1Paulius atkeliavo į Derbę ir Listrą. Ir štai ten buvo vienas mokinys, vardu Timotiejus, kurio motina buvo įtikėjusi žydė, o tėvasgraikas.
1Paulo alifika Derbe na Lustra, ambako aliishi mfuasi mmoja aitwaye Timotheo. Mama yake ambaye pia alikuwa mfuasi, alikuwa Myahudi; lakini baba yake alikuwa Mgiriki.
2Apie jį gerai liudijo Listros ir Ikonijaus broliai.
2Timotheo alikuwa na sifa kubwa kati ya wale ndugu wa Lustra na Ikonio.
3Paulius panorėjo jį pasiimti su savimi. Jis apipjaustydino jį dėl žydų, gyvenančių tame krašte. Mat visi žinojo jo tėvą esant graiką.
3Paulo alitaka Timotheo aandamane naye safarini, kwa hiyo alimtahiri. Alifanya hivyo kwa sababu Wayahudi wote walioishi sehemu hizo walijua kwamba baba yake Timotheo alikuwa Mgiriki.
4Keliaudami per miestus, jie liepdavo tikintiesiems laikytis Jeruzalės apaštalų bei vyresniųjų priimtų nutarimų.
4Walipokuwa wanapita katika ile miji waliwapa watu yale maagizo yaliyotolewa na mitume na wazee kule Yerusalemu, wakawaambia wayazingatie.
5Taip bažnyčios stiprėjo tikėjimu ir kasdien augo skaičiumi.
5Hivyo, yale makanisa yalizidi kuwa imara katika imani, na idadi ya waumini ikaongezeka kila siku.
6Jiems perėjus Frygiją ir Galatijos šalį, Šventoji Dvasia draudė jiems skelbti žodį Azijoje.
6Walipitia sehemu za Frugia na Galatia kwani Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kuhubiri huo ujumbe mkoani Asia.
7Atvykę iki Myzijos, jie mėgino eiti į Bitiniją, tačiau Dvasia jų neleido.
7Walipofika kwenye mipaka ya Musia, walijaribu kuingia mkoani Bithunia, lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
8Perėję Myziją, jie nuėjo į Troadę.
8Basi, walipitia Musia, wakaenda moja kwa moja mpaka Troa.
9Čia Paulius naktį turėjo regėjimą: jam pasirodė makedonietis, kuris maldavo: “Ateik į Makedoniją ir padėk mums!”
9Usiku huo, Paulo aliona ono ambalo alimwona mtu mmoja wa Makedonia amesimama pale na kumwomba: "Vuka, uje Makedonia ukatusaidie."
10Po šio regėjimo mes nedelsdami pasistengėme išvykti į Makedoniją, įsitikinę, kad Viešpats mus pašaukė skelbti jiems Evangeliją.
10Mara baada ya Paulo kuona ono hilo, tulijitayarisha kwenda Makedonia bila kukawia, tukiwa na hakika kwamba Mungu ametuita tuwapelekee Habari Njema.
11Išplaukę iš Troadės, leidomės tiesiog į Samotrakę ir rytojaus dieną į Neapolį.
11Kutoka Troa, tulisafiri kwa meli moja kwa moja mpaka Samothrake, na kesho yake tukatia nanga Neapoli.
12Iš čia atvykome į Filipuspirmąjį šios Makedonijos dalies ir kolonijos miestą. Šiame mieste užtrukome kelias dienas.
12Kutoka huko, tulikwenda mpaka Filipi, mji wa wilaya ya kwanza ya Makedonia, na ambao pia ni koloni la Waroma. Tulikaa katika mji huo siku kadhaa.
13Sabato dieną išėjome už miesto prie upės, kur pagal paprotį buvo maldos vieta, ir atsisėdę kalbėjome susirinkusioms moterims.
13Siku ya Sabato tulitoka nje ya mji, tukaenda kando ya mto ambapo tulidhani ya kuwa ni mahali pa kusali. Tuliketi, tukaongea na wanawake waliokusanyika mahali hapo.
14Viena dievobaiminga moteris, vardu Lidija, prekiaujanti purpuro drabužiais, kilusi iš Tiatyrų miesto, klausėsi, ir Viešpats atvėrė jos širdį tam, ką kalbėjo Paulius.
