1Sąmyšiui pasibaigus, Paulius susikvietė mokinius ir atsisveikinęs iškeliavo į Makedoniją.
1Ile ghasia ya Efeso ilipokwisha tulia Paulo aliwaita pamoja wale waumini, akawatia moyo. Kisha akawaaga, akasafiri kwenda Makedonia.
2Keliaudamas per anuos kraštus ir skatindamas mokinius gausiais žodžiais, jis atvyko į Graikiją,
2Alipitia sehemu za nchi zile akiwatia watu moyo kwa maneno mengi. Halafu akafika Ugiriki.
3kur pasiliko tris mėnesius. Kai jam besirengiant plaukti į Siriją žydai ėmė ruošti prieš jį sąmokslą, jis nutarė grįžti atgal per Makedoniją.
3ambako alikaa kwa miezi mitatu. Alipokuwa anajitayarisha kwenda Siria, aligundua kwamba Wayahudi walikuwa wanamfanyia mpango mbaya; hivyo aliamua kurudi kwa kupitia Makedonia.
4Iki Azijos jį lydėjo Sopatras iš Berėjos, Aristarchas ir Sekundas iš Tesalonikos, Gajus iš Derbės ir Timotiejus, Tichikas ir Trofimas iš Azijos.
4Sopatro, mwana wa Pirho kutoka Berea, aliandamana naye; pia Aristarko na Sekundo kutoka Thesalonika, Gayo kutoka Derbe, Timotheo, Tukiko na Trofimo wa mkoa wa Asia.
5Šie iškeliavo pirmiau ir laukė mūsų Troadėje.
5Hao walitutangulia na kutungojea kule Troa.
6Po Neraugintos duonos dienų mes išplaukėme iš Filipų ir per penkias dienas atvykome pas juos į Troadę; ten išbuvome septynias dienas.
6Sisi, baada ya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, tulipanda meli kutoka Filipi na baada ya siku tatu tukawafikia kule Troa. Huko tulikaa kwa muda wa juma moja.
7Pirmą savaitės dieną, mokiniams susirinkus laužyti duonos, Paulius mokė juos ir, kadangi žadėjo rytojaus dieną iškeliauti, tai užtęsė savo kalbą iki vidurnakčio.
7Jumamosi jioni, tulikutana ili kumega mkate. Kwa vile Paulo alikuwa amekusudia kuondoka kesho yake, aliwahutubia watu na kuendelea kuongea nao hadi usiku wa manane.
8Aukštutiniame kambaryje, kur jie buvo susirinkę, degė daug žibintų.
8Katika chumba tulimokuwa, ghorofani, kulikuwa na taa nyingi zinawaka.
9Vienas jaunuolis, vardu Eutichas, sėdėjęs ant lango, giliai įmigo ir, Pauliui ilgiau bedėstant, miego įveiktas, iš trečio aukšto nukrito žemėn. Kai jį pakėlė, jis buvo nebegyvas.
9Kijana mmoja aitwaye Eutuko alikuwa ameketi dirishani wakati Paulo alipokuwa anaendelea kuhutubu. Eutuko alianza kusinzia kidogokidogo na hatimaye usingizi ukambana, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu. Wakamwokota amekwisha kufa.
10Nulipęs žemyn, Paulius pasilenkė ir, apglėbęs jį, tarė: “Nekelkite triukšmo, gyvybė tebėra jame”.
10Lakini Paulo alishuka chini, akainama, akamkumbatia na kusema, "Msiwe na wasiwasi maana kuna uhai bado ndani yake."
11Vėl užlipęs aukštyn, jis laužė ir valgė duoną. Dar ilgai jis kalbėjo, lig pat aušros, ir tada iškeliavo.
11Kisha akapanda tena ghorofani, akamega mkate, akala. Aliendelea kuhubiri kwa muda mrefu hadi alfajiri, halafu akaondoka.
12O jaunuolį atvedė gyvą, ir tai buvo nemaža paguoda.
12Wale watu walimchukua yule kijana nyumbani akiwa mzima kabisa, wakapata kitulizo kikubwa.
