu Rodė, atėjo paklausti, kas ten.
13Petro alibisha mlango wa nje na mtumishi mmoja msichana aitwaye Roda, akaenda mlangoni kuitikia.
14Pažinusi Petro balsą, ji iš džiaugsmo pamiršo atidaryti vartus, bet nubėgo vidun ir pranešė, jog Petras stovįs už vartų.
14Huyo msichana aliitambua sauti ya Petro akafurahi mno, hata badala ya kuufungua ule mlango, akakimbilia ndani na kuwaambia kwamba Petro alikuwa amesimama nje mlangoni.
15Jie jai sakė: “Tu pakvaišai!” Bet ji tvirtino savo. Tada jie tarė: “Tai jo angelas”.
15Wakamwambia yule msichana, "Una wazimu!" Lakini yeye akasisitiza kwamba ilikuwa kweli. Nao wakamwambia, "Huyo ni malaika wake."
16Tuo tarpu Petras toliau beldė. Atidarę jie pamatė Petrą ir nustėro.
16Wakati huo Petro alikuwa anaendelea kupiga hodi. Mwishowe walifungua mlango, wakamwona, wakashangaa.
17Ranka davęs ženklą laikytis tyliai, jis jiems papasakojo, kaip Viešpats išvedė jį iš kalėjimo. Jis dar pridūrė: “Praneškite apie tai Jokūbui ir kitiems broliams”. Ir išėjęs jis nuėjo į kitą vietą.
17Petro aliwaashiria kwa mkono wakae kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Kisha akawaambia watoe taarifa ya jambo hilo kwa Yakobo na wale ndugu wengine, halafu akatoka akaenda mahali pengine.
18Išaušus dienai tarp kareivių kilo nemenkas sąmyšis dėl to, kas galėję nutikti Petrui.
18Kulipokucha, ulitokea wasiwasi mkubwa kati ya wale askari kuhusu yaliyokuwa yamempata Petro.
19Erodas, paieškojęs jo ir neradęs, ištardė sargybinius ir įsakė nubausti juos mirtimi. Po to iš Judėjos nuvyko į Cezarėją ir ten pasiliko.
19Herode aliamuru ufanywe msako lakini hawakuweza kumpata. Hivyo aliamuru wale askari wahojiwe, akatoa amri wauawe. Halafu akatoka huko Yudea akaenda Kaisarea ambako alikaa.
20Erodas nirto ant Tyro ir Sidono gyventojų. Bet jie susitarę atvyko pas jį ir, palenkę savo pusėn karaliaus rūmininką Blastą, prašė taikos, nes jų kraštas maitinosi iš karaliaus.
20Herode alikasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Lakini wao walimpelekea wajumbe. Nao wakafaulu kwanza kumpata Blasto awe upande wao. Blasto alikuwa msimamizi mkuu wa ikulu ya mfalme. Kisha, wakamwendea Herode wakamwomba kuwe na amani, kwa maana nchi yao ilitegemea nchi ya mfalme kwa chakula.
21Nustatytą dieną Erodas, apsivilkęs karališkais drabužiais, atsisėdo į sostą ir sakė jiems prakalbą.
21Siku moja iliyochaguliwa, Herode akiwa amevaa mavazi rasmi na kuketi katika kiti cha kifalme aliwahutubia watu.
22Liaudis ėmė šaukti: “Tai dievo, ne žmogaus balsas!”
22Wale watu walimpigia kelele za shangwe wakisema, "Hii ni sauti ya mungu, si ya mtu."
23Ir beregint jį ištiko Viešpaties angelas, kad neatidavė Dievui garbės. Ir jis mirė, kirminų suėstas.
23Papo hapo malaika wa Bwana akamwangusha Herode chini kwa sababu hakumpa Mungu hizo sifa. Akaliwa na wadudu, akafa.
24O Viešpaties žodis augo ir plito.
24Neno la Mungu likazidi kuenea na kukua.
25Barnabas ir Saulius, atlikę savo uždavinį ir paėmę su savimi Joną, vadinamą Morkumi, sugrįžo iš Jeruzalės.
25Baada ya Barnaba na Saulo kutekeleza shughuli zao, walitoka tena Yerusalemu wakamchukua Yohane aitwaye pia Marko.