Lithuanian

Swahili: New Testament

Acts

23

1Skvarbiu žvilgsniu permetęs sinedrioną, Paulius prabilo: “Vyrai broliai! Iki šios dienos elgiausi Dievo akivaizdoje visiškai gryna sąžine”.
1Paulo aliwakodolea macho wale wanabaraza, halafu akaanza kusema, "Ndugu zangu, mpaka hivi leo nimekuwa nikiishi na dhamiri njema mbele ya Mungu."
2Bet vyriausiasis kunigas Ananijas įsakė šalia stovintiesiems smogti jam per burną.
2Hapo Kuhani Mkuu Anania akaamuru wale waliokuwa wamesimama karibu na Paulo wampige kofi mdomoni.
3Tuomet Paulius jam tarė: “Tau smogs Dievas, tu, pabaltinta siena! Tu čia sėdi, kad mane teistum pagal Įstatymą, o liepi mane mušti prieš Įstatymą?”
3Basi, Paulo akamwambia, "Mungu mwenyewe atakupiga kofi wewe uliye kama ukuta uliopakwa chokaa! Unawezaje kukaa hapo ili unihukumu kisheria na huku wewe mwenyewe unaivunja Sheria kwa kuamuru nipigwe?"
4Šalia esantys tarė: “Tu keiki vyriausiąjį Dievo kunigą?!”
4Watu waliokuwa wamesimama pale wakamwambia Paulo, "Unamtukana Kuhani Mkuu wa Mungu!"
5Paulius atsiliepė: “Broliai, aš nežinojau, kad jis vyriausiasis kunigas. Juk parašyta: ‘Nepiktžodžiauk savo tautos vadovui’ ”.
5Paulo akajibu, "Ndugu zangu, sikujua kama yeye ni Kuhani Mkuu. Maana Maandiko yasema hivi: Usiseme vibaya juu ya mtawala wa watu wako."
6Supratęs, kad viena dalis buvo sadukiejai, o kita­fariziejai, Paulius sušuko sinedrionui: “Vyrai broliai, aš fariziejus, fariziejaus sūnus, ir esu teisiamas už mirusiųjų prisikėlimo viltį!”
6Wakati huo Paulo alikwisha tambua kwamba sehemu moja ya wanabaraza wale ilikuwa ni Masadukayo na nyingine Mafarisayo. Basi, alipaaza sauti yake mbele ya Baraza: "Ndugu zangu, mimi ni Mfarisayo, mwana wa Mfarisayo. Mimi nimeletwa mahakamani kwa kuwa ninatumaini kwamba wafu watafufuka."
7Jam tai pasakius, tarp fariziejų ir sadukiejų kilo barnis, ir susirinkimas suskilo.
7Baada ya kusema hivyo, mzozo mkali ulitokea kati ya Mafarisayo na Masadukayo na mkutano ukagawanyika sehemu mbili.
8Mat sadukiejai sako, kad nėra nei prisikėlimo, nei angelų, nei dvasios, o fariziejai tuos dalykus pripažįsta.
8Kisa chenyewe kilikuwa hiki: Masadukayo hushikilia kwamba wafu hawafufuki, hakuna malaika, na roho nazo hazipo. Lakini Mafarisayo husadiki hayo yote matatu.
9Todėl kilo didelis triukšmas. Atsistoję fariziejų pusės Rašto žinovai griežtai prieštaravo, sakydami: “Mes nerandame nieko blogo šitame žmoguje. O jeigu jam kalbėjo dvasia arba angelas, nesipriešinkime Dievui!”
9Kelele ziliongezeka na baadhi ya walimu wa Sheria wa kikundi cha Mafarisayo walisimama na kutoa malalamiko yao kwa nguvu: "Hatuoni chochote kilicho kiovu katika mtu huyu; huenda ikawa kwamba roho au malaika ameongea naye."
10Įsisiautėjus smarkiam ginčui, tribūnas, bijodamas, kad jie nesudraskytų Pauliaus, įsakė kareivių daliniui nusileisti žemyn, išplėšti Paulių iš jų ir nuvesti į kareivines.
10Mzozo ulizidi kuwa mwingi hata mkuu wa jeshi akaogopa kwamba Paulo angeraruliwa vipandevipande. Kwa hiyo, aliwaamuru askari wake kuingia kati ya lile kundi, wamtoe Paulo na kumrudisha ndani ya ngome.
