1Po penkių dienų atvyko vyriausiasis kunigas Ananijas su vyresniaisiais ir oratoriumi Tertulu. Jie pateikė valdytojui kaltinimus prieš Paulių.
1Baada ya siku tano, Kuhani Mkuu Anania aliwasili Kaisarea pamoja na wazee kadhaa na wakili mmoja wa sheria aitwaye Tertulo. Walimwendea yule mkuu wa mkoa wakamweleza mashtaka yao juu ya Paulo.
2Kai pastarasis buvo iškviestas, Tertulas pradėjo savo kaltinamąją kalbą: “Tavo rūpesčiu turėdami tikrą taiką ir didelę gerovę šitoje tautoje,
2Paulo aliitwa na Tertulo akafungua mashtaka hivi: "Mheshimiwa Felisi, uongozi wako bora umeleta amani kubwa na marekebisho ya lazima yanafanywa kwa manufaa ya taifa letu.
3mes, prakilnusis Feliksai, visuomet ir visur tai pripažįstame su didžiu dėkingumu.
3Tunalipokea jambo hili kwa furaha daima na kutoa shukrani nyingi kwako kila mahali.
4Nenorėdamas tavęs ilgiau gaišinti, prašau tave trumpai mūsų paklausyti su savo įprastu maloningumu.
4Lakini, bila kupoteza wakati wako zaidi, tunakusihi kwa wema wako, usikilize taarifa yetu fupi.
5Mes nustatėme šį žmogų esant tarsi marą. Jis kursto maištą viso pasaulio žydijoje ir yra nazariečių sektos vadeiva.
5Tumegundua kwamba mtu huyu ni wa hatari mno. Yeye huanzisha ghasia kati ya Wayahudi kila mahali duniani na pia ni kiongozi wa kile chama cha Wanazareti.
6Jis net mėgino išniekinti šventyklą. Štai kodėl jį suėmėme ir norėjome nuteisti pagal savąjį Įstatymą.
6Tena alijaribu kulikufuru Hekalu nasi tukamtia nguvuni. Kama ukimhoji wewe mwenyewe, utaweza kubainisha mambo haya yote tunayomshtaki kwayo." Tulitaka kumhukumu kufuatana na Sheria yetu.
7Bet tribūnas Lisijas su didele prievarta išplėšė jį iš mūsų rankų
7Lakini Lusia, mkuu wa jeshi, aliingilia kati, akamchukua kwa nguvu kutoka mikononi mwetu.
8ir liepė jo kaltintojams atvykti pas tave. Apie tai, kuo jį kaltiname, pats galėsi viską sužinoti, jį išklausinėjęs”.
8Kisha akaamuru washtaki wake waje mbele yako.
9Tiems žodžiams pritarė žydai, tvirtindami, kad taip esą iš tikrųjų.
9Nao Wayahudi waliunga mkono mashtaka hayo wakisema kwamba hayo yote yalikuwa kweli.
10Valdytojui davus ženklą, Paulius atsakė: “Žinodamas tave jau daug metų esant šios tautos teisėju, drąsiai ginsiu savo bylą.
10Basi, mkuu wa mkoa alimwashiria Paulo aseme. Naye Paulo akasema, "Nafurahi kujitetea mbele yako nikijua kwamba umekuwa hakimu wa taifa hili kwa miaka mingi.
11Tau nesunku nustatyti, jog praėjo ne daugiau kaip dvylika dienų, kai atvykau į Jeruzalę pagarbinti.
11Unaweza kujihakikishia kwamba si zaidi ya siku kumi na mbili tu zimepita tangu nilipokwenda kuabudu Yerusalemu.
12Ir niekas manęs nematė su kuo nors besiginčijant šventykloje nei suburiant minią sinagogose ar mieste.
12Wayahudi hawakunikuta nikijadiliana na mtu yeyote. Hawakunikuta nikichochea watu Hekaluni wala katika masunagogi yao, wala mahali pengine popote katika mji huo.
13Jie negali įrodyti to, kuo dabar mane kaltina.
13Wala hawawezi kuthibitisha mashtaka waliyotoa juu yangu.
14Bet aš tau išpažįstu, jog tarnauju savo tėvų Dievui pagal Kelią, jų vadinamą sekta, tikėdamas visa, kas parašyta Įstatyme ir Pranašuose,
14Ninachokubali mbele yako ni hiki: Mimi ninamwabudu Mungu na wazee wetu nikiishi kufuatana na Njia ile ambayo wao wanaiita chama cha uzushi. Ninaamini mambo yote yaliyoandikwa katika vitabu vya Sheria na manabii.
15ir turiu viltį Dieve, kurią jie patys irgi pripažįsta, jog bus prisikėlimas iš numirusiųtiek teisiųjų, tiek neteisiųjų.
