1“Vyrai broliai ir tėvai! Paklausykite, ką dabar pasakysiu sau apginti”.
1"Ndugu zangu na akina baba, nisikilizeni sasa nikijitetea mbele yenu!"
2Išgirdę jį kreipiantis į juos hebrajiškai, jie dar labiau nurimo. O jis kalbėjo toliau:
2Waliposikia akiongea nao kwa Kiebrania wakazidi kukaa kimya zaidi kuliko hapo awali. Naye Paulo akaendelea kusema,
3“Aš esu žydas, gimęs Tarse, Kilikijoje, bet išauklėtas šitame mieste, prie Gamalielio kojų, tobulai išmokytas pagal mūsų protėvių Įstatymą, ir buvau ypatingai uolus dėl Dievo, kaip ir jūs visi šiandien.
3"Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia. Lakini nililelewa papa hapa mjini Yerusalemu chini ya mkufunzi Gamalieli. Nilifundishwa kufuata kwa uthabiti Sheria ya wazee wetu. Nilijitolea kwa moyo wote kwa Mungu kama ninyi wenyewe mlivyo hivi leo.
4Todėl iki mirties persekiojau šį Kelią, pančiodamas ir mesdamas į kalėjimą vyrus ir moteris.
4Niliwatesa hata kuwaua wale watu waliofuata Njia hii. Niliwatia nguvuni wanaume kwa wanawake na kuwafunga gerezani.
5Tai gali paliudyti ir vyriausiasis kunigas, ir visa vyresniųjų taryba. Iš jų buvau gavęs laiškus broliams ir keliavau į Damaską, kad tenykščius surištus atgabenčiau į Jeruzalę nubausti.
5Kuhani Mkuu na baraza lote la wazee wanaweza kushuhudia jambo hilo. Kutoka kwao nilipokea barua walioandikiwa wale ndugu Wayahudi waliokuwa huko Damasko. Nilikwenda Damasko ili niwatie nguvuni watu hao na kuwaleta wamefungwa mpaka Yerusalemu ili waadhibiwe.
6Man keliaujant ir artinantis prie Damasko, apie vidurdienį staiga mane apšvietė ryški šviesa iš dangaus.
6"Basi, nilipokuwa njiani karibu kufika Damasko, yapata saa sita mchana, mwangu mkubwa kutoka mbinguni ulitokea ghafla ukaniangazia pande zote.
7Aš kritau ant žemės ir išgirdau balsą, man sakantį: ‘Sauliau, Sauliau, kam mane persekioji?’
7Hapo nilianguka chini, nikasikia sauti ikiniambia: Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa?
8Aš paklausiau: ‘Kas Tu esi, Viešpatie?’ Jis man atsakė: ‘Aš esu Jėzus iš Nazareto, kurį tu persekioji’.
8Nami nikauliza: Nani wewe, Bwana? Naye akaniambia: Mimi ni Yesu wa Nazareti ambaye wewe unamtesa.
9Buvusieji su manimi matė šviesą ir išsigando, bet negirdėjo man kalbančiojo balso.
9Wale wenzangu waliuona ule mwanga lakini hawakusikia sauti ya yule aliyeongea nami.
10Aš dar paklausiau: ‘Ką man daryti, Viešpatie?’ O Viešpats man tarė: ‘Kelkis, eik į Damaską, tenai tau bus pasakyta visa, ką tau reikia daryti’.
10Basi, mimi nikauliza: Nifanye nini Bwana? Naye Bwana akaniambia: Simama, nenda Damasko na huko utaambiwa yote ambayo umepangiwa kufanya.
11Kadangi tos šviesos šlovės apakintas nieko nebemačiau, palydovų už rankos vedamas pasiekiau Damaską.
11Kutokana na ule mwanga mkali sikuweza kuona na hivyo iliwabidi wale wenzangu kuniongoza kwa kunishika mkono mpaka nikafika Damasko.
12Toksai Ananijas, Įstatymo požiūriu dievotas vyras, apie kurį gerai liudijo visi aplinkiniai žydai,
12"Huko kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Anania, mtu mcha Mungu, mwenye kuitii Sheria yetu na aliyeheshimika sana mbele ya Wayahudi waliokuwa wanaishi Damasko.
13atėjęs stojo prieš mane ir tarė: ‘Broli Sauliau, praregėk!’ Ir tą pačią akimirką aš jį pamačiau.
13Yeye alikuja kuniona, akasimama karibu nami, akasema: Ndugu Saulo! Ona tena. Papo hapo nikaona tena, nikamwangalia.
14O jis kalbėjo: ‘Mūsų protėvių Dievas išsirinko tave, kad pažintum Jo valią, išvystum Teisųjį ir išgirstum balsą iš Jo lūpų,
14Halafu Anania akasema: Mungu wa babu zetu amekuchagua upate kujua matakwa yake na kumwona yule mtumishi wake mwadilifu na kumsikia yeye mwenyewe akiongea.
15nes tu būsi Jo liudytojas visiems žmonėms, skelbdamas, ką girdėjai ir regėjai.
15Kwa maana utamshuhudia kwa watu wote ukiwaambia yale uliyoyaona na kuyasikia.
16Tad ko lauki? Kelkis, pasikrikštyk ir nusiplauk nuodėmes, šaukdamasis Viešpaties vardo!’