11Kitą naktį šalia jo stojo Viešpats ir tarė: “Būk drąsus, Pauliau! Kaip liudijai apie mane Jeruzalėje, taip turėsi liudyti ir Romoje”.
11Usiku uliofuata, Bwana alisimama karibu na Paulo, akamwambia, "Jipe moyo! Umenishuhudia katika Yerusalemu, utafanya vivyo hivyo mjini Roma."
12Dieną slaptai susirinko žydų būrys ir prisiekė nei valgyti, nei gerti, kol nužudys Paulių.
12Kulipokucha, Wayahudi walifanya kikao cha faragha. Wakala kiapo: "Hatutakula wala kunywa mpaka tutakapokuwa tumekwisha muua Paulo."
13Tokią sankalbą padarė daugiau negu keturiasdešimt žmonių.
13Watu zaidi ya arobaini ndio waliokula njama kufanya hivyo.
14Jie nuėjo pas aukštuosius kunigus bei vyresniuosius ir pasakė: “Mes siekte prisiekėme nieko neragauti, kol nužudysime Paulių.
14Basi, walikwenda kwa makuhani wakuu na wazee, wakasema, "Sisi tumeapa kwamba hatutaonja chochote kwa vinywa vyetu mpaka hapo tutakapokuwa tumemuua Paulo.
15Todėl dabar jūs kartu su sinedrionu prašykite tribūną, kad jis pristatytų jį jums rytoj, lyg norėtumėte tiksliau ištirti jo bylą. Tuo tarpu mes būsime pasiruošę užmušti jį kelyje”.
15Sasa basi, ninyi pamoja na Baraza tumeni ujumbe kwa mkuu wa jeshi ili amlete Paulo kwenu mkijisingizia kwamba mnataka kupata habari kamili zaidi juu yake. Tuko tayari kumuua hata kabla hajafika karibu."
16Apie šį suokalbį nugirdo Pauliaus sesers sūnus. Jis atėjo į kareivines ir pranešė Pauliui.
16Lakini mtoto wa kiume wa dada yake Paulo alisikia juu ya mpango huo; hivyo akaenda ndani ya ngome, akamjulisha Paulo juu ya njama hiyo.
17Tada Paulius, pasivadinęs vieną šimtininką, paprašė: “Nuvesk šį jaunuolį pas tribūną. Jis turi jam kai ką pranešti”.
17Hapo Paulo akamwita mmoja wa askari, akamwambia, "Mchukue kijana huyu kwa mkuu wa jeshi; ana kitu cha kumwambia."
18Tas, paėmęs jį, nuvedė pas tribūną ir paaiškino: “Kalinys Paulius pasišaukė mane ir paprašė, kad atvesčiau pas tave šitą jaunuolį. Jis turįs tau kai ką pasakyti”.
18Askari akamchukua huyo kijana, akamwongoza mpaka kwa mkuu wa jeshi, akasema, "Yule mfungwa Paulo ameniita akaniomba nimlete kijana huyu kwako kwa maana ana jambo la kukwambia."
19Tribūnas, paėmęs jį už rankos, pasivedė į šalį ir paklausė: “Ką turi man pranešti?”
19Mkuu wa jeshi alimshika huyo kijana mkono, akampeleka mahali pa faragha, akamwuliza, "Una nini cha kuniambia?"
20Tas atsakė: “Žydai susitarė prašyti tave, kad rytoj nuvestum Paulių į sinedrioną, neva norėdami tiksliau ištirti jo bylą.
20Yeye akasema, "Wayahudi wamepatana wakuombe umpeleke Paulo Barazani wakijisingizia kwamba Baraza lingependa kupata habari kamili zaidi juu yake.
21Netikėk jais! Nes jo tyko daugiau negu keturiasdešimt vyrų, kurie prisiekė nei valgyti, nei gerti, kol jį nužudys. Jie jau dabar pasiruošę ir laukia tavo sutikimo”.
21Lakini wewe usikubali kwa maana kuna watu zaidi ya arobaini walio tayari kumvamia. Wameapa kutokula wala kunywa mpaka watakapokuwa wamemuua. Sasa wako tayari, wanangojea tu uamuzi wako."
