1Po viso šito Paulius iškeliavo iš Atėnų ir nuvyko į Korintą.
1Baada ya hayo, Paulo aliondoka Athene, akaenda Korintho.
2Čia jis sutiko vieną iš Ponto kilusį žydą, vardu Akvilą, su žmona Priscile, neseniai atsikėlusius iš Italijos. Mat Klaudijus buvo išleidęs įsakymą visiems žydams išsikraustyti iš Romos. Jis nuėjo pas juos
2Huko Korintho, alimkuta Myahudi mmoja aitwaye Akula, mzaliwa wa Ponto. Akula pamoja na mkewe aitwaye Priskila, walikuwa wamerudi kutoka Italia siku hizohizo kwa sababu Kaisari Klaudio alikuwa ameamuru Wayahudi wote waondoke Roma. Paulo alikwenda kuwaona,
3ir, kadangi mokėjo bendrą amatą, pasiliko ten ir dirbo. Jie vertėsi palapinių audimu.
3na kwa vile wao walikuwa mafundi wa kushona mahema kama alivyokuwa yeye, Paulo alikaa nao akafanya kazi.
4Kiekvieną sabatą Paulius kalbėdavo sinagogoje, įtikinėdamas žydus ir graikus.
4Kila Sabato alifanya majadiliano katika sunagogi akijaribu kuwavuta Wayahudi na Wagiriki.
5Atvykus iš Makedonijos Silui ir Timotiejui, Paulius buvo Dvasios paragintas ir liudijo žydams, kad Jėzus yra Kristus.
5Baada ya Sila na Timotheo kuwasili kutoka Makedonia, Paulo alianza kutumia wakati wake wote kwa ajili ya kuhubiri, akawathibitishia Wayahudi kwamba Yesu ndiye Kristo.
6Bet jiems prieštaraujant ir piktžodžiaujant, jis nusipurtė drabužius ir tarė: “Jūsų kraujas tekrinta ant jūsų pačių galvų! Aš nekaltas ir nuo šiol eisiu pas pagonis”.
6Walipompinga na kuanza kumtukana, aliyakung'uta mavazi yake mbele yao akisema, "Mkipotea ni shauri lenu wenyewe; mimi sina lawama yoyote juu ya jambo hilo. Na tangu sasa nitawaendea watu na mataifa mengine."
7Ir, pasitraukęs iš ten, persikėlė į vieno dievobaimingo vyro, vardu Ticijaus Justo, namus, buvusius šalia sinagogos.
7Basi, akatoka hapo akaenda kukaa nyumbani kwa mtu mmoja mcha Mungu aitwaye Tito Yusto. Nyumba yake Tito ilikuwa karibu na lile sunagogi.
8Sinagogos vyresnysis Krispas su visais savo namiškiais įtikėjo Viešpatį. Ir daugelis korintiečių klausydamiesi įtikėjo ir buvo pakrikštyti.
8Lakini Krispo, mkuu wa sunagogi, alimwamini Bwana yeye pamoja na jamaa yake yote. Wakorintho wengi waliusikiliza ujumbe huo, wakaamini na kubatizwa.
9Naktį Viešpats regėjime prabilo Pauliui: “Nebijok! Kalbėk ir netylėk!
9Siku moja usiku, Bwana alimwambia Paulo katika maono: "Usiogope, endelea kuhubiri tu bila kufa moyo,
10Aš esu su tavimi ir niekas nesikėsins tau kenkti, nes šiame mieste daugel žmoniųmanieji”.
10maana mimi niko pamoja nawe. Hakuna mtu atakayejaribu kukudhuru maana hapa mjini pana watu wengi walio upande wangu."
11Ir jis ten pasiliko metus ir šešis mėnesius, mokydamas juos Dievo žodžio.
11Basi, Paulo alikaa huko akifundisha neno la Mungu kati yao kwa muda wa mwaka mmoja na nusu.
12Galionui būnant Achajos prokonsulu, žydai visi kaip vienas sukilo prieš Paulių, nusitempė jį į teismo vietą
12Lakini wakati Galio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Akaya, Wayahudi walimvamia Paulo kwa pamoja na kumpeleka mahakamani.
13ir pareiškė: “Šitas įtikinėja žmones garbinti Dievą Įstatymui priešingu būdu”.
13Wakasema, "Tunamshtaki mtu huyu kwa sababu ya kuwashawishi watu wamwabudu Mungu kwa namna inayopingana na Sheria."
14Pauliui rengiantis prabilti, Galionas tarė žydams: “Jei tai būtų koks nusikaltimas ar piktas darbas, tuomet, žydų vyrai, būtų dėl ko jus išklausyti.
14Kabla tu Paulo hajaanza kusema, Galio aliwaambia Wayahudi, "Sikilizeni enyi Wayahudi! Kama kweli jambo hili lingekuwa juu ya uhalifu au uovu ningekuwa tayari kuwasikilizeni.
