Lithuanian

Swahili: New Testament

Acts

15

1Kai kurie, atvykę iš Judėjos, ėmė mokyti brolius: “Jei nesiduosite apipjaustomi pagal Mozės paprotį, negalėsite būti išgelbėti”.
1Basi, watu wengine walifika Antiokia kutoka Yudea wakaanza kuwafundisha wale ndugu wakisema, "Kama hamtatahiriwa kufuatana na mapokeo ya Sheria ya Mose, hamtaweza kuokolewa."
2Kilo nemažas vaidas ir ginčas tarp jų ir Pauliaus bei Barnabo. Buvo nutarta, kad Paulius, Barnabas ir kai kurie kiti iš anų nuvyktų dėl šio klausimo į Jeruzalę pas apaštalus ir vyresniuosius.
2Jambo hili lilisababisha ubishi mkubwa, na baada ya Paulo na Barnaba kujadiliana nao, ikaamuliwa Paulo na Barnaba pamoja na waumini kadhaa wa lile kanisa la Antiokia waende Yerusalemu kuwaona wale mitume na wazee kuhusu jambo hilo.
3Bažnyčios aprūpinti, jie iškeliavo per Finikiją ir Samariją, pasakodami apie pagonių atsivertimą, ir tuo padarė didelį džiaugsmą visiems broliams.
3Basi, kanisa liliwaaga, nao walipokuwa wanapitia Foinike na Samaria waliwaeleza watu jinsi mataifa mengine yalivyomgeukia Mungu. Habari hizo zikawafurahisha sana ndugu hao wote.
4Atvykę į Jeruzalę, jie buvo priimti bažnyčios, apaštalų bei vyresniųjų ir pranešė jiems, ką Dievas kartu su jais nuveikė.
4Walipofika Yerusalemu walikaribishwa na kanisa, mitume na wazee; nao wakawapa taarifa juu ya yote Mungu aliyoyafanya pamoja nao.
5Tuomet pakilo kai kurie įtikėjusieji iš fariziejų partijos ir tarė: “Juos reikia apipjaustyti ir įsakyti, kad laikytųsi Mozės Įstatymo”.
5Lakini waumini wengine waliokuwa wa kikundi cha Mafarisayo walisimama, wakasema, "Ni lazima watu wa mataifa mengine watahiriwe na kufundishwa kuifuata Sheria ya Mose."
6Apaštalai ir vyresnieji susirinko šio klausimo apsvarstyti.
6Basi, mitume na wazee walifanya mkutano maalum wa kuchunguza jambo hilo.
7Įsiliepsnojus ilgam ginčui, Petras pakilo ir kreipėsi į juos: “Vyrai broliai, jūs žinote, kad Dievas jau nuo senų dienų išsirinko mane iš jūsų, kad pagonys iš mano lūpų išgirstų Evangelijos žodį ir įtikėtų.
7Baada ya majadiliano marefu, Petro alisimama, akasema, "Ndugu zangu, ninyi mnafahamu kwamba hapo awali Mungu alipenda kunichagua mimi miongoni mwenu niihubiri Habari Njema, ili watu wa mataifa wapate kusikia na kuamini.
8Ir Dievas, kuris pažįsta žmonių širdis, paliudijo jų naudai, duodamas jiems Šventąją Dvasią kaip ir mums.
8Naye Mungu anayejua mioyo ya watu, alithibitisha kwamba amewakubali kwa kuwapa nao Roho Mtakatifu kama alivyotupa sisi.
9Jis nepadarė skirtumo tarp mūsų ir jų, tikėjimu nuskaistindamas jų širdis.
9Hakufanya ubaguzi wowote kati yetu na wao; aliitakasa mioyo yao kwa imani.
10Tad kodėl gundote Dievą ir kraunate ant mokinių sprando jungą, kurio nei mūsų tėvai, nei mes patys negalėjome panešti?
10Sasa basi, kwa nini kumjaribu Mungu kwa kuwatwika hao waumini mzigo ambao wala babu zetu, wala sisi hatukuweza kuubeba?
11Juk mes tikime, kad Viešpaties Jėzaus Kristaus malone būsime išgelbėti kaip ir jie”.
11Isiwe hivyo, ila tunaamini kwamba, sisi kama vile wao, tunaokolewa kwa njia ya neema ya Bwana Yesu."