14Miongoni mwa wale waliotusikiliza alikuwa mwanamke mmoja mcha Mungu aitwaye Ludia mwenyeji wa Thuatira, ambaye alikuwa mfanyabiashara ya nguo za kitani za rangi ya zambarau. Bwana aliufungua moyo wake hata akayapokea yale maneno Paulo aliyokuwa anasema.
15Kai ji su savo namiškiais buvo pakrikštyta, ėmė mūsų prašyti: “Jei mane laikote Viešpaties tikinčiąja, ateikite ir pasilikite mano namuose”. Ji tiesiog mus privertė.
15Baada ya huyo mama pamoja na jamaa yake kubatizwa, alitualika akisema, "Kama kweli mmeona kwamba mimi namwamini Bwana, karibuni nyumbani kwangu mkakae." Akatuhimiza twende.
16Kartą, einančius į maldos vietą, mus pasitiko viena tarnaitė, turinti spėjimo dvasią. Spėdama ji daug uždirbdavo savo šeimininkams.
16Siku moja, tulipokuwa tunakwenda mahali pa kusali, msichana mmoja aliyekuwa na pepo mwenye uwezo wa kuagua alikutana nasi. Msichana huyo alikuwa anawapatia matajiri wake fedha nyingi kwa uaguzi wake.
17Ji ėmė sekti paskui Paulių bei mus, šaukdama: “Šitie vyrai yra aukščiausiojo Dievo tarnai ir skelbia mums išgelbėjimo kelią”.
17Basi, huyo msichana alimfuata Paulo na sisi, akipiga kelele na kusema, "Hawa watu ni watumishi wa Mungu Mkuu. Wanawatangazieni njia ya wokovu."
18Taip ji darė daugelį dienų. Nebeapsikęsdamas Paulius atsigręžė ir paliepė dvasiai: “Jėzaus Kristaus vardu įsakau tau iš jos išeiti!” Ir dvasia tučtuojau išėjo.
18Akawa anafanya hivyo kwa siku nyingi hata siku moja Paulo alikasirika, akamgeukia na kumwambia huyo pepo, "Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu!" Mara huyo pepo akamtoka.
19Šeimininkai, pamatę, kad jų pasipelnymo viltys žlugo, sugriebė Paulių bei Silą ir nutempė į miesto aikštę pas vyresnybę.
19Matajiri wa yule msichana walipoona kwamba tumaini lao la kupata mali limekwisha, waliwakamata Paulo na Sila, wakawaburuta mpaka hadharani, mbele ya wakuu.
20Nuvedę pas pretorius, jie tarė: “Šitie žmonės mūsų mieste kelia sąmyšį. Jie yra žydai
20Wakawashtaki kwa mahakimu wakisema, "Watu hawa ni Wayahudi na wanafanya fujo katika mji wetu.
21ir skelbia papročius, kurių mums, romėnams, nevalia nei priimti, nei laikytis”.
21Wanafundisha desturi ambazo sisi raia wa Roma haturuhusiwi kuzikubali wala kuzifuata."
22Prieš juos sukilo ir minia. Pretoriai nuplėšė nuo jų drabužius ir įsakė juos mušti lazdomis.
22Kundi la watu likajiunga nao, likawashambulia. Wale mahakimu wakawatatulia Paulo na Sila mavazi yao, wakaamuru wapigwe viboko.
23Davę daug kirčių, įmetė juos į kalėjimą, įsakydami kalėjimo prižiūrėtojui rūpestingai saugoti.
23Baada ya kupigwa sana wakatiwa ndani, na askari wa gereza akaamriwa kuwaweka chini ya ulinzi mkali.
24Gavęs tokį įsakymą, kalėjimo prižiūrėtojas įgrūdo juos į vidinę kamerą, o jų kojas įtvėrė į šiekštą.
24Kutokana na maagizo hayo, huyo askari aliwaweka katika chumba cha ndani kabisa cha gereza na kuifunga miguu yao kwenye nguzo.
25Apie vidurnaktį Paulius ir Silas meldėsi ir giedojo Dievui himnus. Kiti kaliniai jų klausėsi.
25Karibu na usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakisali na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, huku wafungwa wengine wakiwa wanasikiliza.
26Staiga kilo toks stiprus žemės drebėjimas, jog kalėjimo pamatai susvyravo. Bematant atsivėrė visos durys, ir visiems nukrito pančiai.
26Ghafla, kulitokea mtetemeko mkuu wa ardhi ambao uliitikisa misingi ya gereza. Mara, milango yote ikafunguka na minyororo iliyowafunga hao wafungwa ikaachana.
