1Antiochijos bažnyčioje buvo pranašų ir mokytojų: Barnabas, Simeonas, pravarde Juodasis, Lucijus Kirėnietis, Manaenas, augęs kartu su tetrarchu Erodu, ir Saulius.
1Katika kanisa la Antiokia kulikuwa na watu wengine waliokuwa manabii na walimu; miongoni mwao akiwa Barnaba, Simoni aitwaye pia Mweusi, Lukio wa Kurene, Manaeni ambaye alikuwa amelelewa pamoja na mfalme Herode, na Saulo.
2Kartą, kai jie tarnavo Viešpačiui ir pasninkavo, Šventoji Dvasia pasakė: “Išskirkite man Barnabą ir Saulių darbui, kuriam Aš juos pašaukiau”.
2Walipokuwa wanafanya ibada yao kwa Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema: "Niteulieni Barnaba na Saulo kwa ajili ya kazi niliyowaitia."
3Tuomet jie pasninkavo ir meldėsi, ir, uždėję ant jų rankas, išleido.
3Basi, baada ya kusali na kufunga zaidi, wakawawekea mikono, wakawaacha waende zao.
4Šventosios Dvasios pasiųsti, jie nukeliavo į Seleukiją, o iš ten laivu pasiekė Kiprą.
4Basi, Barnaba na Saulo walipokwisha tumwa na Roho Mtakatifu, walishuka hadi Seleukia, na kutoka huko walipanda meli hadi kisiwa cha Kupro.
5Atvykę į Salaminą, jie pamokslavo Dievo žodį žydų sinagogose. Jiems talkino Jonas.
5Walipofika Salami walihubiri neno la Mungu katika masunagogi ya Kiyahudi. Yohane (Marko) alikuwa msaidizi wao.
6Perėję visą salą iki Pafo, jie susitiko vieną magą, netikrą pranašą žydą, vardu Barjėzų,
6Walitembea toka upande mmoja wa kisiwa mpaka Pafo upande wa pili, na huko walimkuta mchawi mmoja Myahudi aitwaye Baryesu ambaye alijisingizia kuwa nabii.
7kuris buvo su prokonsulu Sergijumi Pauliumi, išmintingu vyru. Šis, pasikvietęs Barnabą ir Saulių, norėjo pasiklausyti Dievo žodžio.
7Huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mkuu wa kile kisiwa, ambaye alikuwa mtu mwelewa sana. Sergio Paulo aliwaita Barnaba na Saulo ili asikie neno la Mungu.
8Bet Elimasmagas (toks šito žodžio vertimas)jiems priešinosi, stengdamasis atitraukti prokonsulą nuo tikėjimo.
8Lakini huyo mchawi Elima (kama alivyokuwa anaitwa kwa Kigiriki), alijaribu kuwapinga ili kumzuia huyo mkuu wa kisiwa asije akaigeukia imani ya Kikristo.
9Tada Saulius, kitaip vadinamas Pauliumi, Šventosios Dvasios kupinas, įdėmiai pažvelgė į jį
9Basi, Saulo ambaye aliitwa pia Paulo, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alimkodolea macho huyo mchawi,
10ir tarė: “Ak tu, visokių klastų bei piktybių pilnas velnio vaike! Tu, teisumo prieše! Ar nesiliausi kraipęs tiesių Viešpaties kelių?
10akasema, "Mdanganyifu wa kupindukia na mlaghai wewe! Wewe ni mtoto wa Ibilisi! Wewe ni adui wa chochote kile kilicho cha kweli; hukomi hata mara moja kujaribu kuzipotosha njia za Bwana zilizonyoka.
11Dabar štai tave ištiks Viešpaties ranka: tu tapsi aklas ir kurį laiką neregėsi saulės”. Ir tučtuojau užgulė jį migla ir tamsa, ir jis ėmė graibytis aplink, ieškodamas, kas jam ištiestų ranką.
11Sasa, mkono wa Bwana utakuadhibu: utakuwa kipofu na hutaweza kuuona mwanga wa jua kwa kitambo." Mara kila kitu kikawa kama ukungu na giza kwake, akaanza kwenda huku na huku akitafuta mtu wa kumshika mkono amwongoze.
12Tai pamatęs, prokonsulas įtikėjo, apstulbintas Viešpaties mokslo.
