Lithuanian

Swahili: New Testament

Acts

14

1Taip pat atsitiko ir Ikonijuje: jie nuėjo į žydų sinagogą ir kalbėjo taip, kad įtikėjo didelė minia žydų ir graikų.
1Kule Ikonio, mambo yalikuwa kama yalivyokuwa kule Antiokia; Paulo na Barnaba walikwenda katika sunagogi la Wayahudi wakaongea kwa uhodari hata Wayahudi wengi na Wagiriki wakawa waumini.
2Bet tikėjimui nepaklusę žydai sukurstė pagonis prieš brolius.
2Lakini Wayahudi wengine waliokataa kuwa waumini walichochea na kutia chuki katika mioyo ya watu wa mataifa mengine ili wawapinge hao ndugu.
3Tačiau jie ten išbuvo daug laiko ir drąsiai kalbėjo Viešpatyje, kuris liudijo savo malonės žodžius ir per jų rankas darė ženklus ir stebuklus.
3Paulo na Barnaba waliendelea kukaa huko kwa muda mrefu. Waliongea kwa uhodari juu ya Bwana, naye Bwana akathibitisha ukweli wa ujumbe walioutoa juu ya neema yake, kwa kuwawezesha kutenda miujiza na maajabu.
4Miesto gyventojai suskilo: vieni buvo už žydus, kiti už apaštalus.
4Watu wa mji huo waligawanyika: wengine waliwaunga mkono Wayahudi, na wengine walikuwa upande wa mitume.
5Kai pagonys ir žydai su savo vyresnybe susiruošė juos išniekinti ir užmėtyti akmenimis,
5Mwishowe, baadhi ya watu wa mataifa mengine na Wayahudi, wakishirikiana na wakuu wao, waliazimu kuwatendea vibaya hao mitume na kuwapiga mawe.
6jie sužinoję pabėgo į Likaonijos miestus Listrą ir Derbę bei jų apylinkes.
6Mitume walipogundua jambo hilo, walikimbilia Lustra na Derbe, miji ya Lukaonia, na katika sehemu za jirani,
7Ten jie skelbė Evangeliją.
7wakawa wanahubiri Habari Njema huko.
8Listroje gyveno vienas vyras nesveikomis kojomis. Jis buvo luošas nuo pat gimimo, niekada nė žingsnio nežengęs.
8Kulikuwa na mtu mmoja huko Lustra ambaye alikuwa amelemaa miguu tangu kuzaliwa, na alikuwa hajapata kutembea kamwe.
9Jis klausėsi Pauliaus kalbant, o šis įdėmiai pažvelgė į jį ir, pamatęs jį turint tikėjimą, kad būtų pagydytas,
9Mtu huyo alikuwa anamsikiliza Paulo alipokuwa anahubiri. Paulo alimtazama kwa makini, na alipoona kuwa alikuwa na imani ya kuweza kuponywa,
10garsiu balsu pasakė: “Atsistok tiesiai ant savo kojų!” Tas pašoko ir ėmė vaikščioti.
10akasema kwa sauti kubwa, "Simama wima kwa miguu yako!" Huyo mtu aliyelemaa akainuka ghafla, akaanza kutembea.
11Minia, pamačiusi, ką Paulius padarė, pradėjo garsiai likaoniškai šaukti: “Dievai, pasivertę žmonėmis, nužengė pas mus!”
11Umati wa watu walipoona alichofanya Paulo, ulianza kupiga kelele kwa lugha ya Kilukaonia: "Miungu imetujia katika sura za binadamu!"
12Barnabą jie vadino Dzeusu, o Paulių­Hermiu, nes jis vadovavo kalbai.
12Barnaba akaitwa Zeu, na Paulo, kwa vile yeye ndiye aliyekuwa anaongea, akaitwa Herme.
13Priešais jų miestą esančios Dzeuso šventyklos kunigas atvarė prie vartų jaučių su vainikais ir norėjo kartu su minia juos paaukoti.
13Naye kuhani wa hekalu la Zeu lililokuwa nje ya mji akaleta fahali na shada za maua mbele ya mlango mkuu wa mji, na pamoja na ule umati wa watu akataka kuwatambikia mitume.
14Sužinoję apaštalai Barnabas ir Paulius perplėšė savo drabužius ir puolė į minią,
14Barnaba na Paulo walipopata habari hiyo waliyararua mavazi yao na kukimbilia katika lile kundi la watu wakisema kwa sauti kubwa:
15šaukdami: “Vyrai, ką darote?! Juk mes tokie patys žmonės kaip ir jūs. Ir mes jums skelbiame Gerąją naujieną, kad nuo šių tuštybių atsiverstumėte į gyvąjį Dievą, ‘kuris sutvėrė dangų ir žemę, jūrą ir visa, kas juose yra’.