27Kalėjimo prižiūrėtojas nubudo ir, pamatęs atviras kalėjimo duris, išsitraukė kalaviją norėdamas nusižudyti: jis pamanė, kad kaliniai pabėgo.
27Askari wa gereza alipoamka na kuiona milango ya gereza imefunguliwa, alidhani kwamba wafungwa wote walikuwa wametoroka na hivyo akauchomoa upanga wake, akataka kujiua.
28Bet Paulius garsiai sušuko: “Nedaryk sau pikto! Mes visi esame čia”.
28Lakini Paulo akaita kwa sauti kubwa: "Usijidhuru mwenyewe kwa maana sisi sote tuko hapa."
29Paprašęs šviesos, jis šoko vidun ir, visas drebėdamas, puolė Pauliui ir Silui po kojų.
29Baada ya kumwita mtu alete taa, huyo askari wa gereza alikimbilia ndani, akajitupa mbele ya miguu ya Paulo na Sila huku akitetemeka kwa hofu.
30Po to išvedė juos laukan ir paklausė: “Gerbiamieji, ką turiu daryti, kad būčiau išgelbėtas?”
30Halafu aliwaongoza nje, akawauliza, "Waheshimiwa, nifanye nini nipate kuokoka?"
31Jie atsakė: “Tikėk Viešpatį Jėzų Kristų ir būsi išgelbėtas tu ir tavo namai”.
31Wao wakamjibu, "Mwamini Bwana Yesu nawe utaokolewa pamoja na jamaa yako yote."
32Ir jie skelbė Viešpaties žodį jam ir jo namiškiams.
32Basi, wakamhubiria neno la Bwana yeye pamoja na jamaa yake.
33Tą pačią nakties valandą jis pasiėmė juos, nuplovė jų žaizdas ir nedelsiant kartu su visais saviškiais buvo pakrikštytas.
33Yule askari aliwachukua saa ileile ya usiku akawasafisha majeraha yao, kisha yeye na jamaa yake wakabatizwa papo hapo.
34Nusivedęs į savo namus, jis padengė jiems stalą ir su visais namiškiais džiūgavo, įtikėjęs Dievą.
34Halafu akawachukua Paulo na Sila nyumbani kwake, akawapa chakula. Yeye na jamaa yake yote wakafanya sherehe kwa vile sasa walikuwa wanamwamini Mungu.
35Dienai išaušus, pretoriai pasiuntė liktorius pranešti kalėjimo viršininkui: “Paleisk tuos žmones!”
35Kesho yake asubuhi, mahakimu waliwatuma maofisa wao wakisema, "Wafungueni wale watu."
36Tas perdavė tuos žodžius Pauliui: “Pretoriai liepia jus paleisti. Galite eiti ir ramiai keliauti”.
36Yule askari wa gereza alimpasha habari Paulo: "Mahakimu wametuma ujumbe ili mfunguliwe. Sasa mnaweza kutoka na kwenda zenu kwa amani."
37Bet Paulius jiems atsakė: “Mus, Romos piliečius, nenuteistus viešai mušė ir įmetė į kalėjimą, o dabar nori slapta paleisti?! Šito nebus! Tegul patys ateina ir išveda!”
37Lakini Paulo alimjibu, "Ati nini? Ingawa hatukuwa na kosa, walitupiga viboko hadharani hali sisi ni raia wa Roma. Tena, walitutia ndani na sasa wanataka kutufungulia kwa siri! Hata kidogo! Ni lazima wao wenyewe waje hapa watufungulie."
38Liktoriai perdavė pretoriams šį atsakymą. Išgirdę, kad tai Romos piliečiai, pretoriai išsigando.
38Hao maofisa waliwapasha habari mahakimu juu ya jambo hilo, nao waliposikia kwamba Paulo na Sila walikuwa raia wa Roma, waliogopa.
39Jie atėjo, atsiprašė ir išsivedę prašė, kad paliktų miestą.
39Hivyo, walikwenda kuwataka radhi na baada ya kuwatoa ndani waliwaomba watoke katika mji ule.
40Išėję iš kalėjimo, Paulius ir Silas užsuko pas Lidiją, pasimatė su broliais, padrąsino juos ir iškeliavo toliau.
40Paulo na Sila walitoka gerezani, wakaenda nyumbani kwa Ludia. Huko walionana na ndugu waumini na baada ya kuwatia moyo wakaondoka.