22Tribūnas atleido jaunuolį ir griežtai įsakė: “Niekam nesakyk, kad tu man tai pranešei”.
22Mkuu wa jeshi alimwacha aende zake akimwonya asimwambie mtu yeyote kwamba amemletea habari hizo.
23Pasišaukęs du šimtininkus, tribūnas pasakė: “Nuo trečios valandos nakties laikykite parengtyje žygiuoti į Cezarėją du šimtus kareivių, septyniasdešimt raitelių ir du šimtus ietininkų.
23Basi, mkuu wa jeshi aliwaita askari wawili akawaambia, "Wekeni tayari askari mia mbili, wapanda farasi sabini na askari mia mbili wa mikuki, waende Kaisarea; muwe tayari kuondoka kabla ya saa tatu leo usiku.
24Parūpinkite ir arklių, kad raitą Paulių saugiai nugabentų pas valdytoją Feliksą”.
24Wekeni farasi kadhaa kwa ajili ya Paulo; mfikisheni salama kwa Felisi, mkuu wa mkoa."
25Ir jis parašė tokio turinio laišką:
25Halafu mkuu huyo wa jeshi akaandika barua hivi:
26“Klaudijus Lisijas kilniausiajam valdytojui Feliksui siunčia sveikinimą.
26"Mimi Klaudio Lusia ninakuandikia wewe Mheshimiwa Felisi, mkuu wa mkoa. Salamu!
27Šitą vyrą žydai buvo nutvėrę ir norėjo nužudyti. Aš, atėjęs su kareiviais, jį išgelbėjau, sužinojęs esant Romos pilietį.
27"Wayahudi walimkamata mtu huyu na karibu wangemuua kama nisingalifahamishwa kwamba yeye ni raia wa Roma na hivyo nikaenda pamoja na askari nikamwokoa.
28Norėdamas patirti jo apkaltinimo priežastį, nuvedžiau jį į jų sinedrioną.
28Nilimpeleka mbele ya Baraza lao kuu nikitaka kujua kisa cha mashtaka yao.
29Radau, kad jis kaltinamas dėl jų Įstatymo klausimų, o ne dėl kokio nusikaltimo, baustino mirtimi ar kalėjimu.
29Niligundua kwamba mashtaka yenyewe yalihusu ubishi juu ya sehemu kadha wa kadha za Sheria yao na hivyo sikuona kwamba amefanya chochote kinachostahili auawe au afungwe gerezani.
30Kadangi man buvo pranešta apie žydų ruošiamą pasikėsinimą į šį vyrą, tai nedelsdamas siunčiu jį pas tave, nurodęs ir kaltintojams, kad jie tau pateiktų prieš jį turimus kaltinimus. Lik sveikas”.
30Nilipofahamishwa kwamba Wayahudi walikuwa wamefanya njama za kumuua, niliamua kumleta kwako. Nikamwambia washtaki wake walete mashtaka yao mbele yako."
31Kareiviai, vykdydami įsakymą, paėmė ir nugabeno nakčia Paulių į Antipatridę.
31Basi, hao askari walimchukua Paulo kama walivyoamriwa; wakampeleka usiku uleule mpaka Antipatri.
32Rytojaus dieną jie pasiuntė su juo raitelius, o patys sugrįžo į kareivines.
32Kesho yake askari wa miguu walirudi ngomeni, wakawaacha wale askari wapanda farasi waendelee na safari pamoja na Paulo.
33Anie, atvykę į Cezarėją, įteikė valdytojui laišką ir pristatė Paulių.
33Walipofika Kaisarea walimpa mkuu wa mkoa ile barua na kumweka Paulo chini ya mamlaka yake.
34Perskaitęs laišką, jis pasiteiravo, iš kokios provincijos tas esąs. Sužinojęs, kad iš Kilikijos,
34Felisi alipoisoma hiyo barua aliwauliza Paulo ametoka mkoa gani. Alipofahamishwa kwamba alikuwa ametoka mkoa wa Kilikia,
35jis pasakė: “Aš tave išklausysiu, kai atvyks tavo kaltintojai”. Ir liepė jį saugoti Erodo pretorijuje.
35akasema, "Nitasikiliza kesi yako baada ya washtaki wako kufika." Kisha akaamuru Paulo awekwe chini ya ulinzi ndani ya ukumbi wa Herode.