1Apolui būnant Korinte, Paulius, perėjęs aukštutines sritis, atvyko į Efezą. Užtikęs ten kelis mokinius,
1Wakati Apolo alipokuwa Korintho, Paulo alisafiri sehemu za bara, akafika Efeso ambako aliwakuta wanafunzi kadhaa.
2paklausė: “Ar įtikėję gavote Šventąją Dvasią?” Jie atsakė: “Mes nė girdėti negirdėjome, kad yra Šventoji Dvasia”.
2Akauliza, "Je, mlipopata kuwa waumini mlipokea Roho Mtakatifu?" Nao wakamjibu, "La! Hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatujasikia."
3Jis klausė toliau: “Kokiu tad krikštu jūs buvote pakrikštyti?” Jie atsakė: “Jono krikštu”.
3Naye akasema, "Sasa mlipata ubatizo wa namna gani?" Wakamjibu, "Ubatizo wa Yohane."
4Tada Paulius tarė: “Jonas krikštijo atgailos krikštu, ragindamas žmones tikėti Tą, kuris ateis po jo, būtent Kristų Jėzų”.
4Naye Paulo akasema, "Ubatizo wa Yohane ulikuwa wa kuonyesha kwamba watu wametubu. Yohane aliwaambia watu wamwamini yule ambaye alikuwa anakuja baada yake, yaani Yesu."
5Tai išgirdę, jie buvo pakrikštyti Viešpaties Jėzaus vardu.
5Baada ya kusikia hayo, walibatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
6Kai Paulius jiems uždėjo rankas, ant jų nužengė Šventoji Dvasia ir jie ėmė kalbėti kalbomis ir pranašauti.
6Basi, Paulo akawawekea mikono, na Roho Mtakatifu akawashukia, wakaanza kusema lugha mbalimbali na kutangaza ujumbe wa Mungu.
7Iš viso jų buvo apie dvylika vyrų.
7Wote jumla, walikuwa watu wapatao kumi na wawili.
8Paulius nuėjo į sinagogą ir ten per tris mėnesius drąsiai kalbėjo, įtikinėdamas ir aiškindamas apie Dievo karalystę.
8Kwa muda wa miezi mitatu Paulo alikuwa akienda katika sunagogi, akawa na majadiliano ya kuvutia sana juu ya Ufalme wa Mungu.
9Kai kurie užkietėjo ir netikėjo, piktžodžiaudami tam Keliui daugumos akyse, tad Paulius pasitraukė nuo jų, atskyrė mokinius ir kasdien juos mokė Tirano mokykloje.
9Lakini wengine walikuwa wakaidi, wakakataa kuamini, wakaanza kuongea vibaya hadharani juu ya Njia ya Bwana. Hapo Paulo alivunja uhusiano nao, akawachukua pembeni wale wanafunzi wake, akawa anazungumza nao kila siku katika jumba la masomo la Turano.
10Tai truko dvejus metus, ir visi Azijos gyventojai, tiek žydai, tiek graikai, išgirdo Viešpaties Jėzaus žodį.
10Aliendelea kufanya hivyo kwa muda wa miaka miwili hata wakazi wote wa Asia, Wayahudi na watu wa mataifa mengine, wakaweza kusikia neno la Bwana.
11Pauliaus rankomis Dievas darė ypatingų stebuklų.
11Mungu alifanya miujiza ya ajabu kwa mikono ya Paulo.
12Žmonės net dėdavo ligoniams jo kūną lietusias skepetėles bei prijuostes, ir nuo jų pasitraukdavo ligos, išeidavo piktosios dvasios.
12Watu walikuwa wakichukua leso na nguo nyingine za kazi ambazo Paulo alikuwa amezitumia, wakazipeleka kwa wagonjwa, nao wakaponywa magonjwa yao; na wale waliokuwa na pepo wabaya wakatokwa na pepo hao.
13Panašiai ir kai kurie keliaujantys žydų egzorcistai mėgino turėjusiems piktųjų dvasių prišaukti Viešpaties Jėzaus vardą, sakydami: “Mes jus saikdiname Jėzaus vardu, kurį skelbia Paulius”.
13Wayahudi kadhaa wenye kupunga pepo wabaya, walisafiri huko na huko, wakijaribu kulitumia jina la Bwana Yesu kwa wale waliokuwa wamepagawa na pepo wabaya. Walikuwa wakisema: "Ninawaamuru kwa jina la Yesu ambaye Paulo anamhubiri."
14Taip darė vieno žydų vyresniojo kunigo Skėvo septyni sūnūs.
14Watoto saba wa Skewa, Kuhani Mkuu wa Kiyahudi, walikuwa miongoni mwa hao waliokuwa wanafanya hivyo.