13Mes, nuėję ir įsėdę į laivą, išplaukėme į Asą, kur ketinome paimti Paulių, nes jis buvo taip patvarkęs, pats norėdamas ten nuvykti pėsčias.
13Sisi tulipanda meli tukatangulia kwenda Aso ambako tungemchukua Paulo. Ndivyo alivyopanga; maana alitaka kufika huko kwa kupitia nchi kavu.
14Kai jis susitiko su mumis Ase, paėmę jį, nuplaukėme į Mitilėnę.
14Basi, alitukuta kule Aso, tukampandisha melini, tukaenda Mitulene.
15Iš ten plaukdami toliau, kitą dieną atsidūrėme priešais Chiją. Rytojaus dieną pasiekėme Samą ir, pabuvę Trogilione, dar po dienos atvykome į Miletą.
15Kutoka huko tulisafiri tukafika Kio kesho yake. Siku ya pili, tulitia nanga Samo na kesho yake tukafika Mileto.
16Kad netektų gaišti Azijoje, Paulius nutarė aplenkti Efezą, nes jis skubėjo, norėdamas, jei įmanoma, Sekminių dieną būti Jeruzalėje.
16Paulo alikuwa amekusudia kuendelea na safari kwa meli bila kupitia Efeso ili asikawie zaidi huko Asia. Alikuwa na haraka ya kufika Yerusalemu kwa sikukuu ya Pentekoste kama ingewezekana.
17Iš Mileto jis pasiuntė į Efezą pakviesti bažnyčios vyresniųjų.
17Kutoka Mileto Paulo alituma ujumbe kwa wazee wa Efeso wakutane naye.
18Kai jie pas jį atvyko, Paulius prabilo: “Jūs žinote, kaip nuo pirmosios dienos, kurią įžengiau į Aziją, visą laiką pas jus elgiausi,
18Walipofika kwake aliwaambia, "Mnajua jinsi nilivyotumia wakati wote pamoja nanyi tangu siku ile ya kwanza nilipofika Asia.
19tarnaudamas Viešpačiui su visu nusižeminimu, ašaromis ir išbandymais, kurie ištiko mane dėl žydų pinklių.
19Mnajua jinsi nilivyomtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote, kwa machozi na matatizo yaliyonipata kutokana na mipango ya hila ya Wayahudi.
20Kaip nieko nenutylėjau, kas naudinga, bet kalbėjau ir mokiau jus tiek viešumoje, tiek po namus,
20Mnajua kwamba sikusita hata kidogo kuwahubiria hadharani na nyumbani mwenu na kuwafundisha chochote ambacho kingewasaidieni.
21liudydamas žydams ir graikams apie atgailą prieš Dievą ir tikėjimą mūsų Viešpačiu Jėzumi Kristumi.
21Niliwaonya wote--Wayahudi kadhalika na watu wa mataifa, wamgeukie Mungu na kumwamini Bwana wetu Yesu.
22Ir štai dabar aš, dvasios kalinys, keliauju į Jeruzalę, nežinodamas, kas man ten nutiks,
22Sasa, sikilizeni! Mimi, nikiwa ninamtii Roho, nakwenda Yerusalemu bila kufahamu yatakayonipata huko.
23tiktai Šventoji Dvasia kiekviename mieste man liudija, sakydama, kad manęs laukia pančiai ir suspaudimai.
23Ninachojua tu ni kwamba Roho Mtakatifu ananithibitishia katika kila mji kwamba vifungo na mateso ndivyo vinavyoningojea.
24Bet tai man nesvarbu, ir aš nebranginu savo gyvybės. Svarbu, kad tik su džiaugsmu baigčiau savo bėgimą ir tarnavimą, kurį gavau iš Viešpaties Jėzaus: liudyti Dievo malonės Evangeliją.
24Lakini, siuthamini uhai wangu kuwa ni kitu sana kwangu. Nataka tu nikamilishe ule utume wangu na kumaliza ile kazi aliyonipa Bwana Yesu niifanye, yaani nitangaze Habari Njema ya neema ya Mungu.
25Ir štai dabar aš žinau, kad jūs visi, su kuriais buvau skelbdamas Dievo karalystę, daugiau nebematysite mano veido.