12Yule mkuu wa kisiwa alipoona hayo, aliongoka akawa muumini; akastaajabia sana mafundisho aliyosikia juu ya Bwana.
13Išplaukę iš Pafo, Paulius ir jo palydovai atvyko į Pergę, Pamfilijoje. Čia Jonas pasitraukė nuo jų ir sugrįžo į Jeruzalę.
13Kutoka Pafo, Paulo na wenzake walipanda meli wakaenda hadi Perga katika Pamfulia; lakini Yohane (Marko) aliwaacha, akarudi Yerusalemu.
14O jie, išvykę iš Pergės, atkeliavo į Pisidijos Antiochiją. Sabato dieną nuėjo į sinagogą ir ten susėdo.
14Lakini wao waliendelea na safari toka Pisga hadi mjini Antiokia Pisidia. Siku ya Sabato waliingia ndani ya Sunagogi, wakakaa.
15Po Įstatymo ir Pranašų skaitymo sinagogos vadovai kreipėsi į juos: “Vyrai broliai, jei turite paskatinimo žodį tautiečiams, tarkite!”
15Baada ya masomo katika kitabu cha Sheria ya Mose na katika maandiko ya manabii, wakuu wa lile sunagogi waliwapelekea ujumbe huu: "Ndugu, kama mnalo jambo la kuwaambia watu ili kuwapa moyo, semeni."
16Tada Paulius atsistojo ir, davęs ranka ženklą nutilti, prabilo: “Izraelio vyrai ir Dievo bijantys žmonės, paklausykite!
16Basi, Paulo alisimama, akatoa ishara kwa mkono, akaanza kuongea: "Wananchi wa Israeli na wengine wote mnaomcha Mungu, sikilizeni!
17Šios Izraelio tautos Dievas išsirinko mūsų tėvus, išaukštino juos, gyvenančius kaip ateivius Egipto šalyje, ir iškelta ranka išvedė juos iš Egipto.
17Mungu wa taifa hili la Israeli aliwateua babu zetu na kuwafanya wawe taifa kubwa walipokuwa ugenini kule Misri. Mungu aliwatoa huko kwa uwezo wake mkuu.
18Apie keturiasdešimt metų Jis pakentė jų elgesį dykumoje,
18Aliwavumilia kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani.
19paskui, išnaikinęs septynias tautas Kanaane, išdalino jiems anų žemę.
19Aliyaangamiza mataifa ya nchi ya Kanaani akawapa hao watu wake ile nchi kuwa mali yao.
20Po to per keturis šimtus penkiasdešimt metų davė teisėjus iki pranašo Samuelio.
20Miaka mia nne na hamsini ilipita, halafu akawapatia waamuzi wawaongoze mpaka wakati wa nabii Samweli.
21Tuo laiku jie ėmė prašyti karaliaus, ir Dievas jiems davė Saulių, Kišo sūnų, Benjamino giminės vyrą, keturiasdešimčiai metų.
21Hapo wakapendelea kuwa na mfalme, na Mungu akawapa Saulo, mtoto wa Kishi wa kabila la Benyamini, awe mfalme wao kwa muda wa miaka arobaini.
22Pašalinęs jį, Jis pakėlė jiems karaliumi Dovydą, apie kurį liudydamas pasakė: ‘Radau Dovydą, Jesės sūnų, vyrą pagal savo širdį, kuris įvykdys visus mano norus’.
22Baada ya kumwondoa Saulo, Mungu alimteua Daudi kuwa mfalme wao. Mungu alionyesha kibali chake kwake akisema: Nimemwona Daudi mtoto wa Yese; ni mtu anayepatana na moyo wangu; mtu ambaye atatimiza yale yote ninayotaka kuyatenda.
23Iš jo palikuonių, kaip buvo žadėjęs, Dievas iškėlė Izraeliui Gelbėtoją Jėzų.
23Kutokana na ukoo wake mtu huyu, Mungu, kama alivyoahidi, amewapelekea watu wa Israeli Mwokozi, ndiye Yesu.
24Prieš Jam ateinant, Jonas skelbė atgailos krikštą visai Izraelio tautai.
24Kabla ya kuja kwake Yesu, Yohane alimtangulia akiwahubiria watu wote wa Israeli kwamba ni lazima watubu na kubatizwa.
25Baigdamas gyvenimo kelią, Jonas pasakė: ‘Kuo jūs mane laikote? Aš nesu Jis. Bet štai po manęs ateina Tas, kuriam aš nevertas atrišti kojų apavo’.