12Tada visas susirinkimas nutilo ir ėmė klausytis Barnabo bei Pauliaus pasakojimo, kokių ženklų ir stebuklų per juos Dievas padarė tarp pagonių.
12Kikundi chote kilikaa kimya, kikawasikiliza Barnaba na Paulo wakieleza miujiza na maajabu ambayo Mungu alitenda kwa mikono yao kati ya watu wa mataifa mengine.
13Kai jie nutilo, atsiliepė Jokūbas ir tarė: “Vyrai broliai, paklausykite manęs!
13Walipomaliza kuongea, Yakobo alianza kusema: "Ndugu zangu, nisikilizeni!
14Simonas papasakojo, kaip Dievas pirmą kartą aplankė pagonis, kad išsirinktų iš jų savo vardui žmones.
14Simoni ameeleza jinsi Mungu hapo awali alivyojishughulisha na watu wa mataifa mengine, akachagua baadhi yao wawe watu wake.
15Čia dera pranašų žodžiai, kaip parašyta:
15Jambo hili ni sawa kabisa na maneno ya manabii, kama Maandiko Matakatifu yasemavyo:
16‘Paskui sugrįšiu ir vėl atstatysiu sugriuvusią Dovydo palapinę. Aš prikelsiu ją iš griuvėsių ir vėl ją išskleisiu,
16Baada ya mambo haya nitarudi. Nitaijenga tena ile nyumba ya Daudi iliyoanguka; nitayatengeneza magofu yake na kuijenga tena.
17kad ieškotų Viešpaties ir visi kiti žmonės, visi pagonys, kuriems skelbiamas mano vardas,­sako Viešpats, visa tai darantis’.
17Hapo watu wengine wote, watu wa mataifa yote niliowaita wawe wangu, watamtafuta Bwana.
18Nuo amžių Dievui žinomi visi Jo darbai.
18Ndivyo asemavyo Bwana, aliyefanya jambo hili lijulikane tangu kale.
19Todėl aš manau, kad į Dievą atsivertusių pagonių nereikia apsunkinti,
19"Kwa hiyo, uamuzi wangu ni huu: tusiwataabishe watu wa mataifa wanomgeukia Mungu.
20o tik jiems parašyti, jog susilaikytų nuo susiteršimo stabais, nuo ištvirkavimo, pasmaugtų gyvulių mėsos ir kraujo.
20Bali tuwapelekee barua kuwaambia wasile vyakula vilivyotiwa najisi kwa kutambikiwa sanamu za miungu; wajiepushe na uasherati; wasile mnyama yeyote aliyenyongwa, na wasinywe damu.
21Juk Mozė kiekviename mieste nuo senų laikų turi savo skelbėjų ir kas sabatą yra skaitomas sinagogose”.
21Kwa maana kwa muda mrefu maneno ya Mose yamekuwa yakihubiriwa katika kila mji na kusomwa katika masunagogi yote kila siku ya Sabato."
22Tada apaštalai ir vyresnieji kartu su visa bažnyčia nutarė pasiųsti į Antiochiją iš savųjų išrinktus vyrus kartu su Pauliumi ir Barnabu: Judą, vadinamą Barsabu, ir Silą, kurie buvo vadovaujantys tarp brolių.
22Mitume, wazee na kanisa lote waliamua kuwachagua watu fulani miongoni mwao na kuwatuma Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba. Basi, wakamchagua Yuda aitwaye pia Barsaba, na Sila ambao wote walikuwa wanajulikana zaidi kati ya ndugu.
23Jiems įteikė tokį raštą: “Apaštalai, vyresnieji ir broliai siunčia sveikinimą broliams, kilusiems iš pagonių Antiochijoje, Sirijoje bei Kilikijoje.
23Wakawapa barua hii: "Sisi mitume na wazee, ndugu zenu, tunawasalimuni ninyi ndugu wa mataifa mengine mlioko huko Antiokia, Siria na Kilikia.
24Sužinoję, kad kai kurie iš mūsų nuvykę savo kalbomis sukėlė jums nerimo ir sujaukė jūsų sielas, liepdami apsipjaustyti ir laikytis Įstatymo,
24Tumesikia kwamba watu wengine kutoka huku kwetu waliwavurugeni kwa maneno yao, wakaitia mioyo yenu katika wasiwasi. Lakini wamefanya hivyo bila ya idhini yoyote kutoka kwetu.