15Bet kai kyla ginčas apie mokymą, vardus bei jūsų Įstatymą, spręskite patys; tokių dalykų teisėjas būti nenoriu”.
15Lakini kama ni shauri la ubishi kuhusu maneno na majina ya Sheria yenu, amueni ninyi wenyewe. Mimi sitaki kuwa hakimu wa mambo haya!"
16Ir pavarė juos nuo teismo krasės.
16Basi, akawafukuza kutoka mahakamani.
17Tada visi graikai užpuolė sinagogos vyresnįjį Sosteną ir sumušė jį prie teismo krasės. Galionas į tai nekreipė dėmesio.
17Nao wote wakamkamata Sosthene ambaye alikuwa kiongozi wa sunagogi, wakampiga palepale mbele ya mahakama. Lakini Galio hakujali kitendo hicho hata kidogo.
18Paulius, išbuvęs Korinte dar netrumpą laiką, atsisveikino su broliais ir kartu su Priscile bei Akvilu išplaukė į Siriją. Kenchrėjoje jis nusiskuto galvą, nes padarė įžadą.
18Paulo alikaa bado na wale ndugu huko Korintho kwa siku nyingi. Kisha aliwaaga, akapanda meli kwenda Siria pamoja na Priskila na Akula. Huko Kenkrea, alinyoa nywele zake kwa sababu ya nadhiri aliyokuwa ameweka.
19Atvykęs į Efezą, jis paliko juos, o pats nuėjęs į sinagogą, ėmė kalbėtis su žydais.
19Walifika Efeso na hapo Paulo aliwaacha Priskila na Akula, akaenda katika sunagogi, akajadiliana na Wayahudi.
20Jie prašė jį pasilikti ilgesnį laiką, bet jis nesutiko
20Walimwomba akae nao muda mrefu zaidi, lakini hakupenda.
21ir atsisveikindamas tarė: “Aš būtinai turiu praleisti ateinančią šventę Jeruzalėje. Jei Dievas panorės, vėl atvyksiu pas jus”. Ir iškeliavo iš Efezo.
21Bali alipokuwa anaondoka, alisema, "Mungu akipenda nitakuja kwenu tena." Akaondoka Efeso kwa meli.
22Atplaukęs į Cezarėją, jis patraukė aukštyn, pasveikino bažnyčią ir išvyko į Antiochiją.
22Meli ilitia nanga Kaisarea, naye Paulo akaenda Yerusalemu kulisalimia lile kanisa, kisha akaenda Antiokia.
23Pabuvęs ten kiek laiko, vėl leidosi į kelionę ir ėjo per Galatijos kraštą bei Frygiją, stiprindamas visus mokinius.
23Alikaa huko muda mfupi, halafu akaendelea na safari kwa kupitia sehemu za Galatia na Frugia akiwatia moyo wafuasi wote.
24Vienas žydas, vardu Apolas, kilęs iš Aleksandrijos, iškalbingas ir puikiai išmanantis Raštus vyras, atvyko į Efezą.
24Myahudi mmoja aitwaye Apolo, mzaliwa wa Aleksandria, alifika Efeso. Alikuwa mtu mwenye ufasaha wa kuongea na mwenye ujuzi mkubwa wa Maandiko Matakatifu.
25Jis buvo pamokytas Viešpaties kelio ir, degdamas dvasia, kalbėjo ir uoliai mokė apie Viešpatį, nors tepažinojo Jono krikštą.
25Alikuwa amefundishwa juu ya hiyo njia ya Bwana, na akiwa motomoto, aliongea juu ya habari za Yesu. Akafundisha kwa usahihi ingawa alikuwa amepata ubatizo wa Yohane tu.
26Jis ėmė drąsiai skelbti sinagogoje. Išgirdę jį, Priscilė ir Akvilas pasikvietė pas save ir nuodugniau išaiškino jam Dievo kelią.
26Priskila na Akula walipomsikia akiongea kwa uhodari ndani ya sunagogi, walimchukua kwao wakamfundisha hiyo Njia ya Mungu kwa usahihi zaidi.
27Kai jis panoro vykti į Achają, broliai parašė mokiniams, ragindami jį priimti. Nuvykęs tenai, jis buvo labai naudingas per malonę įtikėjusiesiems.
27Apolo alipoamua kwenda Akaya, wale ndugu walimtia moyo kwa kuwaandikia wafuasi kule Akaya wampokee. Alipofika huko, aliweza kwa msaada wa neema ya Mungu, kuwasaidia sana wale ndugu waliopata kuwa waumini;
28Mat jis viešumoje smarkiai sukirsdavo žydus, iš Raštų įrodydamas Jėzų esant Kristų.
28kwa maana aliendelea kwa uhodari kuwashinda Wayahudi hadharani akithibitisha kwa Maandiko Matakatifu kuwa Yesu ni Kristo.