25"Nimekuwa nikienda huko na huko kati yenu nikiuhubiri Ufalme wa Mungu. Sasa lakini, najua hakuna hata mmoja wenu atakayeniona tena.
26Todėl šiandien jums liudiju, jog esu švarus nuo visų kraujo.
26Hivyo, leo hii ninawathibitishieni rasmi kwamba ikijatokea akapotea mmoja wenu, mimi sina lawama yoyote.
27Aš nevengiau jums paskelbti visų Dievo nutarimų.
27Kwa maana sikusita hata kidogo kuwatangazieni azimio lote la Mungu.
28Būkite rūpestingi sau ir visai kaimenei, kuriai Šventoji Dvasia jus paskyrė prižiūrėtojais, kad ganytumėte Dievo bažnyčią, kurią Jis įsigijo savo krauju.
28Jihadharini wenyewe; lilindeni lile kundi ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi muwe walezi wake. Lichungeni kanisa la Mungu ambalo amejipatia kwa damu ya Mwanae.
29Nes aš žinau, kad, man pasitraukus, įsibraus pas jus žiaurių vilkų, kurie nepagailės kaimenės.
29Nafahamu vizuri sana kwamba baada ya kuondoka kwangu mbwa mwitu wakali watawavamieni, na hawatakuwa na huruma kwa kundi hilo.
30Net iš jūsų atsiras tokių, kurie kreivomis kalbomis stengsis patraukti paskui save mokinius.
30Hata kutoka miongoni mwenu watatokea watu ambao watasema mambo ya uongo ili kuwapotosha watu na kuwafanya wawafuate wao tu.
31Todėl budėkite ir nepamirškite, kad aš per trejus metus dieną ir naktį nepaliaudamas, su ašaromis įspėjinėjau kiekvieną.
31Kwa hiyo, muwe macho mkikumbuka kwamba kwa muda wa miaka mitatu, usiku na mchana, sikuchoka kumwonya kila mmoja wenu kwa machozi.
32O dabar, broliai, pavedu jus Dievui ir Jo malonės žodžiui, kuris turi galią jus išugdyti ir duoti jums paveldėjimą tarp visų pašventintųjų.
32"Na sasa basi, ninawaweka ninyi chini ya ulinzi wa Mungu na ujumbe wa neema yake. Yeye anao uwezo wa kuwajenga ninyi na kuwawezesha mzipate zile baraka alizowawekea watu wake.
33Nė iš vieno negeidžiau nei sidabro, nei aukso, nei drabužio.
33Mimi sikutamani hata mara moja fedha, wala dhahabu, wala nguo za mtu yeyote.
34Jūs žinote, kad mano ir buvusiųjų su manimi reikalams tarnavo šitos va mano rankos.
34Mnajua ninyi wenyewe kwamba nimefanya kazi kwa mikono yangu mwenyewe, ili kujipatia mahitaji yangu na ya wenzangu.
35Ir aš jums visur rodydavau, kad, šitaip triūsiant, reikia paremti silpnuosius ir atminti Viešpaties Jėzaus pasakytus žodžius: ‘Labiau palaiminta duoti negu imti’ ”.
35Nimekuwa nikiwapeni daima mfano kwamba kwa kufanya kazi mithili hiyo tunapaswa kuwasaidia walio dhaifu, tukikumbuka maneno ya Bwana Yesu mwenyewe: Heri zaidi kutoa kuliko kupokea."
36Tai pasakęs, jis atsiklaupė ir kartu su visais pasimeldė.
36Baada ya kusema hayo, Paulo alipiga magoti pamoja nao wote, akasali.
37Visi pradėjo graudžiai verkti ir, puldami Pauliui ant kaklo, jį bučiavo.
37Wote walikuwa wanalia; wakamwaga kwa kumkumbatia na kumbusu.
38Jie ypač nuliūdo dėl žodžių, kad daugiau nebematysią jo veido. Po to jie palydėjo jį į laivą.
38Jambo lililowahuzunisha zaidi lilikuwa neno alilosema kwamba hawangemwona tena. Basi, wakamsindikiza hadi melini.