25Yohane alipokuwa anamaliza ujumbe wake aliwaambia watu: Mnadhani mimi ni nani? Mimi si yule mnayemtazamia. Huyo anakuja baada yangu na mimi sistahili hata kuzifungua kamba za viatu vyake.
26Vyrai broliai, Abraomo giminės sūnūs ir čia esantys Dievo bijantys žmonės! Tai jums atsiųstas šis išgelbėjimo žodis.
26"Ndugu, ninyi mlio watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wengine wote mnaomcha Mungu! Ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
27Nes Jeruzalės gyventojai ir jų vyresnieji nepažino Jo ir pasmerkdami įvykdė pranašų žodžius, skaitomus kiekvieną sabatą.
27Kwa maana wenyeji wa Yerusalemu na wakuu wao hawakumtambua yeye kuwa Mwokozi. Wala hawakuelewa maneno ya manabii yanayosomwa kila Sabato. Hata hivyo, waliyafanya maneno ya manabii yatimie kwa kumhukumu Yesu adhabu ya kifo.
28Nors nerado Jame jokios mirties vertos kaltės, jie reikalavo iš Piloto, kad Jis būtų nužudytas.
28Ingawa hawakumpata na hatia inayostahili auawe, walimwomba Pilato amhukumu auawe.
29Išpildę visa, kas buvo apie Jį parašyta, nuėmė Jį nuo medžio ir paguldė į kapą.
29Na baada ya kutekeleza yote yaliyokuwa yameandikwa kumhusu yeye, walimshusha kutoka msalabani, wakamweka kaburini.
30Bet Dievas Jį prikėlė iš numirusių.
30Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
31Jis per daugelį dienų rodėsi tiems, kurie buvo su Juo atėję iš Galilėjos į Jeruzalę. Jie yra Jo liudytojai žmonėms.
31Naye, kwa siku nyingi aliwatokea wale waliofuatana naye kutoka Galilaya mpaka Yerusalemu. Hao ndio walio sasa mashahidi wake kwa watu wa Israeli.
32Ir mes jums skelbiame Gerąją naujieną: tėvams duotąjį pažadą
32Sisi tumekuja hapa kuwaleteeni Habari Njema: jambo lile Mungu alilowaahidia babu zetu amelitimiza sasa kwa ajili yetu sisi tulio wajukuu wao kwa kumfufua Yesu kutoka wafu.
33Dievas įvykdė mums, jų vaikams, prikeldamas Jėzų, kaip ir parašyta antroje psalmėje: ‘Tu esi mano Sūnus, šiandien Aš pagimdžiau Tave!’
33Kama ilivyoandikwa katika zaburi ya pili: Wewe ni Mwanangu, mimi leo nimekuwa baba yako.
34O kad Jį prikėlė iš numirusių ir kad Jis neturėjo supūti, Dievas buvo taip nusakęs: ‘Aš ištesėsiu šventus bei tikrus pažadus Dovydui’.
34Na juu ya kumfufua kutoka wafu, asipate tena kurudi huko na kuoza, Mungu alisema hivi: Nitakupa baraka takatifu na za kweli nilizomwahidia Daudi.
35Todėl ir kitoje vietoje sakoma: ‘Tu neleisi savo Šventajam matyti supuvimo’.
35Naam, na katika sehemu nyingine za zaburi asema: Hutamwacha Mtakatifu wako aoze.
36Juk Dovydas, patarnavęs savajai kartai pagal Dievo valią, užmigo, buvo palaidotas prie savo tėvų ir supuvo.
36Sasa, Daudi mwenyewe alitimiza mapenzi ya Mungu wakati wake; kisha akafa na kuzikwa karibu na wazee wake, na mwili wake ukaoza.
37O Tas, kurį Dievas prikėlė, nesupuvo.
37Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.
38Taigi tebūnie jums žinoma, vyrai broliai, kad per Jį jums skelbiamas nuodėmių atleidimas.
38Jueni wazi, ndugu zangu, kwamba ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu kwa njia ya Yesu Kristo;
39Ir kiekvienas, kuris tiki, išteisinamas Juo nuo viso to, nuo ko nepajėgė jūsų išteisinti Mozės Įstatymas.
39na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya Sheria ya Mose.
