Lithuanian

Swahili: New Testament

Acts

17

1Perėję Amfipolį ir Apoloniją, jie atvyko į Tesaloniką, kur buvo žydų sinagoga.
1Kwa kupitia Amfipoli na Apolonia, walisafiri mpaka Thesalonika ambako kulikuwa na sunagogi la Wayahudi.
2Pagal savo įprotį Paulius užėjo pas juos ir tris sabatus aiškinosi su jais Raštus,
2Paulo alijiunga nao kama ilivyokuwa desturi yake akajadiliana nao Sabato tatu mfululizo, akatumia Maandiko Matakatifu.
3dėstydamas ir įrodinėdamas, kad Kristus turėjo kentėti ir prisikelti iš numirusių ir kad: “Kristus­tai Jėzus, kurį aš jums skelbiu”.
3Aliyaeleza na kuonyesha kwamba ilimbidi Kristo kuteswa na kufufuka kutoka wafu. Akawaambia, "Yesu ambaye mimi namhubiri kwenu ndiye Kristo."
4Kai kurie iš jų įtikėjo ir prisidėjo prie Pauliaus ir Silo, taip pat daugybė pamaldžių graikų ir nemaža aukštos kilmės moterų.
4Baadhi yao walikubali wakajiunga na Paulo na Sila. Kadhalika, idadi kubwa ya Wagiriki waliomcha Mungu pamoja na wanawake wengi wa tabaka la juu, walijiunga nao.
5Bet neįtikėję žydai, apimti pavydo, surinko iš gatvės piktų žmonių, sukurstė minią ir sukėlė mieste sąmyšį. Jie užpuolė Jasono namus ir ėmė ten ieškoti Pauliaus ir Silo, norėdami išvesti juos prieš minią.
5Lakini Wayahudi wakaona wivu; wakawakodi wafidhuli sokoni, wakafanya kikundi na kuzusha fujo mjini kote. Wakaivamia nyumba ya Yasoni wakitumaini kuwapata humo Paulo na Sila ili wawalete hadharani.
6Jų neradę, nusitempė Jasoną ir kelis brolius pas miesto vadovus, šaukdami: “Tie žmonės, kurie verčia visą pasaulį aukštyn kojom, atvyko ir čia,
6Lakini hawakuwapata na hivyo walimburuta Yasoni pamoja na ndugu wengine mpaka kwa wakuu wa mji, wakapiga kelele: "Watu hawa wamekuwa wakivuruga dunia yote na sasa wako hapa mjini.
7o Jasonas juos priglaudė. Visi šitie laužo ciesoriaus įsakymus, tvirtindami, jog esąs kitas karalius, būtent Jėzus”.
7Yasoni amewakaribisha nyumbani kwake. Wote wanafanya kinyume cha amri ya Kaisari wakisema eti Kuna mfalme mwingine aitwaye Yesu."
8Taip jie sukėlė nerimo jų klausiusiai miniai ir miesto vadovams.
8Kwa maneno hayo waliwatia wasiwasi wakuu wa mji na kundi la watu.
9Šie, gavę iš Jasono ir kitų užstatą, paleido juos.
9Wakawafanya Yasoni na wenzake watoe dhamana, kisha wakawaacha waende zao.
10Broliai tuojau pat, nakčia, išsiuntė Paulių ir Silą į Berėją. Ten atvykę, jie užėjo į žydų sinagogą.
10Usiku, wale ndugu waliwahimiza Paulo na Sila waende Berea. Mara tu walipofika huko, walikwenda katika sunagogi la Wayahudi.
11Tenykščiai pasirodė esą kilnesni už tesalonikiečius. Jie noriai priėmė žodį ir kasdien tyrinėjo Raštus, ar taip esą iš tikrųjų.
11Watu wa huko walikuwa wasikivu zaidi kuliko wale wa Thesalonika. Waliupokea ule ujumbe kwa hamu kubwa, wakawa wanayachunguza Maandiko Matakatifu kila siku, ili kuona kama yale waliyosema Paulo na Sila yalikuwa kweli.
12Daugelis iš jų įtikėjo, taip pat nemažai kilmingų graikų moterų ir vyrų.