15Bet piktoji dvasia jiems atsakė: “Pažįstu Jėzų ir žinau Paulių. O kas jūs esate?”
15Lakini pepo mbaya aliwajibu, "Ninamfahamu Yesu, ninamjua pia Paulo, lakini ninyi ni nani?"
16Ir žmogus, turįs piktąją dvasią, užpuolė juos ir nugalėjo su tokia jėga, kad jie nuogi ir sužaloti išbėgo iš anų namų.
16Kisha yule mtu aliyepagawa aliwarukia wote kwa kishindo, akawashinda nguvu. Na hao watoto wa Skewa wakakimbia kutoka ile nyumba wakiwa uchi na wamejaa majeraha.
17Apie tai sužinojo visi žydai ir graikai, gyvenantys Efeze. Visus apėmė baimė, o Viešpaties Jėzaus vardas buvo išaukštintas.
17Kila mtu huko Efeso, Myahudi na asiye Myahudi, alisikia juu ya tukio hilo. Wote waliingiwa na hofu, wakalitukuza jina la Bwana Yesu.
18Daug įtikėjusiųjų atėję išpažindavo ir pasisakydavo, ką buvo darę.
18Waumini wengi walijitokeza wakakiri hadharani mambo waliyokuwa wametenda.
19Daugelis, užsiiminėjusių magija, sunešė savo knygas ir visų akyse sudegino. Apskaičiuota, kad jos buvo vertos penkiasdešimties tūkstančių sidabro drachmų.
19Wengine waliokuwa wameshughulikia mambo ya uchawi hapo awali, walikusanya vitabu vyao, wakavichoma mbele ya wote. Walikisia gharama ya vitabu hivyo, wakaona yafikia vipande vya fedha elfu hamsini.
20Šitaip galingai Viešpaties žodis plito ir ėmė viršų.
20Kwa namna hiyo, neno la Bwana lilizidi kuenea na kuwa na nguvu zaidi.
21Atlikęs tuos darbus, Paulius dvasioje nusprendė keliauti per Makedoniją ir Achają į Jeruzalę. “Pabuvęs ten,sakė jis,turiu pamatyti ir Romą”.
21Baada ya mambo hayo, Paulo aliamua kwenda Yerusalemu kwa kupitia Makedonia na Akaya. Alisema, "Baada ya kufika huko, itanilazimu kuona Roma pia."
22Jis nusiuntė į Makedoniją du savo pagalbininkus, Timotiejų ir Erastą, o pats kurį laiką pasiliko Azijoje.
22Hivyo, aliwatuma wawili wa wasaidizi wake, Timotheo na Erasto, wamtangulie kwenda Makedonia, naye akabaki kwa muda huko Asia.
23Tuo metu kilo nemažas sąmyšis dėl Kelio.
23Wakati huo ndipo kulipotokea ghasia kubwa huko Efeso kwa sababu ya hiyo Njia ya Bwana.
24Vienas sidabrakalys, vardu Demetrijas, gaminęs sidabrines Artemidės šventyklos miniatiūras ir duodavęs gerai uždirbti amatininkams,
24Kulikuwa na mfua fedha mmoja aitwaye Demetrio, ambaye alikuwa na kazi ya kutengeneza sanamu za nyumba ya mungu wa kike aitwaye Artemi. Shughuli hiyo iliwapatia mafundi faida kubwa.
25susivadino juos bei kitus to amato darbininkus ir kalbėjo: “Vyrai, jūs žinote, kad šiuo amatu remiasi mūsų gerovė.
25Demetrio aliwakusanya hao wafanyakazi pamoja na wengine waliokuwa na kazi kama hiyo, akawaambia, "Wananchi, mnafahamu kwamba kipato chetu kinatokana na biashara hii.
26Bet jūs matote ir girdite, kad tas Paulius ne tik Efeze, bet ir beveik visoje Azijoje įtikino ir nukreipė į šalį daug žmonių, tvirtindamas, esą tai ne dievai, kurie pagaminami žmonių rankomis.
26Sasa, mnaweza kusikia na kujionea wenyewe mambo Paulo anayofanya, si tu hapa Efeso, ila pia kote katika Asia. Yeye amewashawishi na kuwageuza watu wakakubali kwamba miungu ile iliyotengenezwa na watu si miungu hata kidogo.
27Gresia pavojus, kad ne tik nusmuks mūsų amatas, bet kad bus paniekinta didžiosios deivės Artemidės šventykla ir žlugs didybė tos, kurią garbina visa Azija ir visas pasaulis”.
27Hivyo iko hatari kwamba biashara yetu itakuwa na jina baya. Si hivyo tu, bali pia jambo hilo linaweza kuifanya nyumba ya mungu Artemi kuwa si kitu cha maana. Hatimaye sifa zake huyo ambaye Asia na dunia yote inamwabudu, zitakwisha."
