1Išsiplėšę iš jų glėbio, išplaukėme ir tiesiu keliu atvykome į Kosą, o kitą dieną į Rodą ir iš ten į Patarą.
1Tulipokwisha agana nao, tulipanda meli tukaenda moja kwa moja mpaka Kosi. Kesho yake tulifika Rodo, na kutoka huko tulikwenda Patara.
2Radę laivą, plaukiantį į Finikiją, įlipome ir išplaukėme.
2Huko, tulikuta meli iliyokuwa inakwenda Foinike, hivyo tulipanda, tukasafiri.
3Išvydę artėjant Kiprą, palikome jį kairėje ir leidomės link Sirijos, kur išlipome Tyre. Ten laivas turėjo iškrauti savo krovinius.
3Baada ya kufika mahali ambapo tuliweza kuona Kupro, tulipitia upande wake wa kusini tukaelekea Siria. Tulitia nanga katika mji wa Tiro ambapo ile meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake.
4Suradę mokinių, išbuvome su jais septynias dienas. Dvasios paskatinti, jie sakė Pauliui nevykti į Jeruzalę.
4Tulikuta waumini huko, tukakaa pamoja nao kwa muda wa juma moja. Waumini hao wakawa waongea kwa nguvu ya Roho, wakamwambia Paulo asiende Yerusalemu.
5Praėjus toms dienoms, mes išėjome ir leidomės į kelionę, o jie visi kartu su žmonomis ir vaikais palydėjo mus iki miesto ribos. Pajūryje suklaupę visi pasimeldėme.
5Lakini muda wetu ulipokwisha tuliondoka. Wote pamoja na wanawake na watoto wao walitusindikiza mpaka nje ya mji. Tulipofika pwani, sote tulipiga magoti tukasali.
6Vieni su kitais atsisveikinę, sulipome į laivą, o jie sugrįžo namo.
6Kisha tuliagana; sisi tukapanda meli nao wakarudi makwao.
7Keliaudami toliau iš Tyro atplaukėme į Ptolemaidę. Ten pasveikinome brolius ir pasilikome pas juos vienai dienai.
7Sisi tuliendelea na safari yetu kutoka Tiro tukafika Tolemai ambapo tuliwasalimu ndugu zetu, tukakaa nao siku moja.
8Kitą dieną Paulius ir mes, buvę su juo, vėl iškeliavome ir atvykome į Cezarėją. Ten nuėjome į evangelisto Pilypo, vieno iš septynių, namus ir pas jį pasilikome.
8Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisarea. Huko Kaisarea tulikwenda nyumbani kwa mhubiri Filipo. Yeye alikuwa mmoja wa wale saba waliochaguliwa kule Yerusalemu.
9Jis turėjo keturias netekėjusias dukteris, kurios pranašaudavo.
9Alikuwa na binti watatu ambao walikuwa na kipaji cha unabii.
10Mums bebūnant ten daugiau dienų, iš Judėjos atėjo vienas pranašas, vardu Agabas.
10Baada ya kukaa huko siku kadhaa, nabii mmoja aitwaye Agabo alifika kutoka Yudea.
11Atėjęs pas mus, jis paėmė Pauliaus juostą ir, susirišęs ja rankas ir kojas, tarė: “Taip sako Šventoji Dvasia: ‘Vyrą, kuriam priklauso ši juosta, taip Jeruzalėje supančios žydai ir atiduos į pagonių rankas’ ”.
11Alitujia, akachukua mkanda wa Paulo, akajifunga mikono na miguu, akasema "Roho Mtakatifu asema hivi: Wayahudi kule Yerusalemu watamfunga namna hii mtu mwenye ukanda na kumtia mikononi mwa watu wa mataifa."
12Tai išgirdę, ir mes, ir tenykščiai prašėme, kad jis neitų į Jeruzalę.
12Tuliposikia hayo, sisi na wale watu wengine waliokuwa hapo tulimsihi Paulo asiende Yerusalemu.
13Bet Paulius atsakė: “Kodėl raudate ir draskote man širdį? Aš pasirengęs Jeruzalėje dėl Viešpaties Jėzaus ne tik būti supančiotas, bet ir numirti!”
13Lakini yeye alijibu, "Mnataka kufanya nini? Mnataka kuvunja moyo wangu kwa machozi? Niko tayari siyo tu kutiwa ndani kule Yerusalemu, ila hata kufa kwa ajili ya Bwana Yesu."
14Jam nesiduodant perkalbamam, mes nurimome ir tarėme: “Tebūnie Viešpaties valia!”
14Tuliposhindwa kumshawishi tulinyamaza, tukasema tu: "Mapenzi ya Bwana yafanyike"
15Po tų dienų, susiruošę į kelią, išvykome į Jeruzalę.
15Baada ya kukaa pale kwa muda, tulifunga mizigo yetu, tukaendelea na safari kwenda Yerusalemu.