25mes susirinkę vieningai nusprendėme pasiųsti pas jus išrinktus vyrus su mūsų mylimaisiais Barnabu ir Pauliumi,
25Hivyo, tumeamua kwa pamoja kuwachagua watu kadhaa na kuwatuma kwenu pamoja na wapenzi wetu Barnaba na Paulo,
26kurie už mūsų Viešpatį Jėzų Kristų yra guldę savo galvas.
26ambao wamehatarisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
27Taigi siunčiame su jais Judą ir Silą, kurie jums tą patį praneš žodžiu.
27Kwa hiyo, tunawatuma Yuda na Sila kwenu; hawa watawaambieni wao wenyewe haya tuliyoandika.
28Šventajai Dvasiai ir mums pasirodė teisinga neužkrauti jums daugiau naštų, išskyrus tai, kas būtina:
28Basi, Roho Mtakatifu na sisi tumekubali tusiwatwike mzigo zaidi ya mambo haya muhimu:
29susilaikyti nuo aukų stabams, kraujo, pasmaugtų gyvulių mėsos ir ištvirkavimo. Jūs gerai elgsitės, saugodamiesi šitų dalykų. Likite sveiki!”
29Msile vyakula vilivyotambikiwa sanamu; msinywe damu; msile nyama ya mnyama aliyenyongwa; na mjiepushe na uasherati. Mtakuwa mmefanya vema kama mkiepa kufanya mambo hayo. Wasalaam!"
30Išsiųstieji, atvykę į Antiochiją, sukvietė bendruomenę ir įteikė laišką.
30Baada ya kuwaaga, hao wajumbe walielekea Antiokia ambako waliita mkutano wa waumini, wakawapa hiyo barua.
31Skaitydami šie džiaugėsi paguoda.
31Walipoisoma hiyo barua, maneno yake yaliwatia moyo, wakafurahi sana.
32Judas ir Silas, būdami pranašai, gausiais žodžiais skatino ir stiprino brolius.
32Yuda na Sila, ambao nao walikuwa manabii, walizungumza na hao ndugu kwa muda mrefu wakiwatia moyo na kuwaimarisha.
33Pabuvę ten kurį laiką, jie buvo brolių išleisti ramybėje pas apaštalus.
33Baada ya kukaa huko kwa muda fulani, ndugu wa Antiokia waliwaaga wakiwatakia amani, kisha wakarudi kwa wale waliokuwa wamewatuma.
34Bet Silas nusprendė ten pasilikti.
34Lakini Sila aliamua kubaki.
35Paulius su Barnabu taip pat pasiliko Antiochijoje, kartu su daugeliu kitų mokydami ir pamokslaudami Viešpaties žodį.
35Paulo na Barnaba walibaki huko Antiokia kwa muda; wakafundisha na kuhubiri neno la Bwana, pamoja na watu wengine wengi.
36Po kiek laiko Paulius tarė Barnabui: “Grįžkime, aplankykime brolius visuose miestuose, kur skelbėme Viešpaties žodį, ir pažiūrėkime, kaip jiems sekasi”.
36Baada ya siku kadhaa, Paulo alimwambia Barnaba, "Turudi tukawatembelee wale ndugu katika kila mji tulikolihubiri neno la Bwana tukajionee jinsi wanavyoendelea."
37Barnabas norėjo pasiimti kartu ir Joną, vadinamą Morkumi,
37Barnaba alitaka wamchukue pia Yohane aitwaye Marko.
38bet Paulius manė būsiant geriau neimti tokio, kuris Pamfilijoje buvo nuo jų pasitraukęs ir nesidarbavo su jais.
38Lakini Paulo hakupendelea kumchukua Marko, ambaye awali aliwaacha kule Pamfulia na kukataa kushiriki katika kazi yao.
39Kilo toks smarkus ginčas, kad jie vienas nuo kito atsiskyrė. Barnabas, pasiėmęs Morkų, išplaukė į Kiprą,
39Basi kukatokea ubishi mkali kati yao, na wakaachana. Barnaba akamchukua Marko, wakapanda meli kwenda Kupro.
40o Paulius, pasirinkęs Silą, iškeliavo, brolių patikėtas Viešpaties malonei.
40Naye Paulo akamchagua Sila, na baada ya ndugu wa mahali hapo kumweka chini ya ulinzi wa neema ya Bwana, akaondoka.
41Jis leidosi per Siriją ir Kilikiją, stiprindamas bažnyčias.
41Katika safari hiyo alipitia Siria na Kilikia akiyaimarisha makanisa.