16Sasa basi, ya nini kukawia zaidi? Simama ubatizwe na uondolewe dhambi zako kwa kuliungama jina lake.
17Vėliau, sugrįžęs į Jeruzalę ir melsdamasis šventykloje, patyriau Dvasios pagavą
17"Basi, nilirudi Yerusalemu, na nilipokuwa nikisali Hekaluni, niliona maono.
18ir išvydau Jėzų. Jis pasakė: ‘Skubiai pasitrauk iš Jeruzalės, nes jie nepriims tavo liudijimo apie mane’.
18Nilimwona Bwana akiniambia: Haraka! Ondoka Yerusalemu upesi kwa maana watu wa hapa binadamu hawataukubali ushuhuda wako juu yangu.
19Aš atsiliepiau: ‘Viešpatie, juk jie žino, kad Tavo tikinčiuosius iš visų sinagogų mesdavau į kalėjimą ir plakdavau.
19Nami nikamjibu: Bwana, wao wanajua wazi kwamba mimi ni yule aliyekuwa anapitapita katika masunagogi na kuwatia nguvuni na kuwapiga wale waliokuwa wanakuamini.
20O kai buvo pralietas tavo liudytojo Stepono kraujas, aš ten stovėjau pritardamas jo nužudymui ir saugodamas žudikų drabužius’.
20Na kwamba wakati shahidi wako Stefano alipouawa, mimi binafsi nilikuwako pale nikakubaliana na kitendo hicho na kuyalinda makoti ya wale waliokuwa wanamuua.
21Bet Jis tarė man: ‘Eik, nes Aš siųsiu tave toli, pas pagonis’ ”.
21Naye Bwana akaniambia: Nenda; ninakutuma mbali kwa mataifa mengine."
22Jie klausėsi jo iki šitų žodžių, o čia ėmė garsiai šaukti: “Nušluoti nuo žemės jį! Tokiam nevalia gyventi!”
22Mpaka hapa, wale watu walikuwa wanamsikiza, lakini aliposema maneno haya, walianza kusema kwa sauti kubwa, "Mwondoe duniani! Mtu wa namna hiyo hastahili kuishi."
23Jie klykė, mosavo drabužiais ir svaidė į orą smėlį.
23Waliendelea kupayukapayuka huku wakitikisa makoti yao na kurusha vumbi angani.
24Tribūnas įsakė nuvesti Paulių į kareivines ir liepė tardyti plakant, kad išsiaiškintų, kodėl žmonės prieš jį taip rėkė.
24Mkuu wa jeshi aliwaamuru watu wake wampeleke Paulo ndani ya ngome, akawaambia wamchape viboko ili wapate kujua kisa cha Wayahudi kumpigia kelele.
25Kai jau buvo pririštas diržais, Paulius kreipėsi į šalia stovintį šimtininką: “Ar jums leista plakti Romos pilietį, ir dar nenuteistą?”
25Lakini walipokwisha mfunga ili wamchape viboko, Paulo alimwuliza jemadari mmoja aliyesimama hapo, "Je, ni halali kwenu kumpiga viboko raia wa Roma kabla hajahukumiwa?"
26Tai išgirdęs, šimtininkas priėjo prie tribūno ir pasakė: “Žiūrėk, ką darai! Tas žmogus yra Romos pilietis”.
26Yule jemadari aliposikia hayo, alimpasha habari mkuu wa jeshi akisema, "Unataka kufanya nini? Mtu huyu ni raia wa Roma!"
27Tribūnas atėjęs paklausė: “Pasakyk man, ar tu Romos pilietis?” Paulius atsakė: “Taip”.
27Basi, mkuu wa jeshi alimwendea Paulo, akamwambia, "Niambie; je, wewe ni raia wa Roma?" Paulo akamjibu, "Naam."
28Tribūnas tarė: “Aš šitą pilietybę įsigijau už didelius pinigus”. Paulius atsiliepė: “O aš turiu ją nuo gimimo”.
28Mkuu wa jeshi akasema, "Mimi nami nimekuwa raia wa Roma kwa kulipa gharama kubwa." Paulo akasema, "Lakini mimi ni raia wa Roma kwa kuzaliwa."
29Bematant pasitraukė nuo jo tie, kurie turėjo jį tardyti. Tribūnas išsigando, sužinojęs, kad Paulius yra Romos pilietis, ir kad jį surišo.
29Wale watu ambao walikuwa tayari kumchunguza Paulo walitoweka mara. Hata yule mkuu wa jeshi aliogopa alipojua kwamba Paulo ni raia wa Roma na kwamba alikuwa amekwisha mfunga minyororo.
30Rytojaus dieną, norėdamas tiksliau išsiaiškinti, kuo jis žydų kaltinamas, tribūnas išlaisvino jį iš grandinių, liepė sušaukti aukštuosius kunigus bei visą sinedrioną ir, atvedęs Paulių, pastatė jų akivaizdoje.
30Kesho yake, mkuu wa jeshi alitaka kujua mashtaka kamili ambayo Wayahudi walikuwa wamemwekea Paulo. Hivyo, alimfungua Paulo minyororo, akaamuru makuhani wakuu na Baraza lote wafanye kikao. Kisha alimleta Paulo, akamsimamisha mbele ya Baraza.