16Mus lydėjo kai kurie mokiniai iš Cezarėjos ir nuvedė apsistoti pas vieną kiprietį, seną mokinį Mnasoną.
16Wengine kati ya wale wafuasi wa Kaisarea walienda pamoja nasi, wakatupeleka nyumbani kwa Mnasoni ambaye tulikuwa tunakwenda kukaa naye kwa muda. Mnasoni alikuwa mwenyeji wa Kupro na alikuwa amekuwa muumini kwa siku nyingi.
17Kai atvykome į Jeruzalę, broliai mus džiaugsmingai priėmė.
17Tulipofika Yerusalemu, ndugu waumini walitupokea vizuri sana.
18Kitą dieną Paulius kartu su mumis nuėjo pas Jokūbą, kur buvo susirinkę visi vyresnieji.
18Kesho yake Paulo alikwenda pamoja nasi kumwamkia Yakobo, na wazee wote wa kanisa walikuwako pia.
19Juos pasveikinęs, jis smulkiai išdėstė visa, ką Dievas padarė pagonijoje per jo tarnystę.
19Baada ya kuwasalimu, Paulo aliwapa taarifa kamili kuhusu yote Mungu aliyokuwa ametenda kati ya mataifa kwa njia ya utumishi wake.
20Jie išklausę šlovino Viešpatį ir tarė Pauliui: “Tu matai, broli, kiek daug tūkstančių žydų tapo tikinčiaisiais, ir jie visi uoliai laikosi Įstatymo.
20Waliposikia hayo, walimtukuza Mungu. Kisha wakamwambia Paulo, "Ndugu, unaweza kuona kwamba kuna maelfu ya Wayahudi ambao sasa wamekuwa waumini na wote hao wanashika kwa makini Sheria ya Mose.
21Bet jiems prikalbėta apie tave, kad tu mokai visus žydus, gyvenančius tarp pagonių, atsižadėti Mozės, sakydamas, jog jiems nereikia apipjaustyti vaikų nei laikytis papročių.
21Wamepata habari zako kwamba umekuwa ukiwafundisha Wayahudi wanaoishi kati ya mataifa mengine kuwa wasiijali Sheria ya Mose, wasiwatahiri watoto wao na kwamba wasizifuate mila za Wayahudi.
22Ką daryti? Jie būtinai susirinks, išgirdę, kad esi atvykęs.
22Sasa, mambo yatakuwaje? Ni dhahiri kuwa watapata habari kwamba umekwisha wasili hapa.
23Todėl padaryk, kaip tau sakome. Pas mus yra keturi vyrai, padarę įžadą.
23Basi, fanya kama tunavyokushauri. Tunao hapa watu wanne ambao wameweka nadhiri.
24Pasiimk juos, apsivalyk kartu su jais ir prisiimk jų išlaidas, kad jie galėtų nusikirpti plaukus. Tada visi pamatys, jog gandai apie tave nieko verti ir tu nenukrypdamas laikaisi Įstatymo.
24Jiunge nao katika ibada ya kujitakasa, ukalipe na gharama zinazohusika, kisha wanyolewe nywele zao. Hivyo watu wote watatambua kwamba habari zile walizoambiwa juu yako hazina msingi wowote, na kwamba wewe binafsi bado unaishi kufuatana na maagizo ya Sheria za Mose.
25O dėl tikinčiųjų iš pagonių, tai mes išsiuntėme nurodymus, kad jie saugotųsi to, kas paaukota stabams, kraujo, pasmaugtų gyvulių mėsos ir ištvirkavimo”.
25Kuhusu wale watu wa mataifa mengine ambao wamekuwa waumini, tumekwisha wapelekea barua tukiwaambia mambo tuliyoamua: wasile chochote kilichotambikiwa miungu ya uongo, wasinywe damu, wasile nyama ya mnyama aliyenyongwa, na wajiepushe na uasherati."
26Tada Paulius pasiėmė tuos vyrus ir kitą dieną su jais apsivalęs įėjo į šventyklą. Ten jis nurodė apsivalymo dienų pabaigą, kada už kiekvieną iš jų turės būti paaukota auka.
26Basi, kesho yake Paulo aliwachukua wale watu akafanya ibada ya kujitakasa pamoja nao. Kisha akaingia Hekaluni kutoa taarifa kuhusu mwisho wa siku za kujitakasa na kuhusu dhabihu itakayotolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
27Toms septynioms dienoms baigiantis, žydai iš Azijos, pastebėję Paulių šventykloje, sukurstė visą minią ir, nutvėrę jį,
27Wakati siku hizo saba zilipokaribia kuisha, Wayahudi waliokuwa wametoka katika mkoa wa Asia walimwona Paulo Hekaluni. Wakachochea hasira kati ya kundi lote la watu, wakamtia nguvuni
28ėmė šaukti: “Izraelio vyrai, padėkite! Šitas žmogus visur visus moko prieš tautą, Įstatymą ir šią vietą. Jis net atsivedė šventyklon graikus ir suteršė šią šventą vietą”.