12Wengi wao waliamini na pia wanawake wa Kigiriki wa tabaka la juu na wanaume pia.
13Sužinoję, kad Paulius jau Berėjoje skelbia Dievo žodį, Tesalonikos žydai atskubėjo ir čia drumsti ir kurstyti žmonių.
13Lakini, Wayahudi wa Thesalonika walipogundua kwamba Paulo alikuwa anahubiri neno la Mungu huko Berea, walikwenda huko, wakaanza kufanya fujo na kuchochea makundi ya watu.
14Tada broliai skubiai išsiuntė Paulių prie jūros, o Silas ir Timotiejus pasiliko ten.
14Wale ndugu wakamsindikiza haraka aende pwani lakini Sila na Timotheo walibaki Berea.
15Pauliaus palydovai nuvedė jį iki Atėnų. Gavę įsakymą pranešti Silui ir Timotiejui, kad kuo greičiau atvyktų pas jį, grįžo atgal.
15Wale ndugu waliomsindikiza Paulo walikwenda pamoja naye mpaka Athene. Kisha, wakarudi pamoja na maagizo kutoka kwa Paulo kwamba Sila na Timotheo wamfuate upesi iwezekanavyo.
16Belaukdamas Atėnuose jų atvykstant ir matydamas pilną miestą stabų, Paulius dvasioje netvėrė pykčiu.
16Paulo alipokuwa anawasubiri Sila na Timotheo huko Athene, moyo wake ulighadhibika sana alipoona jinsi mji huo ulivyokuwa umejaa sanamu za miungu.
17Jis aiškinosi sinagogoje su žydais ir pamaldžiaisiais, o aikštėje kasdien su tais, kurie ten būdavo.
17Alijadiliana na Wayahudi na watu wengine waliomcha Mungu katika sunagogi; na kila siku alikuwa na majadiliano sokoni pamoja na wowote wale waliojitokeza.
18Kai kurie epikūrininkų ir stoikų filosofai bandė su juo ginčytis. Vieni klausė: “Ką šis plepys nori pasakyti?” O kiti: “Atrodo, kad jis svetimų demonų skelbėjas”. Mat jis skelbė Jėzų ir prisikėlimą.
18Wengine waliofuata falsafa ya Epikuro na Stoiki walibishana naye. Wengine walisema, "Anataka kusema nini huyu bwanamaneno?" Kwa kuwa Paulo alikuwa anahubiri juu ya Yesu na juu ya ufufuo, wengine walisema, "Inaonekana kama anahubiri juu ya miungu ya kigeni."
19Jie paėmė, nusivedė jį į Areopagą ir tarė jam: “Ar galėtume sužinoti, kokį naują mokslą tu skelbi?
19Hivyo walimchukua Paulo, wakampeleka Areopago, wakasema, "Tunataka kujua jambo hili jipya ulilokuwa unazungumzia.
20Nes tu kalbi mūsų ausims negirdėtus dalykus. Taigi norėtume sužinoti, kas tai būtų”.
20Vitu vingine tulivyosikia kwa masikio yetu vinaonekana kuwa viroja kwetu. Tungependa kujua mambo haya yana maana gani."
21Mat visi atėniečiai ir ten gyvenantys ateiviai leisdavo laiką ne kaip kitaip, o tik pasakodami arba klausydami ką nors nauja.
21Wananchi wa Athene na wakazi wengine wa huko walikuwa wanatumia wakati wao wote kuhadithiana na kusikiliza habari mpyampya.
22Tada Paulius, atsistojęs Areopago viduryje, prabilo: “Atėnų vyrai, matau, kad jūs visais atžvilgiais labai religingi.
22Basi, Paulo alisimama mbele ya baraza la Areopago, akasema, "Wananchi wa Athene! Ninaona kwamba ninyi, kwa vyovyote, ni watu wa dini sana.
23Vaikščiodamas ir apžiūrinėdamas jūsų šventenybes, radau aukurą su užrašu: ‘Nežinomam dievui’. Taigi Tą, kurį nepažindami garbinate, aš jums ir skelbiu.