15"Ndugu, kwa nini mnafanya mambo hayo? Sisi pia ni binadamu kama ninyi. Na, tuko hapa kuwahubirieni Habari Njema, mpate kuziacha hizi sanamu tupu, mkamgeukie Mungu aliye hai, Mungu aliyeumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo.
16Praėjusiais amžiais Jis leido eiti visoms tautoms savais keliais.
16Zamani Mungu aliruhusu kila taifa lifanye lilivyopenda.
17Tačiau Jis nepaliko savęs nepaliudyto, darydamas gera, duodamas mums lietaus iš dangaus ir vaisingų metų, pripildydamas mūsų širdis maisto ir džiaugsmo”.
17Hata hivyo, Mungu hakuacha kujidhihirisha kwa mambo mema anayowatendea: huwanyeshea mvua toka angani, huwapa mavuno kwa wakati wake, huwapa chakula na kuijaza mioyo yenu furaha."
18Tai dėstydami, jiedu šiaip ne taip sulaikė minią, kad jiems neaukotų.
18Ingawa walisema hivyo haikuwa rahisi kuwazuia wale watu wasiwatambikie.
19Bet iš Antiochijos ir Ikonijaus atvyko žydai ir, perkalbėję žmones, užmėtė Paulių akmenimis ir išvilko už miesto, palaikę jį mirusiu.
19Lakini Wayahudi kadhaa walikuja kutoka Antiokia na Ikonio, wakawafanya watu wajiunge nao, wakampiga mawe Paulo na kumburuta hadi nje ya mji wakidhani amekwisha kufa.
20Susirinkus aplink jį mokiniams, jis atsikėlė ir parėjo į miestą. O rytojaus dieną kartu su Barnabu iškeliavo į Derbę.
20Lakini waumini walipokusanyika na kumzunguka, aliamka akarudi mjini. Kesho yake, yeye pamoja na Barnaba walikwenda Derbe.
21Šitame mieste jie skelbė Evangeliją ir išmokė daugelį. Paskui grįžo atgal į Listrą, Ikonijų ir Antiochiją.
21Baada ya Paulo na Barnabas kuhubiri Habari Njema huko Derbe na kupata wafuasi wengi, walifunga safari kwenda Antiokia kwa kupitia Lustra na Ikonio.
22Ten jie stiprino mokinių sielas, ragino juos pasilikti tikėjime ir sakė: “Per daugelį išmėginimų mes turime įeiti į Dievo karalystę”.
22Waliwaimarisha waumini wa miji hiyo na kuwatia moyo wabaki imara katika imani. Wakawaambia, "Ni lazima sisi sote tupitie katika taabu nyingi ili tuingie katika ufalme wa Mungu."
23Kiekvienoje bažnyčioje su malda ir pasninku, uždėdami rankas, jie paskyrė jiems vyresniuosius ir pavedė juos Viešpačiui, kurį šie buvo įtikėję.
23Waliteua wazee katika kila kanisa kwa ajili ya waumini, na baada ya kusali na kufunga, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana ambaye walikuwa wanamwamini.
24Apkeliavę Pisidiją, jie atvyko į Pamfiliją.
24Baada ya kupitia katika nchi ya Pisidia, walifika Pamfulia.
25Paskelbę žodį Pergėje, leidosi žemyn į Ataliją.
25Baada ya kuhubiri ule ujumbe huko Perga, walikwenda Atalia.
26Iš ten išplaukė į Antiochiją, kur buvo pavesti Dievo malonei, kad nuveiktų darbą, kurį dabar pabaigė.
26Kutoka huko walisafiri kwa meli wakarudi Antiokia ambako hapo awali walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi wa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameitimiza.
27Sugrįžę jie sušaukė bažnyčią ir papasakojo, kokius darbus nuveikęs Dievas per juos ir kaip atvėręs pagonims tikėjimo vartus.
27Walipofika huko Antiokia walifanya mkutano wa kanisa la mahali hapo, wakawapa taarifa juu ya mambo Mungu aliyofanya pamoja nao, na jinsi alivyowafungulia mlango watu wa mataifa mengine mlango wa kuingia katika imani.
28Ir jie išbuvo su mokiniais netrumpą laiką.
28Wakakaa pamoja na wale waumini kwa muda mrefu.