28wakipiga kelele: "Wananchi wa Israeli, msaada, msaada! Huyu ndiye yule mtu anayewafundisha watu kila mahali mambo yanayopinga watu wa Israeli, yanayopinga Sheria ya Mose na mahali hapa patakatifu. Hata sasa amewaingiza watu wa mataifa mengine Hekaluni na kupatia najisi mahali hapa patakatifu."
29Mat jie prieš tai matė su juo mieste Trofimą iš Efezo ir manė, kad Paulius jį atsivedęs į šventyklą.
29Sababu ya kusema hivyo ni kwamba walikuwa wamemwona Trofimo mwenyeji, wa Efeso, akiwa pamoja na Paulo mjini, wakadhani kwamba Paulo alikuwa amemwingiza Hekaluni.
30Sujudo visas miestas, subėgo žmonės, nutvėrė Paulių ir ištempė jį iš šventyklos. Durys bematant buvo uždarytos.
30Mji wote ulienea ghasia; watu wakaja kutoka pande zote, wakamkamata Paulo, wakamburuta, wakamtoa nje ya Hekalu na papo hapo milango ya Hekalu ikafungwa.
31Jiems ketinant jį užmušti, įgulos viršininkuitribūnui buvo duota žinia, kad visoje Jeruzalėje kyla sąmyšis.
31Walikuwa tayari kumuua, lakini habari zilimfikia mkuu wa jeshi la Kiroma kuwa Yerusalemu yote ilikuwa imejaa ghasia.
32Jis nedelsdamas su kareiviais ir šimtininkais atskubėjo ten. Jie, pamatę tribūną ir kareivius, liovėsi mušę Paulių.
32Mara, mkuu wa jeshi akawachukua askari na jemadari, akalikabili lile kundi la watu. Nao walipomwona mkuu wa jeshi na askari, wakaacha kumpiga Paulo.
33Prisiartinęs tribūnas suėmė Paulių ir įsakė surišti dviem grandinėmis. Paskui paklausė, kas jis esąs ir ką padaręs.
33Mkuu wa jeshi alimwendea Paulo, akamtia nguvuni na kuamuru afungwe minyororo miwili. Kisha akauliza, "Ni mtu gani huyu, na amefanya nini?"
34Tuo tarpu iš minios šaukė tai šį, tai tą. Negalėdamas dėl triukšmo nieko tikro apie jį sužinoti, tribūnas įsakė nuvesti Paulių į kareivines.
34Wengine katika lile kundi la watu walikuwa wanapayuka kitu hiki na wengine kitu kingine. Kwa sababu ya ghasia hiyo, mkuu wa jeshi hakufaulu kujua kisa kamili. Hivyo, aliamuru watu wake wampeleke Paulo ndani ya ngome.
35Atėjus prie laiptų, dėl minios įsisiautėjimo kareiviams teko jį nešte nešti.
35Paulo alipofika kwenye ngazi, askari walilazimika kumbeba kwa sababu ya fujo za watu.
36Nes žmonių minia sekė iš paskos, šaukdama: “Mirtis jam!”
36Kwa maana kundi kubwa la watu walimfuata wakipiga kelele, "Muulie mbali!"
37Vedamas į kareivines, Paulius kreipėsi į tribūną: “Ar galiu tau šį tą pasakyti?” Šis atsiliepė: “Tu moki graikiškai?
37Walipokuwa wanamwingiza ndani ya ngome, Paulo alimwomba mkuu wa jeshi akisema, "Naweza kukwambia kitu?" Yule mkuu wa jeshi akamjibu, "Je unajua Kigiriki?
38Tai tune anas egiptietis, kuris neseniai sukėlė sąmyšį ir išsivedė į dykumą keturis tūkstančius vyrų žudikų?”
38Kwani wewe si yule Mmisri ambaye hivi majuzi alianzisha uasi na kuwaongoza majahili elfu nne hadi jangwani?"
39Paulius atsakė: “Aš esu žydas iš Kilikijos Tarso, taigi žymaus miesto pilietis. Prašau tavęs, leisk man prabilti žmonėms”.
39Paulo akajibu, "Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia; mimi ni raia wa mji maarufu. Tafadhali, niruhusu niongee na watu.
40Tribūnas sutiko. Paulius atsistojo ant laiptų ir pamojo ranka miniai. Visiems nutilus, jis prabilo hebrajų kalba:
40Yule mkuu wa jeshi akamruhusu. Hivyo Paulo alisimama juu ya ngazi, akawapungia mkono wale watu na walipokaa kimya, akaanza kuongea nao kwa Kiebrania.