23Sababu yenyewe ni kwamba katika pitapita yangu niliangalia sanamu zenu za ibada nikakuta madhabahu moja ambayo imeandikwa: Kwa ajili ya Mungu yule Asiyejulikana. Basi, huyo mnayemwabudu bila kujua, ndiye ninayemhubiri kwenu.
24Dievas, pasaulio ir visko, kas jame yra, Kūrėjas, būdamas dangaus ir žemės Viešpats, negyvena žmonių rankomis statytose šventyklose
24Mungu, aliyeumba ulimwengu na vyote vilivyomo, ni Bwana wa mbingu na nchi; yeye hakai katika hekalu zilizojengwa na watu.
25ir nėra žmonių rankomis aptarnaujamas, tarsi Jam ko nors trūktų. Jis gi pats visiems duoda gyvybę, alsavimą ir visa kita.
25Wala hatumikiwi kwa mikono ya watu kana kwamba anahitaji chochote kile, kwa maana yeye mwenyewe ndiye anayewapa watu uhai, anawawezesha kupumua na anawapa kila kitu.
26Iš vieno kraujo Jis išvedė visas žmonių tautas, kad šios gyventų visoje žemėje. Jis nustatė iš anksto paskirtus laikus ir apsigyvenimo ribas,
26Kutokana na mtu mmoja aliumba mataifa yote na kuyawezesha kuishi duniani kote. Aliamua na kupanga kabla kabisa lini na wapi mataifa hayo yangeishi.
27kad žmonės ieškotų Viešpaties ir tartum apgraibomis Jį atrastų, nors Jis netoli nuo kiekvieno iš mūsų.
27Alifanya hivyo, ili mataifa hayo yapate kumfuata, na kama vile kwa kupapasapapasa, yapate kumfikia. Hata hivyo lakini, Mungu hayuko mbali na kila mmoja wetu.
28Juk mes Jame gyvename, judame ir esame, kaip yra pasakę ir kai kurie jūsų poetai: ‘Mes irgi esame kilę iš Jo’.
28Kama alivyosema mtu mmoja: Ndani yake yeye sisi tunaishi, tunajimudu, na tuko! Ni kama washairi wenu wengine walivyosema: Sisi ni watoto wake.
29Todėl, būdami dieviškos kilmės, neturime manyti, jog Dievybė yra panaši į auksą, sidabrą ar akmenį, įgavusį pavidalą žmogaus sumanymų ir sugebėjimų dėka.
29Ikiwa basi, sisi ni watoto wa Mungu, haifai kumfikiria Mungu kuwa kama dhahabu, fedha au hata jiwe lililochongwa na kutiwa nakshi na binadamu.
30Ir štai Dievas nebežiūri anų neišmanymo laikų ir dabar įsako visur visiems žmonėms atgailauti,
30Mungu alifanya kama kwamba haoni nyakati zile watu walipokuwa wajinga. Lakini sasa, anaamuru watu wote kila mahali watubu.
31nes Jis nustatė dieną, kada teisingai teis visą pasaulį per žmogų, kurį paskyrė ir visiems už Jį laidavo, prikeldamas Jį iš numirusių”.
31Kwa maana amekwisha weka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki kwa njia ya mtu mmoja aliyemteua. Mungu amewathibitishia wote jambo hili kwa kumfufua mtu huyo kutoka wafu!"
32Išgirdę apie prisikėlimą iš numirusių, vieni ėmė šaipytis, o kiti sakė: “Apie tai tavęs paklausysime kitą kartą”.
32Walipomsikia Paulo anasema juu ya jambo la kufufuka kwa wafu, wengine wao waliangua kicheko; lakini wengine walisema, "Tunataka kukusikia tena juu ya jambo hili!"
33Šitaip Paulius paliko jų būrį.
33Hivyo, Paulo aliwaacha, akatoka barazani.
34Vis dėlto kai kurie vyrai prisidėjo prie jo ir įtikėjo. Iš jų Dionizas, Areopago narys, viena moteris, vardu Damaridė, ir jų draugai.
34Lakini watu kadhaa waliandamana naye, wakawa waumini. Miongoni mwao walikuwa Dionisio wa Areopago, mwanamke mmoja aitwaye Damari na wengineo.