40Tad saugokitės, kad jums nepritaptų, kas pasakyta Pranašuose:
40Jihadharini basi, msije mkapatwa na yale yaliyosemwa na manabii:
41‘Žiūrėkite, niekintojai, stebėkitės ir pranykite! Nes Aš darau darbą jūsų dienomis, darbą, kuriuo nepatikėsite, jei kas jums pasakos’ ”.
41Sikilizeni enyi wenye madharau, shangaeni mpotee! Kwa maana kitu ninachofanya sasa, nyakati zenu, ni kitu ambacho hamtakiamini hata kama mtu akiwaelezeni."
42Žydams išeinant iš sinagogos, pagonys prašė, kad ir kitą sabatą būtų kalbama apie tuos dalykus.
42Paulo na Barnaba walipokuwa wanatoka katika ile sunagogi, wale watu waliwaalika waje tena siku ya Sabato iliyofuata, waongee zaidi juu ya mambo hayo.
43Sinagogos susirinkimui pasibaigus, daugelis žydų ir pamaldžių prozelitų sekė Paulių ir Barnabą, kurie, kalbėdami jiems, įtikinėjo pasilikti Dievo malonėje.
43Mkutano huo ulipomalizika, Wayahudi wengi na watu wa mataifa mengine waliokuwa wameongokea dini ya Kiyahudi waliwafuata Paulo na Barnaba. Hao mitume waliongea nao, wakawatia moyo waendelee kuishi wakitegemea neema ya Mungu.
44Kitą sabatą beveik visas miestas susirinko pasiklausyti Dievo žodžio.
44Siku ya Sabato iliyofuata, karibu kila mtu katika ule mji alikuja kusikiliza neno la Bwana.
45Išvydusius tokias minias žydus apėmė pavydas, ir jie piktžodžiaudami ėmė prieštarauti tam, ką kalbėjo Paulius.
45Lakini Wayahudi walipoliona hilo kundi la watu walijaa wivu, wakapinga alichokuwa anasema Paulo na kumtukana.
46Bet Paulius ir Barnabas drąsiai pasakė: “Pirmiausia jums turėjo būti skelbiamas Dievo žodis. Bet kadangi jūs Jį atmetate ir patys laikote save nevertais amžinojo gyvenimo, tai štai mes kreipiamės į pagonis.
46Hata hivyo, Paulo na Barnaba waliongea kwa uhodari zaidi, wakasema, "Ilikuwa ni lazima neno la Mungu liwafikieni ninyi kwanza; lakini kwa kuwa mmelikataa na kujiona hamstahili uzima wa milele, basi, tunawaacheni na kuwaendea watu wa mataifa mengine.
47Nes taip mums liepė Viešpats: ‘Paskyriau Tave, kad būtum šviesa pagonims, kad būtumei išgelbėjimu iki pat žemės pakraščių’ ”.
47Maana Bwana alituagiza hivi: Nimekuteua wewe uwe mwanga kwa mataifa, uwe njia ya wokovu kwa ulimwengu wote."
48Tai girdėdami, pagonys džiaugėsi ir šlovino Viešpaties žodį; ir įtikėjo visi skirtieji amžinajam gyvenimui.
48Watu wa mataifa mengine waliposikia jambo hilo walifurahi, wakausifu ujumbe wa Mungu; na wale waliokuwa wamechaguliwa kupata uzima wa milele, wakawa waumini.
49Ir Viešpaties žodis pasklido po visą kraštą.
49Neno la Bwana likaenea kila mahali katika sehemu ile.
50Bet žydai, sukurstę pamaldžias bei gerbiamas moteris ir įtakingus miesto piliečius, sukėlė Pauliaus ir Barnabo persekiojimą ir išvijo juos iš savo žemių.
50Lakini Wayahudi waliwachochea wanawake wa tabaka ya juu wa mataifa mengine ambao walikuwa wacha Mungu, na wanaume maarufu wa mji huo. Wakaanza kuwatesa Paulo na Barnaba, wakawafukuza kutoka katika eneo lao.
51O tie, nusikratę prieš juos nuo kojų dulkes, atvyko į Ikonijų.
51Basi, mitume wakayakung'uta mavumbi yaliyokuwa katika miguu yao kama onyo, kisha wakaenda Ikonio.
52Mokiniai buvo pilni džiaugsmo ir Šventosios Dvasios.
52Lakini hao wafuasi walikuwa wamejaa furaha na Roho Mtakatifu.