15Mimi namtumainia Mungu, na wao wanalo tumaini hilo, kwamba watu, wema na wabaya, watafufuka.
16Todėl stengiuosi visuomet turėti tyrą sąžinę prieš Dievą ir prieš žmones.
16Kwa hiyo ninajitahidi daima kuwa na dhamiri njema mbele ya Mungu na mbele ya watu.
17Aš po daugelio metų atkeliavau savo tautai atiduoti gailestingumo dovanų ir aukų.
17"Baada ya kukaa mbali kwa miaka kadhaa, nilirudi Yerusalemu ili kuwapelekea wananchi wenzangu msaada na kutoa dhabihu.
18Todėl kai kurie Azijos žydai rado mane apsivaliusį šventykloje be jokios minios ir be jokio triukšmo.
18Wakati nilipokuwa nikifanya hayo ndipo waliponikuta Hekaluni, nilipokuwa nimekwisha fanya ile ibada ya kujitakasa. Hakukuwako kundi la watu wala ghasia.
19Tai jiems reikėtų čia būti ir, jei ką turi prieš mane, kaltinti tavo akyse.
19Lakini kulikuwa na Wayahudi wengine kutoka mkoa wa Asia; hao ndio wangepaswa kuwa hapa mbele yako na kutoa mashtaka yao kama wana chochote cha kusema dhidi yangu.
20Pagaliau tegul ir šitie pasako, kokį nusikaltimą jie man įrodė, kai stovėjau prieš sinedrioną?
20Au, waache hawa walio hapa waseme kosa waliloliona kwangu wakati niliposimama mbele ya Baraza lao kuu,
21Nebent tik žodžius, kuriuos šaukiau, stovėdamas tarp jų: ‘Šiandien jūs mane teisiate už mirusiųjų prisikėlimą!’ ”
21isipokuwa tu maneno haya niliyosema niliposimama mbele yao: Mnanihukumu leo hii kwa sababu ya kushikilia kwamba wafu watafufuliwa!"
22Feliksas, gerai nusimanydamas apie tą Kelią, tai išklausęs, atidėjo skundo svarstymą, sakydamas: “Kai atvyks tribūnas Lisijas, tuomet ir išaiškinsiu jūsų klausimą”.
22Hapo, Felisi, ambaye mwenyewe alikuwa anaifahamu hiyo Njia vizuri, aliahirisha kesi hiyo. Akawaambia, "Nitatoa hukumu juu ya kesi hiyo wakati Luisa, mkuu wa jeshi, atakapokuja hapa."
23Jis davė nurodymą šimtininkui saugoti Paulių, tačiau daryti jam lengvatų ir niekam iš jo žmonių nedrausti jam patarnauti ar pas jį ateiti.
23Kisha akamwamuru yule jemadari amweke Paulo kizuizini, lakini awe na uhuru kiasi, na rafiki zake wasizuiwe kumpatia mahitaji yake.
24Po kelių dienų Feliksas atėjo su savo žmona Druzila, kuri buvo žydė. Jis liepė pakviesti Paulių ir išklausė jo apie tikėjimą Kristumi.
24Baada ya siku chache, Felisi alifika pamoja na mkewe Drusila ambaye alikuwa Myahudi. Aliamuru Paulo aletwe, akamsikiliza akiongea juu ya kumwamini Yesu Kristo.
25Pauliui dėstant apie teisumą, susilaikymą ir būsimąjį teismą, Feliksas išsigando ir tarė: “Šiam kartui užtenka. Gali eiti. Kai turėsiu laiko, tave pasišauksiu”.
25Lakini wakati Paulo alipoanza kuongea juu ya uadilifu, juu ya kuwa na kiasi na juu ya siku ya hukumu inayokuja, Felisi aliogopa, akasema, "Kwa sasa unaweza kwenda; nitakuita tena nitakapopata nafasi."
26Be to, jis tikėjosi, kad Paulius duos jam pinigų, jog jį išleistų, todėl dažniau jį kviesdavosi ir su juo kalbėdavosi.
26Wakati huohuo alikuwa anatumaini kwamba Paulo angempa fedha. Kwa sababu hii alimwita Paulo mara kwa mara na kuzungumza naye.
27Prabėgus dvejiems metams, Feliksą pakeitė įpėdinis Porcijus Festas. Norėdamas padaryti žydams malonumą, Feliksas paliko Paulių kalėjime.
27Baada ya miaka miwili, Porkio Festo alichukua nafasi ya Felisi, akawa mkuu wa Mkoa. Kwa kuwa alitaka kujipendekeza kwa Wayahudi, Felisi alimwacha Paulo kizuizini.