28Tai išgirdę, jie labai įniršo ir ėmė šaukti: “Didi efeziečių Artemidė!”
28Waliposikia hayo, waliwaka hasira, wakaanza kupiga kelele: "Mkuu ni Artemi, wa Efeso!"
29Sąmyšis apėmė visą miestą, ir jie, pagriebę Pauliaus palydovus, makedoniečius Gajų ir Aristarchą, visi kaip vienas pasileido bėgti į teatrą.
29Mji wote ukajaa ghasia. Wakawavamia Gayo na Aristarko, wenyeji wa Makedonia, ambao walikuwa wasafiri wenzake Paulo, wakakimbia nao mpaka kwenye ukumbi wa michezo.
30Pauliui panorus įsimaišyti į minią, mokiniai jo neleido.
30Paulo mwenyewe alitaka kuukabili huo umati wa watu, lakini wale waumini walimzuia.
31Taip pat ir keli jo bičiuliai, Azijos valdininkai, per kitus prašė, kad jis neitų į teatrą.
31Maofisa wengine wa huo mkoa wa Asia, waliokuwa rafiki zake, walimtumia Paulo ujumbe wakimsihi asijihatarishe kwa kwenda kwenye ukumbi wa michezo.
32O ten vieni rėkavo vienaip, kitikitaip. Susirinkimas buvo toks pakrikęs, jog daugumas net nežinojo, kuriam galui susirinkta.
32Wakati huo, kila mtu alikuwa anapayuka; wengine hili na wengine lile, mpaka hata ule mkutano ukavurugika. Wengi hawakujua hata sababu ya kukutana kwao.
33Iš minios ištempė Aleksandrą, kurį žydai stūmė į priekį. Aleksandras, pamojęs ranka, norėjo pasiaiškinti miniai.
33Kwa vile Wayahudi walimfanya Aleksanda ajitokeze mbele, baadhi ya watu katika ule umati walidhani kuwa ndiye. Basi, Aleksanda aliwaashiria watu kwa mkono akitaka kujitetea mbele ya ule umati wa watu.
34Bet, pažinę jį esant žydą, visi vienu balsu ėmė rėkti ir kokias dvi valandas šūkavo: “Didi efeziečių Artemidė!”
34Lakini walipotambua kuwa yeye ni Myahudi, wote kwa sauti moja walipiga kelele: "Mkuu ni Artemi wa Efeso!" Wakaendelea kupayukapayuka hivyo kwa muda wa saa mbili.
35Galiausiai miesto raštininkas, nuraminęs minią, pasakė: “Efezo vyrai! Kur rasi žmogų, kuris nežinotų, jog efeziečių miestas garbina didžiąją deivę Artemidę ir iš dangaus nukritusią jos statulą?!
35Hatimaye karani wa mji alifaulu kuwanyamazisha, akawaambia, "Wananchi wa Efeso, kila mtu anajua kwamba mji huu wa Efeso ni mlinzi wa nyumba ya mungu Artemi na mlinzi wa ile sanamu iliyoanguka kutoka mbinguni.
36Šito niekas negali paneigti. Taigi nusiraminkite ir nieko galvotrūkčiais nedarykite.
36Hakuna anayeweza kukana mambo haya. Hivyo basi, tulieni; msifanye chochote bila hadhari.
37Jūs atitempėte čionai šiuos vyrus, kurie nėra nei šventyklos vagys, nei piktžodžiautojai mūsų deivei.
37Mmewaita watu hawa hapa ingawaje hawakuikufuru nyumba ya mungu wala kumtukana mungu wetu wa kike.
38Jei Demetrijas ir jo bendrai amatininkai turi prieš ką nors skundą, tai tam yra teismo dienos ir prokonsulai, tegul sau bylinėjasi.
38Kama, basi Demetrio na wafanyakazi wake wana mashtaka yao kuhusu watu hawa, yapo mahakama na wakuu wa mikoa; wanaweza kushtakiana huko.
39O jeigu jūs turite kokį kitą apsvarstytiną reikalą, tai jį bus galima išspręsti teisėtame susirinkime.
39Kama mna matatizo mengine, yapelekeni katika kikao halali.
40Šiaip jau yra pavojus būti apkaltintiems maištu dėl to, kas šiandien čia dėjosi, nes nėra jokio pagrindo, kuriuo galėtume pateisinti šį sambrūzdį”. Tai pasakęs, jis paleido susirinkimą.
40Kwa maana tungaliweza kushtakiwa kwa kusababisha ghasia kutokana na vituko vya leo. Ghasia hii haina msingi halali na hatungeweza kutoa sababu za kuridhisha za ghasia hiyo."
41Baada ya kusema hayo aliuvunja mkutano.